Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Kipindi cha uwaziri wa Mambo ya ndani cha mwigulu.
1.ben Sana name kupoteza
2.lisu KUPIGWA RISASI
3.watu wasiojulikana
4.maiti kuokotwa ndani ya viroba.
5.utekaji. n.k
Kwa haha matukio HAFAI KUWA KIONGOZI.
 
Dr Mwigulu Nchemba kati ya Watanzania 10 wanaolitaja jina lake ni wawili au watatu ndiyo wanamwona ni Kiongozi mzuri. Dr. Mwigulu alikuwa mzuri wakati upinzani ulipokuwa imara - yaani Waziri wa Vijembe Vijembe hivi.

Hata nafasi aliyopewa na JPM ndiyo ilikuwa inamfaa. Kwa sasa alipaswa kuwa ile ya Bashungwa sio sijui. Wizara ya Fedha Mwigulu hafai - mnaweza mkawa mnaogopa bure tu.

Bora hata Dr Mkenda au Dr Kimei ana PR nzuri kuliko Mwigulu. Kuna wengi wanafaa nafasi hiyo lakini sio Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa mkorofi, mwenye visasi na mjanja mjanja hivi.

Mwigulu bora hata angepewa nafasi ya Mhagama halafu Mhagama akapewa TAMISEMI na Ummy akapewa Utalii au Kilimo. Kwa Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa haswa ni hakika uchumi utadorora kwa sababu utakuwa wa kisiasa zaidi na hata usitegmee wafanyakazi kupata maslahi mazuri na hata wafanyabiashara itakuwa hovyo hovyo tu.

Kwa kifupi Mwigulu hafai pale - bora abadilishwe haraka.
Kelele za nini teuni wakwenu anayewafaa kutoka cdm huyo kateuliwa na walio madarakani ambao ni ccm.

Tatizo mnajifurahisha sana je kama mlishasema wote wa ccm hawafai ni yupi atakayewafaa bwana?

Acheni watu wachape kazi na ninyi undeni serikali yenu
 
ni sahihi mkuu lakini tutulie tu mama amesema kwasasa hatoi mtu ila siku zinavyozidi kwenda atafanya mabadiliko makubwa mnoo
 
Nakumbuka alipo pata ajali ya kugonga punda watu walikuwa tayari kumtolea damu punda kuliko huyo cha ajabu alipo pona akamshukur jpm kwa kumjereshea uhai ama kweli ya Kaisar mwachie mwenyewe
 
Labda kwao huko Iramba sijui kiomboi, ila kuja huku Ikungi, manyoni na itigi hawampendi na hata sigida mjini paka kule ilongero hawampendi
Unadhani sisi wa iramba tunamhitaji? Watu wanakenua meno ni mifupa huyo jamaa watu hawampendi hadi kwao, sema akikujua kiukweli Izraili anakuhusu
 
Mimi namkubali Mwigulu hata naamini atakuja kuwa Rais wa hii nchi.
Yaani umeandika sentensi moja hapo umemaliza!
Kijana, Jifunze kujenga hoja ili utushawishi kuwa huyo Mwigulu wako anafaa kuwa rais ajaye.
Weka sababu kwanini anafaa.
 
Unadhani sisi wa iramba tunamhitaji? Watu wanakenua meno ni mifupa huyo jamaa watu hawampendi hadi kwao, sema akikujua kiukweli Izraili anakuhusu
Inasemekana aliiba mnoo kura. Alimwibia kura jiwe hadi zikazidi idadi ya wapiga kura wenyewe! 2025 anang'olewa!
 
Kwa Kimei no,Mchaga hapana.


Asili yake ndiyo hiyo .
Wachaga ni kama wahindi na wasomalia .
Wanajua chaneli za kifedha kote duniani.

Uchumi unahitaji mtu anayejua kucheza na ghiliba za kifedha kote duniani.
Waziri anayeua uchumi kwa lengo la kufilisi watu wa eneo au rangi fulani hatufai kabisa.
 
Waziri Mwigulu ni smart na ni mkali kweli kweli, ndio maana TEAM WORK ni muhimu kuliko TASK FORCE.
 
Back
Top Bottom