Nawezaje kuondoa matangazo kwenye android?

Nawezaje kuondoa matangazo kwenye android?

Wakuu naomba msaada wenu kuondoa matangazo kwenye sim.

Hii ni mwra yangu ya kwanza kutumia android maana nilikua natumia window ila juzi hapa nimeamua kuanza kutumia android* matangazo yanataka kuniua.

Yani matangazo yanakuja kwa fujo, unaondoa tangazo linarudi, kidogo tena linarudi hii mambo window haipo kabisa.

Nisaidieni niweke app gani za kuniondolea huu ujinga wakuu.

Msaada wenu ntaupokea kwa mikono miwili.
 
Kuna app inaitwa Adaway hiyo kwa matangazo ni kiboko ukiiweka tu matangazo yote kwisha ila bila root haiwezekani
 
Sasa wewe hutaki matangazo unadhani developer naye atanufaika VP na kazi yake basi Kama VP lipia ili mnufaishe developer na upate app ambayo ni free ads. Anyway unaweza tumia ADBLOCKER haipatikani playstore Google utaipata ila kiukweli sio fair kabisa.
 
Sasa wewe hutaki matangazo unadhani developer naye atanufaika VP na kazi yake basi Kama VP lipia ili mnufaishe developer na upate app ambayo ni free ads. Anyway unaweza tumia ADBLOCKER haipatikani playstore Google utaipata ila kiukweli sio fair kabisa.
kweli hii ni dhulma
 
Habari zenu bandugu,
Naomba mwenye kujua namna ya kuzuia haya matangazo(ADS) yanayotokea kwenye simu za smartphone, yananikera sana maana unakuta unajambo la maana unafanya, mara linapita tangazo.

Tafadhali mwenye kujua.
 
Habari zenu bandugu,
Naomba mwenye kujua namna ya kuzuia haya matangazo(ADDS),yanayotokea kwenye simu smartphone,yananikera sana maana unakuta unajambo la maana unafanya,mara linapita tangazo.
Tafadhali mwenye kujua
Mie nafanyaga hivi Hatua ya kwanza iroot hiyo simu
Ukisharoot niambie
 
Ku "root" ndiyo nini, na huyo anaesema ukifunga data sasa unafunguaje application wakati kwenye net?
 
Wadau nimeanza kupata hii shid
1476607390704.png
1476607401351.png
a toka juzi, natumia Tigo na simu ni note 4..hizi ads zimekuwa kero na pia zinanipeleka direct google play na muda mwingine ads za porn zinakuwa displayed!!
Je solution ya hii kitu ni nini??
 
Back
Top Bottom