Thomas10
JF-Expert Member
- Mar 9, 2017
- 841
- 2,268
Habarini!
Ndoa ya ndugu yangu wa damu (kaka) imeingiliwa na kirusi hatarishi, maji yamezidi unga. Alimuoa binti (mke wake) kigori kabisa, na kwa utamaduni wetu, hili huwa tukio la heshima kwa muaji na waozeshaji (familia ya binti) pia.
Baada ya miaka sita ya furaha na huzuni, ndoa ya ndugu yangu imesimama wima, ikiwa na jumla ya watoto watatu, wakiume wawili na kabinti.
Kati ya watoto hao, mtoto mmoja (wa tatu) hafanani kabisa na watoto wengine, na hafanani na baba yake wala mama yakepia hafanani na yeyote katika familia yetu wala ya mwanamke.
Jambo hili lilimpa shaka bro, alijipa moyo lakini uafrika wetu ukamshinda. Maswali ya "mbona hafanani na sisi?" yalikuwa mengi, jambo lililomfanya bro aamue kutafuta suluhu ya nafsi yake.
Alianza kwa kupima DNA kwa Siri bila yeyote ndani ya familia kujua...majibu yakaonesha si wake (Tz)Akaenda nae Nairobi, huko akampima tena, ikaonesha si damu yake.
Kwa maelezo yake, anadai alienda kwa gwiji fulani huko Mombasa, nako akaambiwa si damu yake... Zaidi tena huko Mombasa, huyo mama (mganga) alimuonesha baba halisi wa mtoto yule
Bro alirudi kwake, akamkalisha kitako mke, akatumia maarifa na ujuzi wake wooote aliojaaaliwa kumshawishi mke amwambie chochote juu ya mtoto yule.
Japo lilikuwa jaribio gumu, lakini mke alikiri kuwa Moses, mtoto wa mwisho, si mtoto wa kaka. Na akamtaja baba yake halisi.
Picha iko hivi;
Shem katika makuzi yake, alikuwa na rafiki yake (mtoto mwenzake) ambaye walitengana baada ya familia ya huyo kijana kuhamia mkoa mwingine. Walipokua, walitafutana na wakaendelea kuwasiliana km wapenzi hadi shem alipoolewa.
Lakini licha ya kuolewa, mawasiliano yao yaliendelea na ahadi yao ilikuwa wazae mtoto mmoja ili iwe kumbukumbu ya mapenzi yao tangu utotoni na walipokuwa wakipata nafasi ya kukutana, basi walikuwa wananyanduana hadi mtoto huyo akapatikana..
Bro anataka kufanya maamuzi; ni moja tu kati ya mawili
1. Avunje ndoa au
2. Alinde ndoa
Binafsi km mshauri wa karibu, nimemshauri alinde ndoa. Kaniuliza KWANINI? Nimekosa jibu!
Ndoa ya ndugu yangu wa damu (kaka) imeingiliwa na kirusi hatarishi, maji yamezidi unga. Alimuoa binti (mke wake) kigori kabisa, na kwa utamaduni wetu, hili huwa tukio la heshima kwa muaji na waozeshaji (familia ya binti) pia.
Baada ya miaka sita ya furaha na huzuni, ndoa ya ndugu yangu imesimama wima, ikiwa na jumla ya watoto watatu, wakiume wawili na kabinti.
Kati ya watoto hao, mtoto mmoja (wa tatu) hafanani kabisa na watoto wengine, na hafanani na baba yake wala mama yakepia hafanani na yeyote katika familia yetu wala ya mwanamke.
Jambo hili lilimpa shaka bro, alijipa moyo lakini uafrika wetu ukamshinda. Maswali ya "mbona hafanani na sisi?" yalikuwa mengi, jambo lililomfanya bro aamue kutafuta suluhu ya nafsi yake.
Alianza kwa kupima DNA kwa Siri bila yeyote ndani ya familia kujua...majibu yakaonesha si wake (Tz)Akaenda nae Nairobi, huko akampima tena, ikaonesha si damu yake.
Kwa maelezo yake, anadai alienda kwa gwiji fulani huko Mombasa, nako akaambiwa si damu yake... Zaidi tena huko Mombasa, huyo mama (mganga) alimuonesha baba halisi wa mtoto yule
Bro alirudi kwake, akamkalisha kitako mke, akatumia maarifa na ujuzi wake wooote aliojaaaliwa kumshawishi mke amwambie chochote juu ya mtoto yule.
Japo lilikuwa jaribio gumu, lakini mke alikiri kuwa Moses, mtoto wa mwisho, si mtoto wa kaka. Na akamtaja baba yake halisi.
Picha iko hivi;
Shem katika makuzi yake, alikuwa na rafiki yake (mtoto mwenzake) ambaye walitengana baada ya familia ya huyo kijana kuhamia mkoa mwingine. Walipokua, walitafutana na wakaendelea kuwasiliana km wapenzi hadi shem alipoolewa.
Lakini licha ya kuolewa, mawasiliano yao yaliendelea na ahadi yao ilikuwa wazae mtoto mmoja ili iwe kumbukumbu ya mapenzi yao tangu utotoni na walipokuwa wakipata nafasi ya kukutana, basi walikuwa wananyanduana hadi mtoto huyo akapatikana..
Bro anataka kufanya maamuzi; ni moja tu kati ya mawili
1. Avunje ndoa au
2. Alinde ndoa
Binafsi km mshauri wa karibu, nimemshauri alinde ndoa. Kaniuliza KWANINI? Nimekosa jibu!