Ndoa ya CCM-CUF Visiwani: Ishara ya CUF kuwa 'CCM-B' huku Bara

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Tangu hatua za kwanza za kutaka maridhiano kati ya CCM na CUF kule Visiwani zilipoanza nimekuwa najiuliza: Jee maridhiano haya yakizaa srikali ya umoja wa kitaifa kule Visiwani uhusiano wa vyama hivyo viwili huku Tanzania Bara utakuwaje? Utaendelea kuwa na ushindani wa jino kwa jino kama ilivyokuwa hapo zamani au huku Bara CUF nayo itabidi ipunguze makali yake dhidi ya chama tawala na hivyo kujipa label ya u-CCM B?

Mimi naona hili ni jambo la msingi kulitafakari kwani huo u-CCM B ninaousema unaanza kujitokeza hasa ukizichunguza kauli za Katibu Mkuu wa CCM – Yusuf Makamba hivi majuzi – akiisifia CUF na kukiponda Chadema.
Wasiwasi wangu ni kwamba CCM wanaweza kuwatumia viongozi wa CUF katika kudhoofisha kampeni za Chadema hasa zile zitakazolenga kuwapo kwa ufisadi uliokithiri katika serikali ya CCM.

Na hili siyo la kuhisi kwani tulishaona huko nyuma jinsi Prof Lipumba alivyokuwa akitoa kauli za kutetea masuala ya ufisadi kama vile kuungana na akina Mkuchika na Sofia Simba kuzipinga kauli la Mengi pale alipowataja mafisadi papa (ambao wengine tayari wako mahakamani wakijibu kesi za ufisadi), na hali kadhalika kuuunga mkono wazo kwamba serikali inunue mitambo ya Dowans iliyoingizwa nchini kutokana na kashfa ya Richmond.

Swali langu ni jee – huku Bara CUF itakubali kupiga ‘zumari namba 2’ (second fiddler) kwa niaba ya CCM?
 
Kafu kwisha,kama kule jikoni kumekwisha itakuwa huku matawini? kafu iko zanzibar bro,huku ng`ambo ni bendera fuata upepo.:A S shade:
 
Tangu hatua za kwanza za kutaka maridhiano kati ya CCM na CUF kule Visiwani zilipoanza nimekuwa najiuliza: Jee maridhiano haya yakizaa srikali ya umoja wa kitaifa kule Visiwani uhusiano wa vyama hivyo viwili huku Tanzania Bara utakuwaje? Utaendelea kuwa na ushindani wa jino kwa jino kama ilivyokuwa hapo zamani au huku Bara CUF nayo itabidi ipunguze makali yake dhidi ya chama tawala na hivyo kujipa label ya u-CCM B?

Mimi naona hili ni jambo la msingi kulitafakari kwani huo u-CCM B ninaousema unaanza kujitokeza hasa ukizichunguza kauli za Katibu Mkuu wa CCM – Yusuf Makamba hivi majuzi – akiisifia CUF na kukiponda Chadema.
Wasiwasi wangu ni kwamba CCM wanaweza kuwatumia viongozi wa CUF katika kudhoofisha kampeni za Chadema hasa zile zitakazolenga kuwapo kwa ufisadi uliokithiri katika serikali ya CCM.

Na hili siyo la kuhisi kwani tulishaona huko nyuma jinsi Prof Lipumba alivyokuwa akitoa kauli za kutetea masuala ya ufisadi kama vile kuungana na akina Mkuchika na Sofia Simba kuzipinga kauli la Mengi pale alipowataja mafisadi papa (ambao wengine tayari wako mahakamani wakijibu kesi za ufisadi), na hali kadhalika kuuunga mkono wazo kwamba serikali inunue mitambo ya Dowans iliyoingizwa nchini kutokana na kashfa ya Richmond.

Swali langu ni jee – huku Bara CUF itakubali kupiga ‘zumari namba 2' (second fiddler) kwa niaba ya CCM?


Zak: Ni suala gumu kulitafakari na kupata jibu lililo sahihi -- ingawa kila dalili zaonyesha kuwa huku bara uhasama kati ya CCM na CUF utapungua sana na ninathubutu kusema kwamba CCM sasa itaiona CUF siyo tishio tena kama zamani. Hali hii inasikitisha sana kwa huku Bara ambako mara mbili 2000 na 2005 CUF ilikuwa nambari 2 kwa kuzoa kura za urais huku bara. Ushindani ulikuwa mkubwa hasa 2005 pale hadi CUF waliposusia kutangazwa na NEC matokeo ya kura ya urais (Chadema walihudhuria) Diamond Jubilee Hall. Sidhani iwapo hali ya ushindani wa namna hii baina ya vyama hivi viwili itatokea tena.

Jinsi CCM ilivyoi-neutralise CUF kule Visiwani kutaathiri sana harakati za chama hicho huku Bara! Tena sana.
 
Yamani hebu tujiulize CUF ina kiti gani cha Ubunge Bara.Wazanzibari wao wamekiunga mkono kwa hali na mali hata kupoteza maisha yao kwa CUF sasa tujiulize Bara tuna nini na wakaazi wa Bara wanafikiria nini JE? tunahitaji UKOMBOZI kama Wazanzibar au tuendelee hali halisi ? naamini CUF itaendelea kuwa tishio kwa CCM Bara.
 
Swali langu ni jee – huku Bara CUF itakubali kupiga ‘zumari namba 2' (second fiddler) kwa niaba ya CCM?

Zak huu ni ukweli mchungu kuukubali lakini ndio hali halisi. Ili kudhoofisha nguvu ya Dr. Slaa, CCM itaitumia CUF kuibomoa Chadema kwa kifanya CUF ni mshirika na the common enemy sasa atakuwa Chadema.

Kwa kuanzia, CUF itagomea ushirikiano wa aina yoyote na Chadema. Hii ndio mbinu kuu iliotumiwa siku zote, wagawe uwatawale. CCM inahakikisha inazigawanya kura za upinzani na benefishary ni yeye, kama vilivyo vita vya panzi.

Nawashauri Chadema, hata kama CUF itawagomea ushirikiano wa aina yoyote, Chadema isisimamishe mtu urais wa Zanzibar, ama kwenye CUF strong hold.

Mpaka sasa, suala la mgombea mwenza wa Chadema, bado ni pasua kichwa.
 
Swali langu ni jee – huku Bara CUF itakubali kupiga ‘zumari namba 2’ (second fiddler) kwa niaba ya CCM?

Zak huu ni ukweli mchungu kuukubali lakini ndio hali halisi. Ili kudhoofisha nguvu ya Dr. Slaa, CCM itaitumia CUF kuibomoa Chadema kwa kifanya CUF ni mshirika na the common enemy sasa atakuwa Chadema.

Kwa kuanzia, CUF itagomea ushirikiano wa aina yoyote na Chadema. Hii ndio mbinu kuu iliotumiwa siku zote, wagawe uwatawale. CCM inahakikisha inazigawanya kura za upinzani na benefishary ni yeye, kama vilivyo vita vya panzi.

Nawashauri Chadema, hata kama CUF itawagomea ushirikiano wa aina yoyote, Chadema isisimamishe mtu urais wa Zanzibar, ama kwenye CUF strong hold.

Mpaka sasa, suala la mgombea mwenza wa Chadema, bado ni pasua kichwa.
 
CCM wana hesabu sana, wamejua hawawezi kuiba kura election after election, wamekuja na insurance policy, wakishindwa uchaguzi na kuiba kura angalau wanakuwa katika serikali ya mseto.

CUF walikuwa katika a tough situation, wakikataa mseto wanaweza kushindwa uchaguzi, au hata kushinda halafu kugeuziwa mchezo kama chaguzi zilizopita.

Wakikubali mseto maana yake hata wakishinda hawawezi kupata uongozi wa peke yao.

At the end of the day idea ya mseto ina make sense, kwa sababu ukiwa na situation ya 49% against 51% kuwa na a winner takes all ni kualika migogoro mitupu. Ila naona kama CUF wamekuwa shortchanged kwa sababu hii kitu ilitakiwa iwepo tangu day one ili kuwa fair.

But hey, who said the world was a fair place.
 
Wakati mwingine huwa nikisoma baadhi ya post huwa nacheka tu...Maana wakati ule CUF ilipokuwa kweli Jino kwa Jino...baadhi ya watu wakabrand chama cha Vurugu....!!!

Sasa aproach imebadilika, kinaonekana CCM-B....i like it...!!!

Pasco... suala la Muungano wa CUF na Chadema halipo. kama sehem CUF hawana mgombea watawaunga Mkono chadema, the same Chadema kama hawana Mgombea sehem watawaunga mkono CUF....!!!...

..CCM hawana muda kuwatumia CUF wala muda kuwatumia Chadema...kwao wao mpinzani ni mpinzani...!! hizi assumption za Wapambe ni zao wao wenyewe kujitengenezea Taswira ya paka wakati hayupo.

By the way CUF ni wazoefu na wana uvumilivu ktk SIASA.
 
Wakati mwingine huwa nikisoma baadhi ya post huwa nacheka tu...Maana wakati ule CUF ilipokuwa kweli Jino kwa Jino...baadhi ya watu wakabrand chama cha Vurugu....!!!

Sasa aproach imebadilika, kinaonekana CCM-B....i like it...!!!

Pasco... suala la Muungano wa CUF na Chadema halipo. kama sehem CUF hawana mgombea watawaunga Mkono chadema, the same Chadema kama hawana Mgombea sehem watawaunga mkono CUF....!!!...

..CCM hawana muda kuwatumia CUF wala muda kuwatumia Chadema...kwao wao mpinzani ni mpinzani...!! hizi assumption za Wapambe ni zao wao wenyewe kujitengenezea Taswira ya paka wakati hayupo.

By the way CUF ni wazoefu na wana uvumilivu ktk SIASA.


Kwenye red: Lakini CCM wakibanwa sana katika uchaguzi na hasa wakiona chama kimoja ni tishio kubwa kwake huamua kutumia vyama vingine vidogovidogo -- angalau katika kutoa vocal support. Hii imefanyika sana huko nyuma, kwani tumeona viongozi wa baadhi ya vyama hivyo wakitoa kauli za kuwaponada viongozi wa chama tishio kwa CCM. haiwezekani CCM haina mkono hapo.

Kuhusu uzoefu wa uvumilivu wa CUF -- hujasema kama hii ni kitu negative au positive kwa CCM (au hata kwa CUF yenyewe). Lakini bila shaka ni positive kwa CCM kwani ukichukulia kule Visiwani, viongozi wa CCM wamekuwa wakila nchi kwa miaka 15 sasa, bila ya uhalali wowote (wakiwa wanapora ushindi) huku CUF wakifanya uvumilivu. Bahati hawakuamua kuingia msituni!
 
hili liko wazi kwani hata sasa cuf wamekua upande wa ccm zaidi ktk mambo mengi, nadhan financial support ndio driving factor ktk hilo!
 
Back
Top Bottom