NCCR Yahimiza Ushirikiano wa Vyama vya Upinzani Katika Uchaguzi

Fredrick Sanga

JF-Expert Member
Jan 27, 2011
3,153
697
Mwandishi wetu, Babati (Tanzania Daima)

CHAMA cha NCCR-Mageuzi, kimekishauri Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuhakikisha kinaweka umoja na vyama vingine ili kujiimarisha katika uchaguzi mkuu ujao hatua itakayofanikisha kuibuka na ushindi katika ngazi ya urais.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Bermi, Kata ya Dareda, Wilaya ya Babati Vijijini, mkoani Manyara, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Danda Juju, suala la vyama vya upinzani kuungana halikwepeki kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kina mtandao mkubwa.
“CHADEMA kwa sasa wanajiona wako juu ya vyama vingine vya siasa, wao wanajiona ndiyo wapinzani wa kweli kuliko wengine wote japokuwa hilo siyo sahihi hata kama kitaungwa mkono na Watanzania wote, alisema na kuongeza kuwa …kitendo cha kutoshirikiana na vyama vingine vya upinzani ili kuishinda CCM kitawagharimu kwa sababu hawawezi kushinda urais wakiwa wao peke yao,” alisema.
Alisema kuwa kabla ya CHADEMA kuwa maarufu, kilianza NCCR-Mageuzi na kwamba kila Mtanzania alijua jinsi chama hicho kilivyotikisa wakiwa na uongozi wa Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema.
Alisema kuwa hata hivyo umaarufu wa NCCR uliporomoka, na ikaja zamu ya Chama cha Wananchi (CUF) ambacho nacho kwa sasa kimepoteza umaarufu na sasa ni zamu ya CHADEMA ambao wanatikisa katika upinzani


My take: Ni wazo makini sana, kwani adui namba moja ni mmoja. Lakini viwe vyama vya upinzani vya ukweli, sio mamluki.
 
Kwanza mbatia ajiuzulu ukamanda alopewa na adui yetu ndo tumfikirie maungano..NCCR mke mdogo wa gamba.
 
Nadhani sababu NCCR wapo katika ndoa isiyo rasmi na CCM ingekuwa ni busara kuishauri CCM kwani ndiyo wanaofanana kiitikadi na kisera pia.

Hawana jipya kabiiiiiiiiiiiiiisa.
 
Juju atuambie ni chama gani hasa cha Upinzani? Hao maswahiba wa Status quo watarefusha tu harakati zetu

Ni jambo zuri kwa upinzani kuungana lakini ni lazima kuwe na kuaminiana na sio political opportunism

Mbona NCCR Mageuzi tayari wako kwenye Muungano na CCM?

Ofcourse,CHADEMA kina historia ya kupigia chapuo muungano.Mwaka 1995 tuliungana na NCCR-Mageuzi na mwaka 2000 na CUF.
 
Juju atuambie ni chama gani hasa cha Upinzani? Hao maswahiba wa Status quo watarefusha tu harakati zetu

Ni jambo zuri kwa upinzani kuungana lakini ni lazima kuwe na kuaminiana na sio political opportunism
 
Hili ni wazo zuri sana.lakini ni vyama vip vya upinzani tunazungumzia? CUF tayari wapo ktk muungano na ccm,Nccr mguu mmoja ndani mmoja nje (Mbatia& JK) TLP ndo usiseme! Sasa CDM waungane na vyama gani? Ushauri wangu kwa vyama vyote vya upinzani; viitishe mkutano wa vyama vyote kujadili hatma ya taifa letu bila kujali itikadi zao: cuf ijiondoe ktk muungano na ccm huko zanzibar.Mrema,Cheyo na mbatia waweke misimamo yao wazi.Ikiwezekana vyama vingine vivunjwe vibakie 4 kutoka ishirini na ngapi sijui nimesahau.Kama kweli vyama vya upinzani vinataka kuwakomboa watz,waweke makubaliano ya maandishi 2015,mgombea urais bara awe mmoja toka chama kimoja wapo,na znz awe mwingine toka chama kimojawapo,wengine waliobakia wapambane kwenye majimbo ili waingie bungeni.Wakifanikiwa kufanya hivyo CCM 2015 ITAKUA HISTORIA HAPA TZ.
 
Juju atuambie ni chama gani hasa cha Upinzani? Hao maswahiba wa Status quo watarefusha tu harakati zetu

Ni jambo zuri kwa upinzani kuungana lakini ni lazima kuwe na kuaminiana na sio political opportunism

Mbona NCCR Mageuzi tayari wako kwenye Muungano na CCM?

Ofcourse,CHADEMA kina historia ya kupigia chapuo muungano.Mwaka 1995 tuliungana na NCCR-Mageuzi na mwaka 2000 na CUF.
Ipo kazi, maana kuna viongozi wanapoke ruswa ya vyeo (Muafaka). JF kuneni vichwa hapa.
 
Vita vya vyama vya upinzani Tanzania ndio mtaji wa CCM.
 
Mwandishi wetu, Babati (Tanzania Daima)

My take: Ni wazo makini sana, kwani adui namba moja ni mmoja. Lakini viwe vyama vya upinzani vya ukweli, sio mamluki.

Hapo kwenye red, ndo panapovivua NCCR, CUF na TLP vyeo vya kushirikiana na sisi, coz wao CCM sio adui yako, ni mshikaji wao, kwetu sisi hawa ni friendly enemies mpaka watapoacha unafiki
 
Siungi mkono hoja kwa asilimia mia moja.

Wazo la kutaka kuviunganisha vyama vya upinzani ni wazo rasmi la CCM.

Kuunganisha vyama vya upinzani Tanzania ni kutaka kuua upinzani.
Kwa mfano mwaka 2010 vyama Saba vya upinzani viliungana na kumsimamisha Ammy Dovutwa kuwa mgombea urais, nini kilitokea?
Siku tano kabla ya uchaguzi alitangaza kujitoa na kuwashawishi watanzania wampigie kura JK na CCM!!!!
 
Vyama vyote vingine isipokuwa CDM vina ndoa na CCM.Muungano wa nini wakati ni kuisifia CCM wakati kila mahali mambo si shwari.Mmejawa wasiwasi wa nini?
 
Mwandishi wetu, Babati (Tanzania Daima)

My take: Ni wazo makini sana, kwani adui namba moja ni mmoja. Lakini viwe vyama vya upinzani vya ukweli, sio mamluki.

NCCR ni janga ndiyo maana Mbatia anateuliwa ubunge na dhaifu. Amewaathiri viongozi wengine wa NCCR wanatafuta kuwa CCM na kuwa wapinzani. Haiwezekani. Wajitahidi tu wavunje chama wakabidhi mali za chama CCM.
 
Hii mbinu imetumika kwa muda mrefu sasa; kupakaza kwamba vyama vingine vina ndoa na CCM isipokuwa CDM. Ni mbinu ya kichovu tu. Anayedanganywa hapa ni nani? Kila chama cha siasa ni mshindani wa chama kingine, maana vyote vinagombea kukubalika kwa wananchi. Haishangazi kuona vinapakaziana. Waelevu hawasikilizi mipakazo bali sera na hoja zinazosaidia nchi, basi.
 
Hii mbinu imetumika kwa muda mrefu sasa; kupakaza kwamba vyama vingine vina ndoa na CCM isipokuwa CDM. Ni mbinu ya kichovu tu. Anayedanganywa hapa ni nani? Kila chama cha siasa ni mshindani wa chama kingine, maana vyote vinagombea kukubalika kwa wananchi. Haishangazi kuona vinapakaziana. Waelevu hawasikilizi mipakazo bali sera na hoja zinazosaidia nchi, basi.
Mmmm, kweli ipo kazi.
 
Back
Top Bottom