Mkuu hii haijakaa vizuri.Watu wamepoteza maisha we unaleta utani
Moderators mbona mnabadilisha heading ya habari yangu baanaaa....
Je hamjasoma tamathali za semi za lugha ya Kiswahili?
Kwa nini hamjanitumia PM kuniambia mnataka kubadili heading?
Ona sasa mnapotosha dhana nzima ya nilichotaka kukiwakilisha...
Please Invisible au Moderator futa tu hii thread maana haina mantiki tena kwa mlichokifanya....
Watu wamepoteza maisha!kwahiyo ndege imepatikana!
Ayayaya!!!, mkuu ulikuwa umeharibu."Ndege Iliyopotea Yapatikana"
Ahhaahahahahha nimecheka hadi nahisi kuumwa tumbo lol.....
Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
mkuu ndio hii ndo ndege iliyopotea, mara ya mwisho ilikuwa inachezewa milembe dodoma ila kuna kichaa mstaafu aliondoka nayo...ukiishusha uipeleke kule milembe dodoma maana inatafutwa!
Ayayaya!!!, mkuu ulikuwa umeharibu.
Hiyo heading ingeweza kusababisha "maafa".
Hii inayouliza tu imezua mshtuko sembuse hiyo, kwa hiyo mods wamefanya vizuri ili kulinda hadhi ya forum, hata kama ni jukwaa la jokes ulitumia lugha kali, ila hata hivyo kama ulivyosema walitakiwa kukuarifu kama utaridhia kubadilisha heading, otherwise wangeiondoa kama waliona imeenda kinyume na rules.
Mkuu nimetumia uandishi unaohitaji fikra ya kina...ndio maana sijataja jina la shirika la ndege hivyo bado sio uzushi
Watu8 hata kama hujataja jina la shirika la ndege,lakini kumbuka pia kuwa issue ya ile ndege kupotea iko hot.Ukweli hata mie nimefungua haraka haraka kutaka kuona.
Anyway,nashukuru kwa kuturusha roho,lakini kumbuka leo siyo tarehe 01/04