Majaribu2013
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 952
- 1,043
- Thread starter
- #41
Kaka nisamehe kidogo. Mimi sina dawa ya kuchua bali ni ya kunywa, hivyo ushauri wangu waweza ukawa mchungu kidogo. Naanza kwa kunukuu hayo maneno yako mwenyewe. Umekiri kuwa hakuna hata hamu ya hayo mengine!! Sijui weye ni mtoto mdogo au ni mtu mzima.
Mtoto hupatikana kwenye hayo mambo mengine!!! Bila hayo, hakuna mtoto labda wa kimaabara. Weye ndiyo kikwazo kaka. Huenda hata jamaa za kwako ndiyo wanamsimanga mtoto wa watu. Acha kusikiliza vya pembeni. Kama weye ni mzima, mbegu zako saafi za afya, na yeye kadhalika, iweje usimpate huyo mtoto?
Amesha athirika kisaikolojia, sasa unatakiwa weye mwenyewe umwandae vizuuri kwa kumtoa out kidogo, mnunulie kanguo kazuuri sana ka ndani (kufuli) sio kwamba hana, lakini hili unamwambia ni very special kwake. Mpe ruhusa kuufungua moyo wake kwako. Haya hayaji kwa siku moja tu.
Taratibu, umwambie unampenda yeye kuliko chochote. Si mtoto wala mjukuu anaye zidi pendo lako kwake. Mthibitishie kuwa, hata kama hamtapata mtoto, yeye ndiye bora kwako. Akikuamini, utashangaa, ataanza kutaapika na kula udongo na embe changa sasa hivi.
Mwandae mkeo
Yaani huu ushauri ni afadhali hata ya punguani kukushauri maana umeongea out of topic kwa 100%! Kama hujaelewa somo bora kuacha tu kuliko kupoteza muda kijinga namna hii!:crying: