Nchi hii inapoteza uelekeo, wasomi mko wapi?

wasomi ni nyoka wenyemakengeza!! wala msitumie muda sana kuwaongelea hao!!! wasaliti na wezi wa mali ya umma..ukombozi huletwa na maskini na wala sio pett tycoon..
 
watanzania tukomae kuna mambo mengine sio lazima uende shuleni inahitaji akili yako zaidi na tujitahidi kufanya ufafiti ktk mazingira ambayo yanatuzunguka tutagundua mambo mengi sana ambayo wasomi hawayajui kwasababu sisi ndio tunaangaika na kuwasomesha halafu baadae tunakuja kuonekana hatuna akili
 
tanzania haitakuwa na wasomi mpaka kizazi cha ccm kife kuanzia mwaka uliozaliwa upinzani 1992 kurudi nyuma.
 
Hili taifa halitakombolewa na wasomi bali walalahoi, wasomi wamejiingiza kwenye siasa muda wote wanatumiwa tu
 
Kawaulizie vyuoni uko utapata jibu sahihi wasomi wetu wako wapi, na wewe mwenyewe vipi, siyo miongoni mwao?
 
Mabadiliko Mengi Duniani Yanaletwa Na Nguvu Ya Umma

Wanaharakati Lakini Mabadiliko Matakatifu Bila Rabsha Yanaletwa Na Wasomi Hivi Kwanini Hawa Wa Kwetu Wamepooza Hivi?
Hivi Nini Kimempata Shivji Hata Kubadili Msimamo Wa Kutetea Taifa Wanafunzi Wa Vyuo Vikuu Wakiandamana Ni Kwaajili Ya Mikopo Hawajawahi Kutoka Kutetea Taifa
Fedha Yetu Imekufa,wabunge Wanatumia Kodi Zetu Kujadili Bajeti Hewa. Hivi Nani Wakuwatetea Hawa Wananchi Wa Tandahimba Na Namtumbo Wasomi Wetu Semeni Serikali Hii IMECHOKAA
Tulia wewe nyumbu ukamuliwe
 
Wasomi uchwara .

Unakuta anajiita msomi alafu eti anatoa maoni kuwa Magufuli hatakiwi kuwa rais ,anatakiwa awe chini ya MTU.

Yani MTU mwadilifu awe chini ya fisadi??

Wasomi Wenye mawazo haya ndio Wenye vyeti feki
 
Wasomi uchwara .

Unakuta anajiita msomi alafu eti anatoa maoni kuwa Magufuli hatakiwi kuwa rais ,anatakiwa awe chini ya MTU.

Yani MTU mwadilifu awe chini ya fisadi??

Wasomi Wenye mawazo haya ndio Wenye vyeti feki

Wewe ni km vile vikagosi vya kwenye tv ....kima wewe
 
Wewe ni km vile vikagosi vya kwenye tv ....kima wewe
Natambua nyumbu wengi mna vyeti feki, mtanyooka awamu hii.

Fukuza wote kwenye ofisi zetu muende kuzungusha mikono na kudeki barabara ili mafisadi wapite.
 
Hii inaweza kuwa miongoni mwa mada nzuri sana kuletwa hapa jukwaani, wiki hii. Kwa kweli ukitafakari kwa makini unaweza kubaini kuwa migogoro na matatizo mengi yanayoikabili nchi yetu yanasababishwa na wasomi. Magufuli juzi amesema wazee ndio wameifikisha hapa nchi hii, lakini bila shaka wazee hao aliowalenga sio wale mbumbumbu, ni wazee wasomi. Yeye JPM anaona suluhisho linaweza kuwa vijana, na anasema ndio maana katika awamu yake ameamua awape nafasi vijana wasomi.

Nina wasiwasi na mtazamo wa JPM. Leo ukifanya utafiti kidogo tu katika vyuo vikuu vyetu unaweza kubaini jambo moja kubwa-vijana wanaharibiwa akili wakiwa bado wakiwa vyuoni, na wanapotoka huko hawana tena mawazo na mitazamo ya kizalendo, bali wanakuwa wabinafsi wanaojiangalia wao wenyewe. Hali hii ni matokeo ya vijana hao kuingizwa katika mifumo ya 'kihalifu' ya kutumikia vyama vya kisiasa badala ya kutumikia nchi.

Wapo vijana wazuri tu, wanatoka vijijini wakiwa na uchungu wa kubadilisha jamii zao pindi wakimaliza masomo yao, lakini wanapofika vyuoni wanakutana na hadaa; wanaanza kushawishiwa kujiunga na makundi ya siasa za kihalifu kwa ahadi ya pesa na ajira nzuri baada ya masomo. Nani asiyefahamu tatizo la ajira hapa nchini? Mifumo yenyewe ya maisha vyuoni inawafanya washawishike kwa urahisi na kubadilisha ndoto zao. Wakati awali walikuwa wakiitazama jamii yao, ghafla wanaanza kujitazama wao wenyewe!

Tatizo ni kubwa sana, mfumo wa elimu yetu nao unatufanya tusiwe rahisi kukwepa mbinu za uhalifu unaofanywa kupitia siasa za vyama. Hivi unaweza kuzungumziaje pale kijana msomi aliyehitimu chuo kikuu anapokuja hapa JF, kwa mfano, kutetea ufisadi wa Lugumi vs polisi au ufisadi mwingine katika taifa, kwa sababu tu yeye yuko katika foleni ya kusubiri ahadi ya ajira? Tunaona hapa jinsi vijana wasomi wanavyojitoa akili kutetea hata mambo ya kijinga yanayofanywa na vyama wanavyovishabikia!

Leo mijadala mingi, rasmi na isiyo rasmi, imepoteza sura ya uzalendo na badala yake inabeba sura ya vyama. Tuliona kwenye Bunge la Katiba jinsi wasomi wa kiwango cha madaktari walivyokuwa wajitoa akili wakawa wanajadili mambo kwa maslahi yao binafsi badala ya maslahi ya taifa. Baada ya Bunge hilo inafahamika nini kilitokea kwa wasomi waliokuwa wanatetea upuuzi!

Ni vigumu kujinasua katika hali hiii. Na ugumu unazidi kuongezeka unapoona hata viongozi wa dini wanaingizwa katika mifumo ya "kihalifu" ya kisiasa. Kinachobakia ni kuwa na nchi ya unafiki, unafiki, unafiki kila mahali...
 
siion dhana halic ya msom nchin, weng wamekua wachua tumbo, walafi, wevi, mafisad, wapotoshaji na wahujumu uchumi. baadh ya wasom ndo wameshirkiana na watawala ku2fikisha hapa tulipo. cpend hata kuwackia utackia phd holder, nna masters ya uchum, mara nna degre 3 without any reflection in the society. asilimia kubwa ya watz ndo kabsa ha2elew n bora liende 2 2nasafar ndefu sana kufikia fikra huru zisofungwa fungwa na chama, din, kabila, ukanda na rangi. naamin n zaid ya miaka 100 mbele uko
 
Back
Top Bottom