Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Ndiyo kateuliwa lakini hapendwi na wengi

Hapendwi na wangapi bana, wapi ulifanya utafiti?.
 
Dr Mwigulu Nchemba kati ya Watanzania 10 wanaolitaja jina lake ni wawili au watatu ndiyo wanamwona ni Kiongozi mzuri. Dr. Mwigulu alikuwa mzuri wakati upinzani ulipokuwa imara - yaani Waziri wa Vijembe Vijembe hivi.

Hata nafasi aliyopewa na JPM ndiyo ilikuwa inamfaa. Kwa sasa alipaswa kuwa ile ya Bashungwa sio sijui. Wizara ya Fedha Mwigulu hafai - mnaweza mkawa mnaogopa bure tu.

Bora hata Dr Mkenda au Dr Kimei ana PR nzuri kuliko Mwigulu. Kuna wengi wanafaa nafasi hiyo lakini sio Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa mkorofi, mwenye visasi na mjanja mjanja hivi.

Mwigulu bora hata angepewa nafasi ya Mhagama halafu Mhagama akapewa TAMISEMI na Ummy akapewa Utalii au Kilimo. Kwa Mwigulu ambaye ni Mwanasiasa haswa ni hakika uchumi utadorora kwa sababu utakuwa wa kisiasa zaidi na hata usitegmee wafanyakazi kupata maslahi mazuri na hata wafanyabiashara itakuwa hovyo hovyo tu.

Kwa kifupi Mwigulu hafai pale - bora abadilishwe haraka.

Unamjua personally.
 
Alikuwa kiongozi mwenye ustadi aliyekuwa tayari kubeba mawe ili kuupinga utawala wa shule sijui hii morali iliishia wapi

Shida yako unataka unavyoona wewe ndo aone yeye. Na Bahati mbaya Ni pale unapojiona wewe sahihi sana.
 
Na ndio amehudumu wizara nyingi nyeti
Hapo Wizara ya Fedha, Mwigulu anaenda kuwa Naibu Waziri. Waziri kamili atakuwa ni Dr Mpango.

Jukumu kubwa ambalo Samia amemkabidhi Dr Mpango ni kusimamia Fedha, Uchumi na mipango. Mwigulu yupo ili tu kukamilisha taratibu.
 
Mie nimefurahi rais hajasikiliza manenobya mitandaoni na wapinzani kumpangia watu...kawapiga low blow moja matata...
Hivi kuna aliyekuwa Waziri, ameachwa kuwa Waziri? Subiri kwanza, kadiri siku ziendavyo ndiyo utafahamu nani kateuliwa kuwa Waziri, na nani aliqchwa alimradi siku zipite, kuzuia taharuki.
 
Kumbuka huyu sio kilaza Mnyika wala kilaza Mbowe. Ame elimika vizuri sana, na ni mmoja ya watanzania waliofauli vizuri. Inawezekana nazungumza na mwana JF ambaye hajui nini maana ya kupata First Class katika ngazi ya Degree.

Alifanya vizuri kwa nafasi ya Ukkurugenzi, Benki Kuu na Naibu Waziri wa Fedha, hayo ya kumkomesha Rwakatare kama Mbunge wa Bukoba kupitia Chadema haiuondoi usomi wake, weredi wake haitufanyi Watanzania wote tusahau uwezo wake.

Hatushangai tunafahamu kuna watanzania wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii na hawana jema. Ukimtukana baba yako wana kusifia, ukimfanyia mazuri mzazi wako wanakuzomea.

Jamii gani hii ya Jamhuri ya JF. Ukiwa Mchaga utasakamwa Ukiwa Msukuma hafai, ukiwa kiliza uko Chadema wewe Msomi, ukiwa na akili puvu ukiwa CCM wewe mjinga. Taabu tupu.
Mwigulunakili anayo, anachokikosa ni hekima na utu.
 
Mwigulu kapewa kama screen, remote ni Dr Mpango.
Wewe ni miongoni mwa wachache walioelewa.

Dr. Mpango ndiye atakuwa Waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango lakini mwenye hadhi ya juu kuliko Mawaziri wote.

Dr Mpqngo ndiye atakuwa Archtect wa kila kitu kwenye Fedha, Uchumi na Mipango. Mwigulu atakuwa Fundi mchundo.
 
Mtu wa hovyo hovyo asiye na faida anayeponea mbeleko za wakubwa tu! Qualification zake za makratasi ni tofauti na matendo yake!
 
Back
Top Bottom