Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 576
Wewe unategemea ngumi ya moto inaanikwaga kihivyo. Waambie wamalawi wako wafanye kweli halafu wasikilize muziki wa Bongo ulivyo mtamu. Kama unadhani nabisha nenda kamuulize Ndili Idd Amin Dadaa. Alikuwa na vifaa vya kisasa sana lakini hakujua namna ya kuvitumia, akaviacha Kagera na wabongo walipovicgukuwa wakavitumia hivyo hivyo kumrudi mpaka akasahau kuitikia kibwagizo. Mtu yeyote mwenye hekima haaniki silaha yake kila adui aione. Ukitaka kujua kwamba adui yako hajambo nenda kamchokoze nyumbani kwake kamgambile stupid infront of my wife wake na watoto wake. Hapo sasa. Kuna nyoka fulani kule kwetu ukienda kutafuta kuni anakaa kwenye matawi na rangi yake inafanana na tawi alilolalia. Unitaka kuuvunja ukuni huo unashangaa ni laini, yeye anakuangalia tu anakusamehe akijua ni bahati mbaya. Lakini akiona unamaanisha kwa makusudi, silaha yake ni mate kama kamasi hivi, akikurushia unaanza palepale kuumuka kama andazi lenye hamira. Usicheze na askari wa Bongo bana. Mdharau mwiba huchomeka.