Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Ndoa: Majanga ya wanawake waliosomea shule za Boarding

Status
Not open for further replies.

Majaribu2013

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
952
Reaction score
1,050
#Majanga

Ukitaka kuona ndoa ya blue haya sasa uoe mwanamke ambaye maisha yake yote yalikuwa ni kwenye shule za boarding, chekechea boarding, primary boarding, secondary boarding, a level boarding, chuo kikuu boarding.

Yaani ndani hawajui lolote, wachafu wa mazingira ya ndani, hawajui kupika vyakula vyote na vya kwenye 6X6 kiujumla hawafai. yaani anaweza akaacha vyombo vichafu mlangoni mpaka jioni viko palepale tu halafu wavivu muda mwingi ni kusinzia tu.

hebu na wengine toeni egisipiriensi yenu.
 
Lakini huko boarding mabinti huwa wanapeana maujanja aisee.
 
#Majanga

Ukitaka kuona ndoa ya blue haya sasa uoe mwanamke ambaye maisha yake yote yalikuwa ni kwenye shule za boarding, chekechea boarding, primary boarding, secondary boarding, a level boarding, chuo kikuu boarding.

Yaani ndani hawajui lolote, wachafu wa mazingira ya ndani, hawajui kupika vyakula vyote na vya kwenye 6X6 kiujumla hawafai. yaani anaweza akaacha vyombo vichafu mlangoni mpaka jioni viko palepale tu halafu wavivu muda mwingi ni kusinzia tu.

hebu na wengine toeni egisipiriensi yenu.
Huyo atakuwa ni tabia yake tu mbaya ya uvivu na uchafu na pia labda boarding za siku hizi tena baadhi ya shule chache sana ambazo nasikia watoto hawafanyi kazi yoyote. Lakini kwa boarding tulizosoma sisi enzi zetu!!!!! thubutu!!!! Unafanya kazi hata nyingine nyumbani hazipo!!! Mnafundishwa kulima, kutafuta kuni, kusafisha mabanda ya ng'ombe, kukatia ng'ombe majani nk.
 
Kweli wanawake hao ni majanga ya kufa mtu,ni wavivu kupindukia,wachafu hakuna mfano
 
Labda ninyi mlozaliwa kwenye utawala wa mzee Ben na baba Riz...Enzi za mwalimu hakukua na boarding za chekechea...kulikua na darasa la kwanza hadi la nne then middle school!
 
lakini ni ukweli kwamba waliosoma boarding schools toka wako wwadogo primary school huwa hawajui house works kabisa. mambo ya kufagia sijui kuosha vyomb sijui kufua kwao yamewapitia kushoto na si wa kike tu hata wa kiume.

sasa atauaje ilihali shulen wanafuliwa kwa mashine, msosi wanapikiwa usafi wanafanyiwa, akifunga shule akija hme kuna madada 3 wa kazi, yy kazi yake ni kuangaia muvi, kuskiliza mziki, kuchat kwenye sosho media na kulala unategemea nini??
 
Majaribu huyo na tafiti zake

Boarding gani unazozungumzia wewe.........labda boarding sa siku hizi

sio zile za enzi hizo tulizosoma sie...

Umeona ee?
yani mi nimejiuliza wale wa boarding ambao unaamka saa 11 na huwezi kuacha kuoga,unakua na sehemu ya kufanya usafi asubuhi,time management inakuwepo hata usipopenda,muda wa ibada lazima uende,shamba kwa sana,hakuna kuvaa nguo za nyumbani(wengine ndo hadi viatu viraba),chakula utajifunza kula chochote(maharage unatoa wale wadudu kwa juu lol)...unajikuta maisha unaweza ishi popote
ngachoka kabsa!
hizi research hizi.
 
Labda ninyi mlozaliwa kwenye utawala wa mzee Ben na baba Riz...Enzi za mwalimu hakukua na boarding za chekechea...kulikua na darasa la kwanza hadi la nne then middle school!

hahahaha, umenichekesha sana sana...............nimemkumbuka baba ghafla.
watoto wa siku hizi sisi wazazi ndio tumeaharibu kwa kujidai tunawapa raha ya maisha kumbe hovyo kabisa.

Jana kuna kijana mmoja alinipigia simu akanishtakia jambo nilicheka sana moyoni mwangu, ni kijana wa 27 na ana gf ambaye anataka kumchumbia sasa kwa muda wote aliokaa na huyo gf wa miezi 6 kila akienda kumtembelea gf wanakula hotelini home hakupikwi, lkn kila mdada anapokuja kumtembelea kidume anakuta kidume kapika msosi fresh na binti anakula na kufurahia menu tamu. sasa mie nikamuuliza kwann binti hapiki?? akadai binti anasema hapendi kupika nikamuulza wewe uliamuaje?? akasema alimlazimisha siku moja ampikie ugali basi binti alichofanya alienda kununua ugalai wa mama ntilie akautia kwenye poti kisha akanunua na mboga. kijana alipofika akatengewa vizuri kwenye sahan sasa akashangaa mbona msosi wenyewe kama vile ugali mbichi manake sasa umejaa maji akamwambia binti huu ugali ni mbichi ngoja tuupike tena uive vzr binti alianza kujiuma uma kumbe hata kusonga ugali hajui................. mkaka wa watu ikabidi aairishe kula akaondoka kwa hasira.
 
Jamani hivi bado wiki ya chambuchambu kwa wanawake haijaisha??
 
Umeona ee?
yani mi nimejiuliza wale wa boarding ambao unaamka saa 11 na huwezi kuacha kuoga,unakua na sehemu ya kufanya usafi asubuhi,time management inakuwepo hata usipopenda,muda wa ibada lazima uende,shamba kwa sana,hakuna kuvaa nguo za nyumbani(wengine ndo hadi viatu viraba),chakula utajifunza kula chochote(maharage unatoa wale wadudu kwa juu lol)...unajikuta maisha unaweza ishi popote
ngachoka kabsa!
hizi research hizi.

ww unaongelea boarding ambazo ulisoma miaka ya <2005 sasa boarding hizi za >2005 ni majanga matupu. na hata wale watt waliosoma primary boarding miaka hiyo nao pia wali lack skills hasa za house works. mie nilisoma boarding toka form 1-6 lkn enzi zile weruweru ilikuwa weruweru kweli manake tulikuwa tunaosha hadi migongo ya ng'ombe. chezeya kilimo wewe...................
 
ww unaongelea boarding ambazo ulisoma miaka ya <2005 sasa boarding hizi za >2005 ni majanga matupu. na hata wale watt waliosoma primary boarding miaka hiyo nao pia wali lack skills hasa za house works. mie nilisoma boarding toka form 1-6 lkn enzi zile weruweru ilikuwa weruweru kweli manake tulikuwa tunaosha hadi migongo ya ng'ombe. chezeya kilimo wewe...................

Sasa my dear ndio maana nikasema hii research haieleweki kabisaaa..mi pia nimegraduate post 2005
alitakiwa basi afanye hata sampling(time,aina ya shule,etc) maana ipo too general.
 
Umeona ee?
yani mi nimejiuliza wale wa boarding ambao unaamka saa 11 na huwezi kuacha kuoga,unakua na sehemu ya kufanya usafi asubuhi,time management inakuwepo hata usipopenda,muda wa ibada lazima uende,shamba kwa sana,hakuna kuvaa nguo za nyumbani(wengine ndo hadi viatu viraba),chakula utajifunza kula chochote(maharage unatoa wale wadudu kwa juu lol)...unajikuta maisha unaweza ishi popote
ngachoka kabsa!
hizi research hizi.

unakumbuka yale maisha ......kule ilikuwa full mkimbizano.hakuna kuremba wala nini..mi nilisomaga na wadada

fulani wakawa wanajifanya High class mashauzi mengi baada ya muda mbona waliisoma namba..

na wakawa wachapakazi kuliko hata sie wengine

hizo boarding ni za siku hizi bana,,sie wa enzi zile tunaelewa
 
ww unaongelea boarding ambazo ulisoma miaka ya <2005 sasa boarding hizi za >2005 ni majanga matupu. na hata wale watt waliosoma primary boarding miaka hiyo nao pia wali lack skills hasa za house works. mie nilisoma boarding toka form 1-6 lkn enzi zile weruweru ilikuwa weruweru kweli manake tulikuwa tunaosha hadi migongo ya ng'ombe. chezeya kilimo wewe...................

alieweka thread angejaribu kutoa Time Frame......

ila yeye amegeneralise kila kitu
 
Majaribu huyo na tafiti zake

Boarding gani unazozungumzia wewe.........labda boarding sa siku hizi

sio zile za enzi hizo tulizosoma sie...
binti yangu kasoma boarding kuanzia darasa la 5 mpaka sasa yupo form 2.
anaporudi home likizo, ndo anatupangia tule nini likizo yoote..... yeye ndo anajua lunch tutakula hiki na dinner tutakula hiki. siyo kupanga tu, na kupika pia. anapika siyo mchezo. Hii inatokana na mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana kuwa naye jikoni na kumfundisha kupika.
Usafi room kwake anafanya mwenyewe, hayo ya 6x6 siwezi kumsemea, lol!
sasa hizo shule za boarding ambazo wanasoma hao ambao yeye kamuoa sijui ni za wapi?
labda asingizie wazazi wa huyo binti aliyemuoa, siyo boarding school
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom