"Haina tabibu
ndwele ya mapenzi"
ndugu wana mmu hayo si maneno yangu, ni malenga wetu hao wanaelezea jinsi mahaba yalivyo na thamani ya pekee.
"Hakukuwa
kupendana, bila
kuheshimiana"
"swadakta" hapo juu ndo penye kiini cha mshawasho wangu wa kuamua kuliumiza dole gumba langu kuandika maneno haya mujarabu kwa watu shupavu wa mmu.
Ndugu zangu mwenzenu yamenikuta makubwa. Mimi nimeoa nikiwa mtu mzima sana. Tofauti ya umri na mke wangu ni miaka kumi na kenda. Miezi sita ya kwanza ndoa yetu ilikuwa ya furaha sana na hakika nilionja raha majinuni ya ndoa. Baada ya hapo ni mateso makubwa sana.
". Hasikii la
mwadhini wala la
mtia maji msikitini"
Mke wangu kaanzisha tabia chafu sana na isiyo mpendeza MUNGU na walimwengu pia. Ilikuwa ni mwezi wa saba wa ndoa yetu usiku wa maanani ndipo kiini cha dukuduku langu lilipoanza. Baada ya kufanya tendo la ndoa kwa raundi ya kwanza ndipo mke wangu mpendwa aliponiomba "twende chooni" akimaanisha nimwingilie kinyume na maumbile.
Kwakweli ilibidi nifanye ili kumridhisha na kumuonya kwamba iwe ni siku ile pekee. Kuanzia hapo mke wangu kaweka msimamo kuwa hanipi haki yangu mpaka nimpe "kiu yake"
Nafikiria kumpa taraka mke wangu ukizingatia bado hatujazaa.
Naombeni ushauri wana mmu wapendwa.
". Heri kufa macho
kuliko moyo"
qoetes master.