Ndoa yangu haina amani

Inategemea na aina ya mke, niliwahi kufulia japo mke wangu hakuwa na kipato kikubwa sana lakini alisimama imara mpaka hapa nilipo na sikusikia jambo lolote la kudhalilisha utu wangu.
Kwa wewe ulioa mke kweli na ulibahatika! Kwa hawa waliooa wanawake chuma ulete huwezi kueleweka siku mishe zikibuma!
 
Mkuu hi ilishanitokea,nilichofanya nikakopaa mtaji kwa baadhi ya watu wangu wakaribu.....kimya kimya nikafungua kibiashara,akawa anaona natoka asubui na Rudi usiku,nikaaza kulipaa bills zote,hapo hatushemedhani ikaenda nikasimama kuja kugundua na biashara akaaza kujirudi,nikaona hapa ndo penyeweeee nilikuwaaa nampelekeaaa motoo mzee baba,nikiwa juu ya kifua namkumbukaa yalee masimango naongezaaa kupeleka Moto mwisho wa siku Hadi hela zakee akaanza kuletaaa kwangu
Hapo ulikaza balaa mzee baba😀 kilume ndago!
 
Story kama hii sikia tu kwa mwenzio,pole sana mkuu kwa unayopitia,sio kwa nia mbaya lakini inaonesha wife ana mchepuko wake tayari anakutafutia sababu tu ya kuachana..
My Take:Achana nae kabla hajakuletea vituko vya wazi wazi
Natafuta pa kuanzia maisha mkuu ndio jambo kubwa kwangu kwa sasa
 
20210929_115631.jpg
 
Liverpool VPN njoo utoe ushauri huku

hawa viumbe hawasikii, wanazidi kuoa
Mkuu Liverpool VPN njoo umshauri jamaa

BTW anayewadanganyaga eti mke anaweza mlea mume ni nani?

Yaan kweli unaomba hela kwa mke ukaangalie mpira .....yaan bila aibu kabisa unaomba
Hawa watu wanachosha sasa...

Umefika muda tuwapige makonzi tu ili kubust akili zao.

Washaambiwa WASIOEEEE ila HAWASIKII.

Haloo brothers NDOA MAJANGA Msioeeee.

#YNWA
 
Amekusikia na tumekusikia Mkuu, nini kifanyike?
Mwanamke keshazaa naye watoto wawili.

Huyu ni Mke wake kabisaa halali ( ukishazaa na mwanamke watoto wawili watatu wala usiumize kichwa tena juu yake ).

Kwa sasa Jamaa, Ajikite kurudisha Thamani yake .

( kihalisia na kama mwanamke angekua Muumini wa Utu, kwa sasa ndio ulikua wakati sahihi wa kusimama na Jamaa, kumpa moyo, kumuombea na KUMFICHIA AIBU JAMAA MBELE ZA WATU)

sisi wanaume kuna ule wakat unataka utoke kidogo, ukae na masela ,n.k, ni wakat wa mwanamke kumwambia " Hubby leo kachamke na wenzako, pesa hii hapa "..

Badala yake mwanamke anazidi kumnyonga jamaaa, Huyu jamaa muda mfupi ujao, ataanza kuona giza, yaan hata kichwa kufunguka ,kitashindwa ..nandio mawazo mabaya mabaya yataanza kumuijiaa...Mke ana mtu .mke amanisaliti..kisa sina hela..kisa hiki....


Lkn niseme ,Toka awali kuna kitu alishakikosea kukitengeza nacho ni HESHIMA.


NDUGU ZANGU, LAZIMA IFIKE MAHALI MWANAMKE AKUHESHIMU PASIPO KUJALI KIPATO CHAKO.


PESA HUJA NA KUONDOKA..LKN UTI WA MTU UTAISHI MILELE NAMILELE MPAKA KUFA KWAKO.


hii inamaana ,Mwanamke mke wako. Lazima auheshimu UTU WAKO wakati wote wa Pesa au kutokua na Pesa.



Tuachane na hayo

Nini Jamaa afanye ???


Jamaa ni mjuzi wa biashara nandio sehem ya maisha yake, watu biashara hkua na kushuka lkn husimama nakuendelea ( niliwah kufungua kabishara nikamuweka Ndugu yangu, alikula mpaka mtaji ,kakafa kote)
Ila sikuacha..


kwakua ana nyumba, na mjuzi wa biashara , Akakope Pesa anayojua inatosha kabisa kuanzisha bishara

Ni vema pia asikae kimya, awashirikishe wazazi, na ndugu zake wa damu, mawazo yao nayake ,ataondoka na kitu ( shida ya wengi ni kukaa na mambo moyoni)

Jamaa asikaee kumfatilia mwanamke, asikae kumuomba kitu kwa mwanamke.

Aanze mapambano , yaan huyo Mwanamke , Dawa yake ni sio kumkimbia, sio kumfukuza sio kuachana naye sababu HAMNA BAYA LA KUFANYA IVO ....LABDA KAMA KUNA USALITI ATAUFANYA KWA JAMAA , SABABU TU YA MAISHA YA JAMAA YA SASA.


Kuomba Mungu, kwa uwezo wetu ,kutoboa maisha ni kazi , unamuomba Mungu akupe njia na kubariki mikono yako.
 
Hongera kwa kuvuka kiunzi nami naamini nitavuka.

Niliwaza kama wewe pia kuna mtu wa karibu anaweza nikopesha kaniambia mpaka mwezi wa 10 tarehe za katikati .

mm nilitaka asinione ili ajue tofauti nikiwepo na nisipo kuwepo

ikishindikana maisha yakitengamaa naoawa wa pili
Usioe mke wa Pili ,,Kaka.

Unayo nafasi kubwa sanaaaa ya kurekebisha na maisha yakaendelea kua sawa.


Mimi kwenye kutengana, huwa nashaur mtu aachane na mwanamke km amesalitiwa na amejua.
 
Inategemea na aina ya mke, niliwahi kufulia japo mke wangu hakuwa na kipato kikubwa sana lakini alisimama imara mpaka hapa nilipo na sikusikia jambo lolote la kudhalilisha utu wangu.
Hili ndio mimi nalisemea .


HONGERA SANA MKUU, WEE UNA MKE ALIYETOKA MBINGUNI KWA BABA MUNGU.
 
HIVI GUYS NI WAPI MNAFELI???

WAPI MNAKWAMA NDUGU ZANGU???

KWANN MNAKUA IVI LAKINI???

KWANN HAMNA UANAUME ???

WHY?? YAAAN UUZE NYUMBA YA WATOTO WAKO????


YAANI UUKIMBIE MJI WAKO ULOUJENGA KWA JASHO LAKO????


ET MIAKA KUMI, ALAFU NIWE NA FARAJA.. UNADHAN MAISHA NIKM RAMAN YA NYUMBA????

JE UKIENDA HUKO ALAFU USIFANIKIWE HIYO MIAKA YOTE KUMI??

NDO URUDI UKUTE KESHAZALISHWA ???


AU MNAONGEAGA TU KUPIGISHA WATU STORI???


HIVI KUNA WANAUME MNARUHUSU MATESO YAWAPATE NAMNA HII???


NIKISEMA NIWATUSI ,MNASEMA NAWALUGHA MBAYA.


MNATIA HASIRA SANA!!!!


NIKWAMBA HAYO NI MADAWA NDO MNAFANYIWA ????



MNAKERA SANA MAZEEE, MNAKERA MNOOOOO, YAAN MNANYANYASWA NA WANAWAKE , WANAWAKE MLOWAOKOTA MAHALI, UKAMUOA, UKAMPA HESHIMA, AKAONEKANA MWANAMKE, UMAPA MRADI, ET KISA UMEKWAMA NAYEYE KAINUKA NDO BASI AKUTESE ??????
Nimejiuliza maswali kama yako mkuu, nikaaandika aa weeeee afu nikafuta, yaani
 
Ukweli nimechoka nahitaji kusafiri mbali na nyumbani kwangu kila mtu aishi maisha yake maana tunakaa muda wote kama mtu na mke mwenza.

Ndoa yangu ina miaka 5 tuna watoto 2. Nilikuwa nafanya Biashara vizuri nikafanikiwa kujenga nyumba ya Familia na kumfungulia wife biashara naye ili asinitegemee kila kitu.

Bahati mbaya biashara yangu ikayumba nikawa nakomaa nayo ila yeye muda wote ni kunikatisha tamaa niachane nayo.
Nikapata dharura ya kusafiri kwanda mkoani kwa wazazi nikamwacha kijana.

Huku nyuma wife akamsonga songa kijana mwisho Biashara yangu ikafugwa nikapigiwa simu na wife kijana anaingiza hasara nimefunga.

Niliporejea home uzi ni ule ule anataka niachane nayo. Kweli nikaamua kuachana nayo kwani kodi ya pango iliisha na pia palifugwa wateja wangekuwa wametuhama zaidi hivyo nikilazimisha naweza tengeneza hasara na madeni
nikahitimisha kufunga Rasmi.

Niko zangu home najipanga kutafuta mishe ya kufanya wife ndiye mwenye kazi ndiye kila kitu kinacho husiana na hela. Manyanyaso yakaanzia hapa,
kelele, kupangiwa anachotaka.

Jumamosi ya ngao jamii kati ya Simba na Yanga niliomba Elfu mbili tu nikakae kwenye kibanda umiza niangalie mechi nilitolewa nje.

Siku hiyo nilishinda home kuna kazi nilikuwa nafanya. Nilichoka kweli,
basi nikajirudia zangu home saa 18:00 kujilalia saa tatu na nusu akawa anaingia. Alipofika akanyosha moja kwa moja kitandani. Nikauliza “wife hupiki?” maana njaa inauma. Akasema sipiki na sijakununulia chochote tutakula kesho. Kila nikimwongelesha kimya basi kuepusha shari nikakaa kimya nikalala japo usingizi wa tabu uchovu + njaa + mawazo

Kuanzia siku hiyo ni kununiwa hakuna kusemeshana. Nimewaza niuze nyumba nipate mtaji naona ugumu biashara zikigoma.

Wazo langu kwa sasa kwa sababu sina thamani kwake niondoke nikatafute maisha mbali ata miaka 10 ili nipate amani na faraja. Nahofia nitakufa bure na mawazo naye abaki na amani yake anilelee tu wanangu.
Pole sana
Nyakati zingine sie wanawake kweli mtihani
 
Back
Top Bottom