Ndesamburo na tamaa ya Madaraka....

Ndesamburo na tamaa ya Madaraka....

Mangi Mkubwa

Senior Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
107
Reaction score
29
Habari za Mchana wana Jf.

Taarifa za ndani zilizonifikia ni kwamba Mbunge wa Jimbo la Moshi Philemoni Ndesamburo (Chadema )ambaye amekuwa Mbunge kwa zaidi ya vipindi vitatu,kwa sasa anamchakato wa kurudi tena kwenye Jimbo hilo katika uchaguzI mkuu ujao.

Ndesamburo ambaye amekuwa akitumia muda mwingi kwa ajili ya kutibu afya yake nje ya nchi na kushindwa kuwatumikia wananchi na hata kuhudhuria vikao muhimu vya Bunge leo inasikitisha kuwa bado mzee huyo anataka kufia kwenye ubunge.

Ndesamburo anamiaka zaidi ya 80 kwa sasa na awali katika uchaguzi ulioisha mwaka 2010 alifanya kampeni zake kwa shida kutokana na afya yake,lakini alifanikiwa kupata viti vingi vya udiwani kwenye kata za manispaa ya moshi zaidi ya 17.

Tangu alivyoshinda uchaguzi mwaka 2010 alikuwa hajawahi kuonekana wala kufanya mikutano ya kisiasa,hadi mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwaka huu ambapo ameanza kutembelea kata zote kwa ajili ya kujiimarisha ili agombania tena jimbo hilo,ambapo hata kwenye mikutano amekuwa ak,ihutubia kwa shida,huku wakati mwingine akitaka kuanguka.

Hatua hiyo ya Ndesamburo kutaka kugombe imekuja baada ya mpango wa kutaka kumuweka mwanae Lucy Owenye kugombea Jimbo la Moshi kuona hatauzika na kumchafua kisiasa hivyo kuamua kugombea kwenye nafasi hiyo.
Kwa sasa kuna wanahabari ambao anawatumia kwa ajili ya kupita kwenye Kata ili kumfanyia utafiti kujua kama anakubalika kiasi gani ili aweze kugombea,na kuwapa kiasi kikubwa cha fedha.

Hali hiyo imefanya Chadema Mkoa na Manispaa ya Moshi kuendelea kukosa nguvu ya umoja,licha ya madiwani wengi kulazimika kukaa kimya kwa kuwa wanamtegemea mzee ndesamburo kama mfadhili wao mkubwa.

Tangu achaguliwe mzee ndesamburo amekwishahudhuria kikao kimoja tu cha baraza la madiwani ambacho amehudhuria januari mwaka huu huku vikao vingine muhimu ikiwemo ya bajeti akishindwa kuhudhuria kwa kuwa alikua Uingereza zaidi ya Mwaka kutibu maradhi yanayomsumbua.

Siandiki waraka huu kwa chuki ila nahitaji kujadili kwa hoja,sina chuki na Mzee ndesamburo,ila na ni rafiki yangu,muda wake wa kupumzika umefika awaachie vijana,kwani Meya wa Manispaa ya Moshi japhary Michael amekuwa kama ndio Mbunge wa Moshi kwa kulazimika kuchukua majukumu yake na maswali yanayotoka kwa wananchi kwani Ndesamburo amekuwa hatambua tena nafasi yake na kugeuka kama mfadhili.
Meya wa Moshi Japhary Naye alikuwa ameshatangaza kugombea nafasi hiyo ya Ubonge wa Moshi lakini kutokana na Mzee Ndesamburo bado anatamaa ya kubaki madarakani imebidi atangaze rasmi kujiondoa kwenye siasa ifikapo mwaka 2015.
Sipo upande wa Meya,kwa atakayesoma hapa ila nazungumzia uhalisia uliopo kwa Jimbo la Moshi ambapo kwa sasa Waandishi hao ndio wanamdanganya mzee ndesa kuwa utafiti waliofanya unaonesha kuwa unakubalika hivyo arudi kugombea.
Moshi ingekuwa na Mbunge ambaye ni mfuatiliaji ambaye angeweza kushirikiana na Meya wa Chadema,moshi ingekuwa na maendeleo makubwa tofauti na ilivyo sasa.

Katika kikao cha bajeti kila Mbunge alisimama na kuzungumza changamoto zilizopo kwenye Jimbo lao lakini kwa kudhihirisha kweli moshi haina Mbunge,sikuona hoja ya Mbunge wetu kuzungumzia hospitali ya Mkoa ya Mawenzi ambapo ni zaidi ya miaka mitatu kwa sasa haina chumba cha upasuaji na ipo JImbo la Moshi.

Kiukweli siyo kwamba wazee hawawezi ila inapofika wakati embu tuwapishe vijana wafanye kazi kwa kuwa muda ambao ndesa anatumia kwa ajili ya matibabu na kucheki afya nje ya nchi unazidi hata ule ambao angetakiwa kuwatumia wana wa Moshi,je ni vema tukaendelea na Mbunge wa namna hiyo kwa kuwa anafedha au akawepo kiongozi mchapakazi na mwenye uwezo wa kuwajibika kwa wananchi?
 
Mwenyekiti ndiyo kawafundisha mnategemea nini kwa wadogo.
 
Mkuu hapa nipingane nawe,

Kugombea sio tamaa ya madaraka bali kung'ang'ania madaraka ndio tamaa.

Ndesamburo ni tofauti sana na viongozi wengine wa Chadema na kwa kifupi wananchi wanamuhitaji yeye kuliko hata yeye anavyohitaji huo ubunge.

Katika viongozi wote wa upinzani, huyu kwangu ni role model and it is my wish to be like him.
 
Mi naona kama ni tamaa ya madaraka kwani hata Nyerere alipoacha kugombea uongozi bado wananchi wanamuhitaji na alikuwa na uwezo wa kuwatumikia wananchi tofauti na Ndesamburo ambaye anataka afie kwenye Ubunge.
 
Kwa nini tusilaumu sheria ya nchi ambayo haijatoa ukomo wa umri au vipindi vya kuwa mbunge? Kama sheria ya nchi iko wazi kwa nini vyama vimzuie mtu anaeweza kuwapa ushindi? Tumesahau ya akina Mzee Kingunge kuwa waziri mpaka umri wa aibu.
 
Mkuu hapa nipingane nawe,

Kugombea sio tamaa ya madaraka bali kung'ang'ania madaraka ndio tamaa.

Ndesamburo ni tofauti sana na viongozi wengine wa Chadema na kwa kifupi wananchi wanamuhitaji yeye kuliko hata yeye anavyohitaji huo ubunge.

Katika viongozi wote wa upinzani, huyu kwangu ni role model and it is my wish to be like him.

Hata mimi namkubali sana Ndesamburo ila nakubali kutokubaliana naye kwenye maamuzi yake anayotaka kuchukua ya kugombea ubunge Moshi Mjini kwa kwel anahitaji kupumzika na hilo awali alikuwa ameshiliona ila cjajua nini kimempata.
 
Kwa nini tusilaumu sheria ya nchi ambayo haijatoa ukomo wa umri au vipindi vya kuwa mbunge? Kama sheria ya nchi iko wazi kwa nini vyama vimzuie mtu anaeweza kuwapa ushindi? Tumesahau ya akina Mzee Kingunge kuwa waziri mpaka umri wa aibu.
Nyani huwa haoni kundule...!
 
Sasa kama ni rafiki yako kwanini usingemshauri privately.?

As long as moshi imepaa sana kimaendleo sidhani kama Kuna haja ya yeye kumpumzika..
 
Habari za Mchana wana Jf.

Taarifa za ndani zilizonifikia ni kwamba Mbunge wa Jimbo la Moshi Philemoni Ndesamburo (Chadema )ambaye amekuwa Mbunge kwa zaidi ya vipindi vitatu,kwa sasa anamchakato wa kurudi tena kwenye Jimbo hilo katika uchaguzI mkuu ujao.

Ndesamburo ambaye amekuwa akitumia muda mwingi kwa ajili ya kutibu afya yake nje ya nchi na kushindwa kuwatumikia wananchi na hata kuhudhuria vikao muhimu vya Bunge leo inasikitisha kuwa bado mzee huyo anataka kufia kwenye ubunge.

Ndesamburo anamiaka zaidi ya 80 kwa sasa na awali katika uchaguzi ulioisha mwaka 2010 alifanya kampeni zake kwa shida kutokana na afya yake,lakini alifanikiwa kupata viti vingi vya udiwani kwenye kata za manispaa ya moshi zaidi ya 17.

Tangu alivyoshinda uchaguzi mwaka 2010 alikuwa hajawahi kuonekana wala kufanya mikutano ya kisiasa,hadi mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwaka huu ambapo ameanza kutembelea kata zote kwa ajili ya kujiimarisha ili agombania tena jimbo hilo,ambapo hata kwenye mikutano amekuwa ak,ihutubia kwa shida,huku wakati mwingine akitaka kuanguka.

Hatua hiyo ya Ndesamburo kutaka kugombe imekuja baada ya mpango wa kutaka kumuweka mwanae Lucy Owenye kugombea Jimbo la Moshi kuona hatauzika na kumchafua kisiasa hivyo kuamua kugombea kwenye nafasi hiyo.
Kwa sasa kuna wanahabari ambao anawatumia kwa ajili ya kupita kwenye Kata ili kumfanyia utafiti kujua kama anakubalika kiasi gani ili aweze kugombea,na kuwapa kiasi kikubwa cha fedha.

Hali hiyo imefanya Chadema Mkoa na Manispaa ya Moshi kuendelea kukosa nguvu ya umoja,licha ya madiwani wengi kulazimika kukaa kimya kwa kuwa wanamtegemea mzee ndesamburo kama mfadhili wao mkubwa.

Tangu achaguliwe mzee ndesamburo amekwishahudhuria kikao kimoja tu cha baraza la madiwani ambacho amehudhuria januari mwaka huu huku vikao vingine muhimu ikiwemo ya bajeti akishindwa kuhudhuria kwa kuwa alikua Uingereza zaidi ya Mwaka kutibu maradhi yanayomsumbua.

Siandiki waraka huu kwa chuki ila nahitaji kujadili kwa hoja,sina chuki na Mzee ndesamburo,ila na ni rafiki yangu,muda wake wa kupumzika umefika awaachie vijana,kwani Meya wa Manispaa ya Moshi japhary Michael amekuwa kama ndio Mbunge wa Moshi kwa kulazimika kuchukua majukumu yake na maswali yanayotoka kwa wananchi kwani Ndesamburo amekuwa hatambua tena nafasi yake na kugeuka kama mfadhili.
Meya wa Moshi Japhary Naye alikuwa ameshatangaza kugombea nafasi hiyo ya Ubonge wa Moshi lakini kutokana na Mzee Ndesamburo bado anatamaa ya kubaki madarakani imebidi atangaze rasmi kujiondoa kwenye siasa ifikapo mwaka 2015.
Sipo upande wa Meya,kwa atakayesoma hapa ila nazungumzia uhalisia uliopo kwa Jimbo la Moshi ambapo kwa sasa Waandishi hao ndio wanamdanganya mzee ndesa kuwa utafiti waliofanya unaonesha kuwa unakubalika hivyo arudi kugombea.
Moshi ingekuwa na Mbunge ambaye ni mfuatiliaji ambaye angeweza kushirikiana na Meya wa Chadema,moshi ingekuwa na maendeleo makubwa tofauti na ilivyo sasa.

Katika kikao cha bajeti kila Mbunge alisimama na kuzungumza changamoto zilizopo kwenye Jimbo lao lakini kwa kudhihirisha kweli moshi haina Mbunge,sikuona hoja ya Mbunge wetu kuzungumzia hospitali ya Mkoa ya Mawenzi ambapo ni zaidi ya miaka mitatu kwa sasa haina chumba cha upasuaji na ipo JImbo la Moshi.

Kiukweli siyo kwamba wazee hawawezi ila inapofika wakati embu tuwapishe vijana wafanye kazi kwa kuwa muda ambao ndesa anatumia kwa ajili ya matibabu na kucheki afya nje ya nchi unazidi hata ule ambao angetakiwa kuwatumia wana wa Moshi,je ni vema tukaendelea na Mbunge wa namna hiyo kwa kuwa anafedha au akawepo kiongozi mchapakazi na mwenye uwezo wa kuwajibika kwa wananchi?

Hizi ni siasa chafu na hila. Inaonekana ID hii imefunguliwa kwa lengo hili

Wananchi wa Moshi ndio wenye ridhaa ya kuamua ni nani awe mbunge wao na sio vinginevyo

Ndesamburo Kufanya siasa na kupita kila kata ni kazi yake kama Mbunge.Sijui kwanini ulalamike sasa hivi kwa mbunge kutekeleza wajibu wake

Kama alikua anaumwa kuna makosa gani akipita kwenye kata kusimamia wapiga kura wake?
 
Back
Top Bottom