Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Mwigulu yuko vizuri sana sema huwa hachelewi kujibu upuuzi wenu na wa viongozi wenu tena kwa fact na ndiyo maana mnamchukia. Kwa Mwigulu Mama Kalamba dume.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Kila sehemu yaonesha mwigulu hawamkubali ajitazame anakosea wapi

Haisaidii kitu,Rais anamkubali na ndiyo maana akampa Wizara nyeti kabisa. Hilo la “hawamkubali” ni kawaida. Hata wewe hapo si wote wanakukubali. Hakuna jipya,chapa kazi Mwigulu
 
Si kwamba namtetea, ila Mwigulu Nchemba anafaa katika wizara hii ya fedha

Tukumbuke alishawahi kuwa katika wizara hii na katika awamu yao hiyo ndio wizara ya fedha ilikuja na mifumo madhubuti ambayo kwa kiasi kikubwa ina control matumizi ya fedha za umma

Kubwa ninalokumbuka na alilofanya vizuri kipindi hicho ni mfumo wa ulipaji mishahara kwa watumishi wa umma "Lawson" (Sina hakika na spelling)

Huu mfumo kwa kiasi kikubwa ndio unaosaidia watumishi kupata mshahara kwa wakati na kwa pamoja kuliko ilivyokuwa zamani

Pia kwa kiasi kikubwa huu mfumo umedhibiti maafisa watumishi kulipa mshahara "account" fake na kwa kiasi kikubwa hakuna namna mtumishi wa umma atakosa mshahara kama yupo kwenye mfumo endapo yupo kazini Kama ilivyokuwa zamani

Pamoja na "ulimbukeni" wake aliouonyesha kipindi cha Magufuri, ila bado ni mtu makini pale anapokuwa na watu sahihi

Binafsi naamini alikuwa hivyo alivyo kwasababu ya kutaka kuendelea kubaki madarakani maana ndio aina ya Boss aliyekuwa nae

Bila kujipendekeza na kujifanya hazimo kulikuwa hamna namna ya kuendelea kula

Tumpe muda tuone Kama "sifa" zitaendelea ndio tumseme

Mtu ambaye naona ni "incompetent" mwanzo mwisho ni Jaffo

Huyu bwana ni Mzee wa makelele sijawahi ona utendaji wake tangu aanze kujulikana. Naamini huyu wanamstili tu lakini hana anachofanya

hivi wewe ungepewa tamisemi ufanye kazi chini ya jpm ungestahimili walau miezi 6?

kufanya kazi na pombe ilikuwa kama kubeba fuko la misumari
 
Bora hata Dr Mkenda au Dr Kimei ana PR nzuri kuliko Mwigulu. Kuna wengi wanafaa nafasi hiyo lakini sio Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa mkorofi, mwenye visasi na mjanja mjanja hivi.
ukimuacha Mwigulu (ambaye umesema humtaki); hao wengine unawajua?
 
Ni wazi Mwendazake hakupendwa kwa sababu ya kumbeba huyu kama hakuna wengine wenye uwezo zaidi.

Anapendwa na Mama Samia Suluhu inatosha. Ja ataendelea kubebwa vizuri sana, wewe usiyempenda huna madhara,huyu ndiyo Waziri wako wa Fedha.
 
Dr Mwigulu Nchemba kati ya Watanzania 10 wanaolitaja jina lake ni wawili au watatu ndiyo wanamwona ni Kiongozi mzuri. Dr. Mwigulu alikuwa mzuri wakati upinzani ulipokuwa imara - yaani Waziri wa Vijembe Vijembe hivi.

Hata nafasi aliyopewa na JPM ndiyo ilikuwa inamfaa. Kwa sasa alipaswa kuwa ile ya Bashungwa sio sijui. Wizara ya Fedha Mwigulu hafai - mnaweza mkawa mnaogopa bure tu.

Bora hata Dr Mkenda au Dr Kimei ana PR nzuri kuliko Mwigulu. Kuna wengi wanafaa nafasi hiyo lakini sio Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa mkorofi, mwenye visasi na mjanja mjanja hivi.

Mwigulu bora hata angepewa nafasi ya Mhagama halafu Mhagama akapewa TAMISEMI na Ummy akapewa Utalii au Kilimo. Kwa Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa haswa ni hakika uchumi utadorora kwa sababu utakuwa wa kisiasa zaidi na hata usitegmee wafanyakazi kupata maslahi mazuri na hata wafanyabiashara itakuwa hovyo hovyo tu.

Kwa kifupi Mwigulu hafai pale - bora abadilishwe haraka.
Acha wivu wa kike
 
Back
Top Bottom