Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,042
- 33,527
Kwa ufuatiliaji wangu niliofanya kwenye mambo mbali mbali, nimegundua kwamba CHADEMA imekuwa ikilaumiwa mara nyingi kwamba haitimizi wajibu wake hadi mambo yanaharibika. Kwamfano;
Wakati wa Bunge la katiba CHADEMA iliongoza vyama vingine kutoka kwenye vikao vilivyokuwa vinaendelea vya Bunge la Katiba kupinga jinsi Bunge hilo lilivyokuwa linaendeshwa.
Na mchakato wa kupata Katiba mpya ukaishia hapo. Lakini wabunge waliobakia walikuwa wengi na walipitisha Katiba Pendekezwa. Kwa nini mchakato wa kupiga kura ya maoni ili kuipitisha hiyo Katiba ulifutiliwa mbali?
Huo ni mfano mmoja tu, lakini ukiangalia hata ile marufuku ya kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ililengwa CHADEMA. Hoja iliyotolewa wakati ule na hata sasa ni kwamba mikutano hiyo inazuia watu wasifanye kazi.
Nchi hii inaongozwa na CCM, ni kwa nini basi kila lawama ya kukwama kwa mambo wanatupiwa CHADEMA? Au CCM wanaona wanaostahili kuongoza nchi yetu ni CHADEMA?
Wakati wa Bunge la katiba CHADEMA iliongoza vyama vingine kutoka kwenye vikao vilivyokuwa vinaendelea vya Bunge la Katiba kupinga jinsi Bunge hilo lilivyokuwa linaendeshwa.
Na mchakato wa kupata Katiba mpya ukaishia hapo. Lakini wabunge waliobakia walikuwa wengi na walipitisha Katiba Pendekezwa. Kwa nini mchakato wa kupiga kura ya maoni ili kuipitisha hiyo Katiba ulifutiliwa mbali?
Huo ni mfano mmoja tu, lakini ukiangalia hata ile marufuku ya kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ililengwa CHADEMA. Hoja iliyotolewa wakati ule na hata sasa ni kwamba mikutano hiyo inazuia watu wasifanye kazi.
Nchi hii inaongozwa na CCM, ni kwa nini basi kila lawama ya kukwama kwa mambo wanatupiwa CHADEMA? Au CCM wanaona wanaostahili kuongoza nchi yetu ni CHADEMA?