Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Tangu hatua za kwanza za kutaka maridhiano kati ya CCM na CUF kule Visiwani zilipoanza nimekuwa najiuliza: Jee maridhiano haya yakizaa srikali ya umoja wa kitaifa kule Visiwani uhusiano wa vyama hivyo viwili huku Tanzania Bara utakuwaje? Utaendelea kuwa na ushindani wa jino kwa jino kama ilivyokuwa hapo zamani au huku Bara CUF nayo itabidi ipunguze makali yake dhidi ya chama tawala na hivyo kujipa label ya u-CCM B?
Mimi naona hili ni jambo la msingi kulitafakari kwani huo u-CCM B ninaousema unaanza kujitokeza hasa ukizichunguza kauli za Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba hivi majuzi akiisifia CUF na kukiponda Chadema.
Wasiwasi wangu ni kwamba CCM wanaweza kuwatumia viongozi wa CUF katika kudhoofisha kampeni za Chadema hasa zile zitakazolenga kuwapo kwa ufisadi uliokithiri katika serikali ya CCM.
Na hili siyo la kuhisi kwani tulishaona huko nyuma jinsi Prof Lipumba alivyokuwa akitoa kauli za kutetea masuala ya ufisadi kama vile kuungana na akina Mkuchika na Sofia Simba kuzipinga kauli la Mengi pale alipowataja mafisadi papa (ambao wengine tayari wako mahakamani wakijibu kesi za ufisadi), na hali kadhalika kuuunga mkono wazo kwamba serikali inunue mitambo ya Dowans iliyoingizwa nchini kutokana na kashfa ya Richmond.
Swali langu ni jee huku Bara CUF itakubali kupiga zumari namba 2 (second fiddler) kwa niaba ya CCM?
Mimi naona hili ni jambo la msingi kulitafakari kwani huo u-CCM B ninaousema unaanza kujitokeza hasa ukizichunguza kauli za Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba hivi majuzi akiisifia CUF na kukiponda Chadema.
Wasiwasi wangu ni kwamba CCM wanaweza kuwatumia viongozi wa CUF katika kudhoofisha kampeni za Chadema hasa zile zitakazolenga kuwapo kwa ufisadi uliokithiri katika serikali ya CCM.
Na hili siyo la kuhisi kwani tulishaona huko nyuma jinsi Prof Lipumba alivyokuwa akitoa kauli za kutetea masuala ya ufisadi kama vile kuungana na akina Mkuchika na Sofia Simba kuzipinga kauli la Mengi pale alipowataja mafisadi papa (ambao wengine tayari wako mahakamani wakijibu kesi za ufisadi), na hali kadhalika kuuunga mkono wazo kwamba serikali inunue mitambo ya Dowans iliyoingizwa nchini kutokana na kashfa ya Richmond.
Swali langu ni jee huku Bara CUF itakubali kupiga zumari namba 2 (second fiddler) kwa niaba ya CCM?