Naziona dalili za PINDA kuibuka Kidedea

Naziona dalili za PINDA kuibuka Kidedea

Jicho la Tai

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2012
Posts
1,452
Reaction score
609
Waziri mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda ni Mgombea ambaye mambo yake yameenda Kimyakimya sana mpaka Dakika za Mwisho.

Hakuna aliyejua kuwa Pinda atagombea Urais mpaka Siku ile ya tarehe 21 Octoba 2014 alipotangaza Kimyakimya na hapo ndipo wapinzani wake kupitia Vijana wao walipoanza kumwagia Shutuma mbalimbali. Kunyume na hayo ni mtu safi ndani ya Chama.

Hajawahi kujitokeza kusema sera zake hadharani kama wengine, kwanza hakutangaza nia kwenye majukwaa zaidi ya kwenda kuchukua fomu na kuzungumza na waandishi wa habari hata hivyo hakuzungumza sera za Kuomba kura zaidi ya kusema nini serikali imekifanya mppaka sasa.

Waandishi wa habari walipotaka kujua yeye ana lipi alisema hawezi kwenda huko kwani Utaratibu wa Chama husimami na kuanza kuongea lolote, mara zote wanaongozwa na ilani ya chama cha Mapinduzi. Hivyo aisema atafanya nini atakuwa amekiuka miiko kwani hata ilani haijatoka.

Nimemuona mara chache sana kwenye vyombo vya Habari tofauti na wengine. Amekuwa akiendesha kila kitu kimyakimya mpaka dakika za mwisho. Watu wengi wamekuwa wakipata wasiwasi kuhusu ukimya wake na kwa habari ambazo ni za Uhakika kutoka chanzo change ni kwamba ana Mtandao wa Wajumbe wengi ambao wanamuunga mkono kuliko hata yeye anavyotegemea.

Hakuna mwenye sababu za kumpinga ndani ya Chama chake, kama sio Rushwa kwenye uchaguzi huo basi kuna uwezekano mkubwa Akapita.
 
Hafai kuwa raisi. Hana uwezo hata chembe.
 
I.Jaji Agustino Ramadhani
2. Asha rose Migiro
3. Ghalib Bilali
4. Mizengo Kayanza Pinda
5.Makongoro Nyerere
Naona dalili za Pinda kushindwa kuanzia ngazi hii
 
I.Jaji Agustino Ramadhani
2. Asha rose Migiro
3. Ghalib Bilali
4. Mizengo Kayanza Pinda
5.Makongoro Nyerere
Naona dalili za Pinda kushindwa kuanzia ngazi hii

Makongoro hawezi kuwepo 5 bora.Amevunja kanuni kwa kuwashambulia wenzake jambo ambalo ni kosa.
 
Makongoro hawezi kuwepo 5 bora.Amevunja kanuni kwa kuwashambulia wenzake jambo ambalo ni kosa.

Uko sahihi mkuu. Amewashambulia sana. Pinda anaweza akapita. Wanaokataa hawana hoja za msingi. Wamekaririshwa
 
"Wapigwe tuu hakuna namna nyingne"huikumbuki hii kauli na baada ya kutamka hayo unaweza niambia nin kilitokea?kuweni wazalendo tuibadilishe hii nchi sio ushabik afu still bado tuna lalamika.yani kupata kiongozi bola ndani ya ccm nisawa nakutafta mwanamke bikra ndani ya wodi ya wazazi.
 
Hafai kuwa raisi. Hana uwezo hata chembe.

Jina lako tu Mfamaji hivyo Huishi kutapatapa. Unaongea kama Ukawa au Kama CCM? Wenye maamuzi hivi sasa ni Wajumbe wa CCM na sio waropokaji kama wewe
 
Last edited by a moderator:
"Wapigwe tuu hakuna namna nyingne"huikumbuki hii kauli na baada ya kutamka hayo unaweza niambia nin kilitokea?kuweni wazalendo tuibadilishe hii nchi sio ushabik afu still bado tuna lalamika.yani kupata kiongozi bola ndani ya ccm nisawa nakutafta mwanamke bikra ndani ya wodi ya wazazi.

Yani akili yako iko Limited. Kwa hiyo unataka kusema Watanzania wote waliopo CCM hawana akili yani ni Mburula kama wewe? Bado siamini hili. Af kama nakufahamu hivi. Ushawahi kutibiwa Hospitali ya Dodoma pale ile maalumu?
 
I.Jaji Agustino Ramadhani
2. Asha rose Migiro
3. Ghalib Bilali
4. Mizengo Kayanza Pinda
5.Makongoro Nyerere
Naona dalili za Pinda kushindwa kuanzia ngazi hii

Umeanza Vizuri ila Mwishoni Umechemka. Hebu rudia tena. Hivi hapo unadhani kati ya Uliowataja nani ana nguvu kuliko wote?
 
Huyu tunajua sera zake. Tutapigwa tu! CCM imejiweka pagumu yenyewe sasa ni wakati wa mavuno. Mimi sioni yeyote CCM si kwa sababu ya ufisadi, misimamo yao bali ni pamoja na uchafu wa chama kwa ujumla na hawasemi kama Warioba. Tutawaamini vipi wakati ni Chama wanasimamia ambacho ndio kibovu. Sioni ni vipi watafanya tofauti na matakwa makubwa ya chamana ndio maana hata Kikwete kashidwa pia
 
wapigwe tu mana hakuna namna nyingine sasa
 
pinda msindikizaji kama alikutuma mwam bie umekwam

Jibu kwa Hoja sio maneno ya Mtaani kwenu. Kwani wanaomsindikiza Rais Marekani huwa hawafiki wanaishia njiani? Huwa wanafika na wanakaa siku ambazo amekaa Rais. Hivyo anaweza kuwa Msindikizaji lakini akafika na akabaki wengine wakarudi. #Tusubiri
 
Makongoro hawezi kuwepo 5 bora.Amevunja kanuni kwa kuwashambulia wenzake jambo ambalo ni kosa.

Kawashambulia au kawaeleza ukweli.

Makongoro Nyerere ndiye mtia nia asiye na doa ndani na nje ya chama.
 
Yani akili yako iko Limited. Kwa hiyo unataka kusema Watanzania wote waliopo CCM hawana akili yani ni Mburula kama wewe? Bado siamini hili. Af kama nakufahamu hivi. Ushawahi kutibiwa Hospitali ya Dodoma pale ile maalumu?

Mkuu sio suala la akili hapa. Kama ni wasomi wengi wapo CCM no question about it, kama ni wenye uzoefu nk ni CCM. Lini suala ni mfumo wake ulivyo mbovu haiwezekaniki hata angechaguliwa mtu articluated kiasi gani akatufaa. This is the problem. Jibu ni kuitupilia mbali waende wake china wavunje mfumo wao warudi tena kutuomba wakiwa na mfumo tutakao uona sasa safi. Mbona haya mambo ni wazi. Hata Brazil/German?Spain etc zikifungwa kwenye kombe la dunia kocha anajiuzuru,timu inasukwa upya, ikirejea ni moto wa kuote mbali. sababu wanapata muda wa kureflect makosa yao.
 
Back
Top Bottom