Nawezaje kupata namba ya NIDA?

Nawezaje kupata namba ya NIDA?

Simeone

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
1,147
Reaction score
1,295
Wakuu kwema,

Umepita muda wa mwezi mmoja tangu nijiandikishe nida ili kupata kitambulisho cha Taifa, sijatumiwa sms na NIN na kawaida wanasema inachukua wiki 1 tu kutoa namba

Mwenye kujua jinsi ya kuangalia kama namba imetoka au kujua maombi yapo hatua gani anielekeze.

ASANTENI.
 
Mkuu hiyo website yao haifanyi kazi ile ni geresha tu, kama una namba ya nida hebu ifanyie majaribio uone kama itakupa matokeo sahihi.
Basi nenda NIDA iliyojirani chap
 
Mkuu hiyo website yao haifanyi kazi ile ni geresha tu, kama una namba ya nida hebu ifanyie majaribio uone kama itakupa matokeo sahihi.
Njia ya Mwisho kutoa Bure. Baada ya hapa utalipia.

Kama hujapata NIN tumia njia hii, Tuma ujumbe kwa mpangilio huu: JINA LAKO LA KWANZA*JINA LA MWISHO*TAREHE YAKO YA KUZALIWA*MWEZI WA KUZALIWA*MWAKA WA KUZALIWA*JINA LA KWANZA LA MAMA MZAZI*JINA LA MWISHO LA MAMA MZAZI kisha kutuma SMS kwenda namba 15274.

Mfano: MUSA*JUMA*02032003*MARIAM*ALI kwenda 15274. Utapokea SMS papohapo ikikujulisha hali ya Kitambulisho chako.

Zingatia: Tumia alama ya nyota (*) kati ya kila kipengele, andika majina yote kwa HERUFI KUBWA kama yalivyo kwenye fomu ya maombi.
 
Njia ya Mwisho kutoa Bure. Baada ya hapa utalipia.

Kama hujapata NIN tumia njia hii, Tuma ujumbe kwa mpangilio huu: JINA LAKO LA KWANZA*JINA LA MWISHO*TAREHE YAKO YA KUZALIWA*MWEZI WA KUZALIWA*MWAKA WA KUZALIWA*JINA LA KWANZA LA MAMA MZAZI*JINA LA MWISHO LA MAMA MZAZI kisha kutuma SMS kwenda namba 15274.

Mfano: MUSA*JUMA*02032003*MARIAM*ALI kwenda 15274. Utapokea SMS papohapo ikikujulisha hali ya Kitambulisho chako.

Zingatia: Tumia alama ya nyota (*) kati ya kila kipengele, andika majina yote kwa HERUFI KUBWA kama yalivyo kwenye fomu ya maombi.
Mkuu hata hiyo nilishajaribu hakuna chochote kinachojibiwa.
 
Jibu rahisi:-
Nenda ofisi za NIDA zilizo karibu yako ili ukapate ufafanuzi sahihi wa nini cha kufanya.
 
Back
Top Bottom