Tunasoma bossTunafatilia jmn sema wengi wapo kimya usitufanyie hivyo
Patashika nguo kuchanika 🔥 🔥 🔥Balaaa zito
Tunafatilia mkuu usiache kuleta
Daaaaah... Kama muvi hv yaan.... Asante sana mkuu
Yaani ni kisa kizuri sana mkuu... Yaani kuna funzo zuri sanaKaribu mkuu, tupo pamoja sana
Yaani ni kisa kizuri sana mkuu... Yaani kuna funzo zuri sana
Hadithi nzuriSEHEMU YA NANE: ANAYEPELEKWA NA MAJI HUFA AKICHEKA
PART 2
888888
NI MIEZI TISA SASA IMEISHA TANGU NIMFSHAMU CK. SIKU YA SIKU KUU YAKE YA KUZALIWA NILIJIPANGA KUMFANYIA SUPRISE. NILIANDAA KEKI YA NGUVU. KISHA NIKAANDA CHAMPAGNE NA KUMNUNULIA SURUALI NA SHATI KAMA APENDAVYO KUVALIA. NILIANDAA KILA KITU NA KWENDA PALE KWAKE JIONI NIKAWA NAMSUBIRI. NILIWEKA ZAWADI ZAKE VYEMA KWA AJILI YA SUPRISE. KEKI.. KADI NA NGUO HIZO. KISHA NIKAENDELEA KUMSUBIRI.SAA MOJA IKAPITA.. SAA MBILI KISHA SAA TATU USIKU BADO HAJAKUJA. NIKAMUWAZIA SANA ATAKUWA WAPI?HIVYO NIKAONA NITACHELEWA NA KUAMUA KUONDOKA. LAKINI ASBH SANA NILISEMA NITARUDI ILI KUMSUPRISE..NILIJIANDAA KWA AJILI YA KWENDA KAZINI. NA SIKUELEKEA KAZINI MOJA KWA MONA ILA NIKAAMUA SASA KWENDA KWA CK. NILIFIKA NI MAJIRA YA SAA KUMI NA MBILI ASBH. NILIMKUTA HARUNA GETINI NA ALINIAMBIA CK HAYUPO. NILIONA GARI NDANI ASIJUE NIMEONA GARI. KISHA NIKAMWAMBI okay basi acha niingie. ali ikataza pia. Nilimgombeza sana tena kwa nguvu mno. Lakini bado alinikataza. NILIMWAMBIA NITAINGIA LAZIMA. KWA VILE NILIKUWA NATUMIA KELELE NYINGI NI KAMA NILIWASUMBUA WALIOKUWA NDANI HIVYO MLINZI ALINIAMBIA NI BORA NIEMDE NIRUDI BADAE. NILIUMIA SANA MOYO WANGU. NA AKILI IKAVURUGIKA SASA NIKAAMUA KWENDA OFCN KWAKE. NILIFIKA OFCN KWAKE NIKAINGIA KWANI NILIRUBUSIWA. NA NILIPIGA SIMU YA CK YA NYUMBANJ HAIKUPOLELEWA. LAKINI NIKAAMUA KUMPIGIA MSHAURI WANGU ANIPE USHAURI.
MARA GHAFLA NAMPIGIA MAMA KELY NAAMBIWA HAJAFIKA KAZINI. NIKAPUUZA NA KUAMUA KUELEKEA KAZINI KWANGU. NIKIWA OFCN KWANGU SARA ALINIFUATA NA KUNIAMBIA DA FLORA MIMI KUNA KITU KINANIUMA NATAKA KUKUAMBIA.
NILIMWAMBIA NI NINI?
ALINIAMBIA NI SIRI ILA UWE MSIRI. NILIMSILILIZA KWA MAKINI. KISHA AKANIAMBIA NAOMBA UVUMILIE NIKIKUAMBIA.
Je no siri gani sarah atamwambia Florah???
Tukijaliwa kesho tutaijua.
Muwe na usiku mwema.
88888
SARA ALIONEKANA ANASHAUKU YA KUNIELEZA NA ALIKUWA KAMA ANAONEKANA KUSIKITKA SANA,, NILIMWAMBIA ANIACHE NIFANYE JAMBO FULANI KAZINI KISHA TUTAZUNGUMZA, NILIKUWA NIKIKUWAZA CK KWA NIN HAPATIKANI, KWA NINI GARI LIKO NDANI NA HAYUPO NI MOJA YA SIKU AMBAZO PIA AKILI YANGU ILIKUWA INAVURUGIKIWA,, NIKIWA NIMESHAMALIZA KUFANYA KAZI YANGU, NILIMIUTA SARA NA TULITOKA NA KWENDA KUSIMAMA KWENYE VERANDA YA OFC, HUKO TULIONGEA SANA NA MAONGEZI YETU YALKUWA HIVI…
Yani da Flora kuna kitu kinaniuma sana. Na sipendi namna ambayo Bite anafanya. Amekuwa akitoka na mumeo kitu ambacho sikifurahii kabisa na ni ukweli haswa. Na ninalila kitu cha kukuhakikishia.
Moyo ulinilipuka. Nilimuuliza sara
Una uhakika?Sara aliniambia ana uhakika na hata kama nataka kuhakikisha yuko tayari kufanya nihakikishe.
Nilitokwa na machozi kwa nini Bite anifanyie hivyo. Niliumia sana na kama kawaida sina wa kumuomba ushauri zaidi ya Mama kelly.
Nilimuuliza sara nifanyeje sasa huku nikiwa nimechanganyikiwa…Sara aliniambia kaa naye mbali ila naomba usimwambie nimekuambia mimi nimeshindwa kuvumilia. Lakini pia flors kuwa msiri na mambo yako. Sio wote wanafurahia kuona unapenswa na ck. Moyo uliniuma sana. Bite nilimpenda kama mdogo wangu. Nilimheshimu sana. Kwa nini anifanyie hivi. Nilikasirika na sasa nilitamani hata sijui kumfanya nini.
888888
NILIONDOKA NIKIWA KAMA NIMEPANICK. NILIENDA MOJA KWA MOJA OFCN KWA MAMA KELY. NIKIWA NAMSUBIRI KWANI HAKUWEPO NA NILIAMBIWA ATAKUJA ALIKUWA MA DHARURA.
NILIKAA OFCN KWAKE NA MFANYAKAXI MWENZAKE NIKIWA NAMSUBIRI. MUNGU WANGU!
Naota ama ni kweli?Sikuamini nilichokiona. Ni mama kely kwenye gari ya ck. Ck anamshusha mama kely na anawasha gari na kuondoka… moyo ulinilipuka. Mapigo ya moyo yalidunda kwa kasi. Sikuweza kuongea ila nilikuwa natetemeka… kumbe wenye pressure husumbuka sana… Nilikuwa nahindwa kupumua ipasavyo. Ni kama niliyekimbizwa sana na kichoka kwa kuhema. Pumzi zangu hazitoki sawa sawa…. kicha kiliniuma kama mishipa ya damu imebast… no ndani ya sekunde kadhaa haya yalinipata…Mama kely hakujua niko ofcn kwake… alikuwa akicheka na kusalimiana na wenzake hukua akiwambia yeye ni Alwatani… hakuna anayeingia mjini asisign kwake… niliumia sana na kutoka na nilikutana naye kwenye korido na hakunisalimia wala hakuonekana kujali. Niliondoka kwa hasira nikiwa nalia sana. Nilijiuliza niende wapi?akili ilinivurugika… Niliumia sana. Kichwa kiliuma na macho kunivimba. Nilianza kuhisi miguu mizito na nilishindwa kuendesha gari. Haraka nilipaki pembeni kwani nilikuwa nikipigiwa honi nyingi na madereva wengine huku wakinitusi wasijue yaliyonisibu.
Mama mmoja alihisi nina tatizo kwani nilisimamisha gari kwa ghafla sana. Nilikuwa nimelegea… alikuja na kugonga kiyoo cha mlangoni kuniambia nifungue lakink sikuwa naweza nililalia staling ya gari. MILANGO ILIKUWA IMEJILOKU.aliiita watu na walipasua kiyoo cha gari na kutoa locku. Silumbuki ilikuwaje ila nilizinduka nikiwa hospital na nilimuona mama yangu mzazi akiniambia mawazo ni ya nini?
88888
Mama alinihoji sana na sikuwa naelewa. Nilianza kurudisha kumbu kumbu pole pole. Na nilianza kukumbuka kila kitu. Niligeukia ukutani na kuanza kulia kwa nini mama kely anitende vile. Mama aliondoka na sasa ni wafanyakazi waliokuwa wanakuja kunisalimia. Wengi walijua ni pressure za mume. Lakini ukweli ya mume hayakuniuma kama ya ck na mama kely. Na kama ingekuwa ni kwa wema kwa nini mama kely asinisalimie na kunipuuza?nililia sana huku hakuna aliyekuwa anaelewa mchezo mzima. Nikiwa nimekaa na Bibi mama tunayefanya naye kazi alinihoji sana na kuniambia ni lazima nitulie la sivyo nitachanganyikiwa kwani nielekeako si kuzuri. Nilitamani kumsimulia issue nzima lakini niliogopa kwani kulikuwa na watu wengine. Mume wangu alikuwa akija kunisalimia na mke wa kaka yake aliongozana naye. Mke wa kaka yake alikuwa akinihudumia kwa kila kitu. Sikumuona mama kely wala biye wala sara. Niliumia sana. Moyo ulijaa chuki na kisasi. Nilikaa hospital siku nne. Kisha niliruhusiwa kutoka na kwenda nyumbani. Nilimuomba bibi mara apatapo nafasi aje kunitembelea. Nyumbani walikuka wamama wenzangu wa kanisani kuniona. Waliomba pamoja na mimi. Walinisomea neno. Na waliondoka. Sikuwa ninabujasiri hata wa kuwatazama. Sikuwapenda sana. Waliondoka na kuniahidi watakuja kumisalimia tena.
88
NIKIWA NIMEPATA NAFUU KABISA NA KUJIONA NAWEZA KUFANYA KILA KITU. NILIMPIGIA BIBI SIMU NA KUMTAKA KUZUNGUMZA NAYE WALAU NIPATE AHUENI. BIBI ALIKUJA NA NILIMUELEZEA MAHUSIANO YANGU NA CK. NA MPAKA TULIPOFIKA. KISHA NIKAMUELEZEA MAHUSIANO YA BITE NA MUME WANGU. NA NILIMUELEZA KWAMBA SARA NDIYE ALIYENIELEZEA YOTE. BIBI ALISIKITIKA SANA NA KUNIAMBIA MWANANGU YOTE HAYA UMEYAPANDA MWENYEWE. NILIKUONYA MWANZO NA NILIKUAMBIA ANAYEPELEKWA NA MAJI HUFA AKICHEKA… SASA NDO WEWE. YOTE HAYA YANAKUPATA UKIWA UNACHEKELEA. UMECHEKELEA MARAFIKI WAPYA… UMECHEKELEA MALI ZA UZINZI NA SASA UNAKUFA NA PRESSURE TUKIKUONA.
ALIENDELEA KUSEMA…
FLora umekuwa mwanamke qa kushangaliwa sasa hivi. Nguo uvaazo ni kituko. Lakini hakuna anayekuambia. Sio kwamba watu wanakuona umependeza wana gamaza la hasha. Wanakuona kama umechamganyikiwa.Flora kwa macho yangu nimekushuhudia ukiwa unabadilisha nguo kwenye gari baada ya wewe kutoka kazini. Na ukavaa nusu uchi. Flora una akili kweli?
Any way nisikugombeze sana maana maji yameshamwagika. Isipokuwa uote yanayotokea sasa hivi hembu yapuuze. Achana na hao marafiki. Rudia tabia yako ya mwanzoni. Hii hali itaisha pole pole. Achana na ck. Achana na mama kely achana ma bite na hata sara achana naye. Fuata maisha yako. Penda kanisa kama zamani. La sivyo utaaibika zaidi. Hio ni negative bado picha. Ila ukichoma negativu hawatapata picha watu. Lakini ukitunza negative picha halisi itajulikana na aibu ya maisha.
BIBI ALIMALIZA KUZUNGUMZZA NA AKANIAMBIA ANAONDOKA. ALIPOONDOKA TU SARA NA BITE NAO WALIINGIA.
888
Nilipowaona nilishindwa kujizuia. Nilianza kuropoka kama sina akili nzuri.
Wanafiki nyie mnanizunguka.. tokeni hapa kwangu malaya ninyi. Wewe bite huna aibu unatoka na mume wangu loo mbona huna haya?Na hata wewe sara mmbea na wewe lenu moja. Na hata mama Kely naye. Malaya nyie. Noliwatukana kwa maneno hayo tu. Sikuwa najua zaidi ya hapo. Waliondoka huku wakiwa wametahayari. Sara alioneka a kiumia na wakati wanaondoka walizozana. Na kila mmoja kuondoka na njia yake. Mama yangu mzazi alikuja kunisalimia na aliniambia mama mkwe wangu kamueleza maneno makali sana juu yangu kuwa na mahusiano na mwanaume.
Mama alianza hivi.
Florah mwanangu mbona unaniacba uchi wangu kila mmoja anione?
Niligutuka kidogo na kisha kung’aka.
Mama nimefanya nini?
Mama aliniambia usinifiche. Tafadhali nieleze ukweli nikusaidie.
Hembu niambie wewe ni wa kuwa na mabwana kweli mwanangu?utumishi wa Mungu umeuacha kwa nini?
Mama alidondosha machozi. Niliogopa kumficha ila kumwambia kweli sikuwa tayari. Alilia sana akinieleza wewe ni wa kwenda kwa waganga?wewe wa kulewa?wewe wa kutoa momba?wewe huyu Flora… ni nini kimekupata mwanangu?mbona umekuwa zaidi ya mmbwa?mbona hali yako imekuwa mbaya kuliko mwanzo?
Mama aliomboleza. Wakati analia mimi ninapata hasira na kuunda agenda mpya akilini juu ya ck na mama kely. Licha ya bite ambaye bado nina hasira naye.
Mama alinisihi nimueleze ukweli ila nilisema amenisingizia. Na mama aliniambia mama mkwe wako kasema kwa namna unavyomuaibisha wala hata hapa hatakuja kabisa.
Niliumia ila nilamwambia mama mbona asiseme mwanae anamuaibisha ili hali anajua tabia zake?
Mama aliniambia huu sjo muda wa kulumbana na kutaka kulipiza kisasi. Ni muda wako wa kujirekebisha. Hembu kumbuka mwanangu Mungu alivyokupigania siku za ujana wako ukamtumainie sasa.
Nilimkatalia mama katu katu kuhusu tuhuma alizonipatia.
Mama aliondoka akiwa hana furaha kabisa.
888888
SIKU ILIYOFUATA NILIENDA KAZINI. BIBI ALINIITA NA KUNIAMBIA KUWA MAKINI SANA. NILITAMANI KUMPIGIA CK SIMU KWANI NILIM MISS. NILIPIGA SIMU YAKE YA OFCN NA KWA BAHATO ALIPOKEA. HAKUONGEA KAMA AWALI. ILA ALIKUWA KAMA ANANIKEJELI. NILIMUULIZA MBONA HUNA RAHA?ALINIELEZA NINI UMENIFANYIA?NILIMUULIZA KWANI NI NINI?
ALINIAMBIA KITU CHA AJABU.
ALINIAMBIA HIVI. KAMA UNAWEZA KUJA HAPA OFCN MARA MOJA NJOO. SIWEZI KUONGEA MA WEWE KWA SIMU. TAFADHALI NJOO MARA MOJA.
HARAKA NILITOKA NA KUWASHA GARI NANKUMFUATA. NILIFIKA NA ALINIKARIBISHA OFCN KWAKE NA KISHA ALINIAMBIA HIVI.
Flora nimekupenda sana. Lakini iweje uniloge?yani unaenda kwa mganga anakupa pete ya kuniloga?na kisha anakuambia ubebe mimba na uue mtoto uli penzi langu kwako lisife. Flora wewe ni wa kunifanyia mimi hivyo?
Nilishangaa sana kajuaje nikajua tu mama kely kamwambia mpaka kajazia.
Aliniambia unabisha?sema ukweli nikusamehe mpenzi wangu. Alinisihi nimwambie ukweli.
888888
NIKIWA NIMEKAA NATAFAKRI NISIJUE NIFANYE NINI,
CK ALINIULIZA UTAKUNYWA NINI MAMII? NILITAFAKARI UZURI WAKE NA UPOLE WAKE, UPENDO WAKE NA SIKU ZOTE ALIVONIHURUMIA,, NILIONA NJIA PEKEE NI KUAMUA KUMUELEZA UKWELI,
NILIMUELEZA NITAKUNYWA JUICE, NA ALINIITISHIA JUICE NA KUNIPATIA. ALIONEKANA MPOLE SANA, NA KISHA ALINIAMBIA NIAMBIE UKWELI FLORA, WANADAMU HUKOSEA, KUTENDA KOSA SIO KOSA BALI KURUDIA KOSA,, NA ALINIONYESHA ZAWADI ZANGU KWENYE DROO YAKE, ALINONYESHA CHENI YA DHAHABU, ALINIONYESHA HERENI NZURI SANA AMBAZO ZILIKUWA KWENYE PARK NZURI SNA NA KUSEMA ALL THESE ARE URS,, NAKUPENDA FLORA, JUST TELL ME THE TRUTH .NIAMBIE HAYA MAMA NIAMBIE,, HAYA MAMII NIAMBIE UKWELI WAKO,, NIAMBIE MPENZI WANGU,, MIMI NA WEWE NI WAPENZI MWAKA SASA UNANIFICHA NINI?
NILIFURAHIA ALIVYONIKUMBATIA, NILIFURAHIA ALIVYONIBEMBELEZA NA AKILI YANGU IKANIAMBIA KWA NINI NIMDANGANYE, BORA NIMWAMBIE UKWELI ANISAMEHE YAISHE TUANZE MAISHA YETU MAPYA.
Flora mimi siamini uchawi na kamwe siwezi kulogeka, yani wala usijali kwani najua uchawi wako haujanidhuru… hivyo usijali kunieleza ukweli mamii.. aliishika shika mikono yangu na kisha akaniambia haya mami niambie.
Noma sana
Hadithi nzuri