Ndoa inaelekea kunishinda

Mkuu kama kukuna mimi ni mwalimu. Maana hata hao wa nje wananililia kwasababu hiyo tu shida hawa watu wanatofautiana sana hasa katika afya zao hususan afya ya uzazi mwingine hainjoy mwingine ana enjoy. Nafikiri na mimi ndio msalaba wangu maana siku anaponikubalia anaenjoy sana ila ni kagoli kamoja hataki uludie na hapo zitapita 2week.
Sawa mkuu..tafuta sababu itakuwepo tu..sisi wanawake wakati mwingine tunashindwa pengine kuzungumza..yawezekana tusitumie maneno sahihi yakawaumiza na kuwaletea majeraha….tunaishia kukaa kimya mwisho wa siku ndo kama hivyo hajisikii kupiga game.

Kupiga au kupigwa game vizuri kunaleta furaha na kuongeza tumaini katika maisha😄😄

Lakini pia hata sisi wanawake madawa ya uzazi tunayotumia wengine huwa yanakataga stimu ya kupiga game kabisa.
 
Hata hivo shukuru mungu umepandishwa cheo kua mke wa ndoa,inaonekana wewe ndiyo ulikua namba moja kati yenu wanne
 
Vumilia wewe miezi sita ni mapema sana yanawezekana hata we bado hujaachana na Ex wako
 
Halafu kwanini anapekuwa pekuwa simu ya mwenzake?? Yaani wanawake huwa wanavitafuta vilio kwa makusudi kabisa. Ukisikia mwanamke mjinga huivunja ndoa yake kwa mikono yake ndio hivi sasa!
Halafu aje kumuomba samahani baada ya kumpatia gonjwa fulani ambalo halina tiba?
 
Ushauri wenu jamani mimi nimeolewa nipo kwenye ndoa hatujamaliza hata mwaka Ila kinachoniumiza mme Wangu ananisaliti, nimemkuta anamiliki simu ya Siri pamoja na line alikuwa kaficha kabatini baada ya kugombana naye akakubali kuwa ana mchepuko akampigia akaweka loud nikawa nawasikia akamuomba samahani kwa kumchezea akamwambia Mimi nimeoa, nina mke nmeona siyo vizuri kumsaliti mke wangu dada akalalamika we badae akakubali kumblock kidogo nikapata amani.

Baada ya hapo hiyo simu ya Siri akaweka mezani akatoka zake Ila kilichoniumiza zaidi baada ya lisaa zilikuwa zinaingia text kutoka no. tofauti tofauti 2 baada ya kuchart nao kumbe nao ni michepuko yake tena jumla nimemfuma na wanawake 3 kwa wakati mmoja.

Msamaha kaniomba Ila nashindwa kumsamehe, naumia sana Bora ningemkamata hata na mmoja nisingeumia sana Ila wa 3 ukitegemea ndoa haina hata mwaka nawaza sijui kalogwa, natamani nimshirikishe hata mchungaji wetu Ila napata wakati mgumu naona ni vitu vya aibu hata kushirikisha watu wetu wa karibu. Natamani niondoke Ila kinachonipa wakati mgumu tayari Mimi ni mjamzito yaani nawaza ingekuwa siyo hii mimba ningeachana nae ananifanya Hadi nakata tamaa na mimba niliyonayo kitu ambacho ni dhambi, Naombeni mnishauri nifanyaje nahisi kuchanganyikiwa nakosa maamuzi presha imeshuka naona Kama dunia imeniangukia kweli ndoa ni ngumu sana duh! Mungu anitie tu nguvu.
aisee

Mungu akutie nguvu.
 
Ni tusi la kizamani, zamani hatukuwa na haya matusi ya siku hizi! Mtu akizingua anakuwa mkuda, leo huambiwi mkuda...utaambiwa..ms***e!
Mimi mwenyewe mbibi..usishangae tulivyobadilisha na kukata ukali🤣🤣
 
Mimi naona kwahao watatu ndoujue hana.malengo nao hebu ona anahangaika nao mchana jioni anawaacha huko anakuja kwako wewe ndomshindi wanaume wengi tunavitabia vya hivo ila wakati mwingine kipato nitatizo ushauri wangu kama anakuhudumia vizuri .kasoro zaid yahiyo vumilia muombe mungu naumuombee hiyo ndoa itakuja kuwa tamu mengine acheni yatokee ili kuruhusu hatua inayofata
 
Back
Top Bottom