Nawezaje ku upgrade simu ya 3G kwenda 4G

Nawezaje ku upgrade simu ya 3G kwenda 4G

socket

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2014
Posts
305
Reaction score
434
Habari zenu bandugu.
Mwenye utaalamu wa ku-upgrade simu yenye uwezo wa 3G kwenda 4G anisaidie.
 
kitu kama hicho hakiwezekani kamwe.
uza hiyo simu ya 3G nunua yenye uwezo wa 4G
 
[emoji4] [emoji4] Jf siliku hizi kuna kila aina ya pumba na chuya zamani kulikuwa kunamwagwa michele humu mpaka tunaogopa

wakuu kina Watu8 jukwaa limevamiwa na kizazi cha Gmail
 
mnao sema haiwezekani na kutoa majibu ya zarau hembu elezeni kitaalam kwa nini haiwezekani ili tuwaelewe basi??
 
Kubadili simu ya 3G iwe 4G haiwezekani, maana ndivyo ilivyotengenezwa kiwandani, uwezo wake ni 3G tu.

Mfano mzuri, ni sawa na kufanya jaribio la kubadili wembe uwe kisu, haiwezekani maana kimaumbo wembe hauwezi kubadilika kuwa kisu. Sasa ndivyo ilivyo pia kwa simu hizi..

Kikubwa, kama unahitaji kutumia technology ya 4G basi ni vizuri ukinunua simu yenye uwezo wa 4G..
 
4G ni hardware kwenye simu na sio software hardware ni kitu kisichoweza kubadilishwa tofauti na software so kutaka iwe hivyo ni sawa na pikpiki iwe tractor haiwezekani
 
Unawezaje kujua simu fulani kua ina uwezo wa 4G
Pia unaweza kuangalia sifa za simu husika kwenye upande wa connectivity (Maelezo hayo yanaweza kuwa kwenye box la simu, user manual au unaweza kuangalia kwenye mtandao).

Kama imeandikwa "4G/LTE - Yes" maana yake ina uwezo wa 4G, ila ikiwa "4G/LTE - No" basi haina uwezo.
 
Back
Top Bottom