Ndio kwanza nina miaka miwili, bado miaka yangu mitatu

Ndio kwanza nina miaka miwili, bado miaka yangu mitatu

scolastika

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2019
Posts
3,863
Reaction score
5,736
Ndio kwanza kumekucha kwenye miaka mitano ya kikatiba bado nina miaka yangu mitatu kamili.
Mlilia nchi imefungwa mtangulizi wangu ameua utalii, mazao hayatoki ndani bei inawaumiza wakulima, sasa nimefungua kaeni kwa kutulia.

Mkadai mtangulizi wangu hapendi kusafiri kwa sababu hajui kingereza, na hatafuti uhusiano na nchi zengine, mwenzenu kingereza najua, Vasco dagama nimekuja ngoja nisafiri nitafute ugali wanangu, kaeni kwa kutulia
Alijiita mzalendo mkadai ni fisadi mimi mzalendo wa kweli nimekuja, kaeni kwa kutulia.

Aliwatumbua ambao hawakutosha kwenye nafasi zao mkasema ni kichaa, aliwahi kulazwa milembe, mwenye akili zangu nipo nimewarudisha mzigoni, kaeni kwa kutulia.

Alipokuwa akisisimama njiani kusikiliza shida za watu mkasema anatafuta popularity, mwenzenu sitafuti popularity shida zote malizeni huko.

Et mnalia maji sijui Umeme, hapo bado mpaka myaite maji mmaa

Ndo kwanza miaka miwili tu, bado niponipo kwanza.

Na kwa vile nimefanya yale mlikuwa mkiyataka nina imani mtaniongezea mingine ili itimie kumi niwafungulie nchi.
 
Baki miaka 100 mama SA100. Mpaka vitukuu vyangu vikukute madarakani kama queen Elizabeth mama.
 
Kila mtu ana fuvu lake hiyo sio guarantee kwamba linatumika ipasavyo.
 
Mama Samia Awe Queen Wetu tuwe tunachagua wabunge na Waziri Mkuu Tuu
 
Huyu Mama mbona amefanana kila kitu na Jiwe, lijiwe nalo livyookota CCM pale mitaa ya Lumumba, akaanza mbwembwe za huyu bibi kinaje kinanguruma,akafika mahali akaanza kukorokochoa roho za watu kama kina Lissu , akajiona mungu, mwisho wake mliona Jiwe kuugua tu na kundei pale muhimbili alikataa kwenda mochwati akaemda mzena akidhani kama wanachomoaga roho za wabishi watakuwa na roho za akiba
 
Huyu Mama mbona amefanana kila kitu na Jiwe, lijiwe nalo livyookota CCM pale mitaa ya Lumumba, akaanza mbwembwe za huyu bibi kinaje kinanguruma,akafika mahali akaanza kukorokochoa roho za watu kama kina Lissu , akajiona mungu, mwisho wake mliona Jiwe kuugua tu na kundei pale muhimbili alikataa kwenda mochwati akaemda mzena akidhani kama wanachomoaga roho za wabishi watakuwa na roho za akiba
Alishakufa mwaka na miezi zaidi ya 7, mbona bado una hasira namna hii?
 
Back
Top Bottom