Naweza kuthibitisha uhalisia wa VISA niliyotumiwa?

Nyamtinga

Member
Nov 12, 2022
20
30
Habari ya wakati huu, wakuu?

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27, na ni ndoto zangu kwenda nchi ya Canada au ughaibuni popote tofauti na bara la Asia kusoma na kutafuta maisha. Nina shahada ya sheria, lakini hata hela ya kwenda pale Law School ni tatizo. Kama kijana nisiye na manung'uniko na kulaumu mzazi kutoniendeleza, nimefanya jitihada kadhaa mpaka sasa, kuomba scholarship na najinoa pia lugha kwa ajili ya mitihani ya IELTS.

Lakini katika mizunguko yangu, kuna mzungu mmoja ambaye hatufahamiani aliniuliza maswali kadhaa, na kwa kuwa anuani yake inaonesha yupo Canada, Jimbo la Quebec, nilimuomba kama kuna namna naweza kwenda nchi yao. Akasema ipo, akanitumia fomu ya VISA ambayo ilikuwa kwa lugha ya Kifaransa. Nikatafuta watu, nikawalipa wakanisaidia kuijaza.

Baadaye, akaniambia nitume hela kwenda huko kwao kwa ajili ya kuthibitisha taarifa zangu, hapo ni baada ya kupokea barua pepe kadhaa zinazoonesha kwamba taarifa zangu zimepokelewa. Nikaamua kwanza elimu yangu inisaidie, maana kusikia cha kike kuingia ni rahisi sana.

Nikadelay kulipia kiasi hicho cha shilingi laki mbili na hamsini, nikamuambia sina, labda next round. Lakini amekuwa mtu anayenisisitiza kuwa ameomba faili langu lihifadhiwe na wamekubali. Nifatilie passport, NIDA, na ripoti ya matibabu, halafu nilipie na pesa.

Kwa kuwa sio mtu tunayefahamiana zaidi ya mitandaoni, naingiwa mashaka, na hili linanileta jinamizi. Ninaomba kujua jinsi ya kuthibitisha taarifa zangu kama kweli zipo Canada. Kwa mwenye ujuzi, naomba anisaidie.
 
Ama kweli chuoni siku hizi vijana wanaenda kujifunza ujinga. Sio kwamba hujui unatapeliwa tatizo hutaki kukubali ukweli.

Acha kujidanganya kuwa mtu huru jiamini unaweza, unajua, huhitaji kupoteza muda wako kwa vitu usivyovijua na visivyokuwepo.

Ni wengi wanakutana na hali ya kutatiza kama yako, sijui shida ni nini! Vijana tunataka maisha maraisi. Mtu tu kutoka mtandaoni akutumie labda computer, simu ...sio rahisi.

Maisha ni win ... Win ..game. Nipe nikupe nadhani ata kwenye sheria unajua tofauti ya Void and legal contract.
 
Visa wanatoa Ubalozi mkuu hao ni matapeli sishangai wewe kutokujua hivyo vitu maana vitu vingine unakutana navyo hali ikiwa Ngumu...application za visa za Ubalozi zipo mtandaoni hata wewe unaweza kudownload na ukawatumia watu usiendelee kumtumia pesa ni za bure hizo wahuni wanachukua kitu chochote na wana watu aina yako wengi wanawafanya waendelee kutapeli...
 
Visa wanatoa Ubalozi mkuu hao ni matapeli sishangai wewe kutokujua hivyo vitu maana vitu vingine unakutana navyo hali ikiwa Ngumu...application za visa za Ubalozi zipo mtandaoni hata wewe unaweza kudownload na ukawatumia watu usiendelee kumtumia pesa ni za bure hizo wahuni wanachukua kitu chochote na wana watu aina yako wengi wanawafanya waendelee kutapeli...
Asante sana mkuu, bila shaka maoni haya ni msaada mkubwa kwangu
 
Ama kweli chuoni siku hizi vijana wanaenda kujifunza ujinga. Sio kwamba hujui unatapeliwa tatizo hutaki kukubali ukweli.

Acha kujidanganya kuwa mtu huru jiamini unaweza, unajua, huhitaji kupoteza muda wako kwa vitu usivyovijua na visivyokuwepo.

Ni wengi wanakutana na hali ya kutatiza kama yako, sijui shida ni nini! Vijana tunataka maisha maraisi. Mtu tu kutoka mtandaoni akutumie labda computer, simu ...sio rahisi.

Maisha ni win ... Win ..game. Nipe nikupe nadhani ata kwenye sheria unajua tofauti ya Void and legal contract.
Ha ha ha, ushauri mzuri nimejifunza.
 
Hapo hamna cha Mzungu wala Mwanamke...!

Hapo mtu yupo zake Lagos nyuma ya Computer, anatafuta Mazuzu.
Ni kweli hao majamaa wa Lagos hawafai, japo nimeona nisikurupuke kwanza, niulizie uhalisia naona sasa nimpotezee tu kabla sijalizwa
 
Habari ya wakati huu, wakuu?

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27, na ni ndoto zangu kwenda nchi ya Canada au ughaibuni popote tofauti na bara la Asia kusoma na kutafuta maisha. Nina shahada ya sheria, lakini hata hela ya kwenda pale Law School ni tatizo. Kama kijana nisiye na manung'uniko na kulaumu mzazi kutoniendeleza, nimefanya jitihada kadhaa mpaka sasa, kuomba scholarship na najinoa pia lugha kwa ajili ya mitihani ya IELTS.

Lakini katika mizunguko yangu, kuna mzungu mmoja ambaye hatufahamiani aliniuliza maswali kadhaa, na kwa kuwa anuani yake inaonesha yupo Canada, Jimbo la Quebec, nilimuomba kama kuna namna naweza kwenda nchi yao. Akasema ipo, akanitumia fomu ya VISA ambayo ilikuwa kwa lugha ya Kifaransa. Nikatafuta watu, nikawalipa wakanisaidia kuijaza.

Baadaye, akaniambia nitume hela kwenda huko kwao kwa ajili ya kuthibitisha taarifa zangu, hapo ni baada ya kupokea barua pepe kadhaa zinazoonesha kwamba taarifa zangu zimepokelewa. Nikaamua kwanza elimu yangu inisaidie, maana kusikia cha kike kuingia ni rahisi sana.

Nikadelay kulipia kiasi hicho cha shilingi laki mbili na hamsini, nikamuambia sina, labda next round. Lakini amekuwa mtu anayenisisitiza kuwa ameomba faili langu lihifadhiwe na wamekubali. Nifatilie passport, NIDA, na ripoti ya matibabu, halafu nilipie na pesa.

Kwa kuwa sio mtu tunayefahamiana zaidi ya mitandaoni, naingiwa mashaka, na hili linanileta jinamizi. Ninaomba kujua jinsi ya kuthibitisha taarifa zangu kama kweli zipo Canada. Kwa mwenye ujuzi, naomba anisaidie.


Rudisha ada za mzazi wako.
 
Habari ya wakati huu, wakuu?

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27, na ni ndoto zangu kwenda nchi ya Canada au ughaibuni popote tofauti na bara la Asia kusoma na kutafuta maisha. Nina shahada ya sheria, lakini hata hela ya kwenda pale Law School ni tatizo. Kama kijana nisiye na manung'uniko na kulaumu mzazi kutoniendeleza, nimefanya jitihada kadhaa mpaka sasa, kuomba scholarship na najinoa pia lugha kwa ajili ya mitihani ya IELTS.

Lakini katika mizunguko yangu, kuna mzungu mmoja ambaye hatufahamiani aliniuliza maswali kadhaa, na kwa kuwa anuani yake inaonesha yupo Canada, Jimbo la Quebec, nilimuomba kama kuna namna naweza kwenda nchi yao. Akasema ipo, akanitumia fomu ya VISA ambayo ilikuwa kwa lugha ya Kifaransa. Nikatafuta watu, nikawalipa wakanisaidia kuijaza.

Baadaye, akaniambia nitume hela kwenda huko kwao kwa ajili ya kuthibitisha taarifa zangu, hapo ni baada ya kupokea barua pepe kadhaa zinazoonesha kwamba taarifa zangu zimepokelewa. Nikaamua kwanza elimu yangu inisaidie, maana kusikia cha kike kuingia ni rahisi sana.

Nikadelay kulipia kiasi hicho cha shilingi laki mbili na hamsini, nikamuambia sina, labda next round. Lakini amekuwa mtu anayenisisitiza kuwa ameomba faili langu lihifadhiwe na wamekubali. Nifatilie passport, NIDA, na ripoti ya matibabu, halafu nilipie na pesa.

Kwa kuwa sio mtu tunayefahamiana zaidi ya mitandaoni, naingiwa mashaka, na hili linanileta jinamizi. Ninaomba kujua jinsi ya kuthibitisha taarifa zangu kama kweli zipo Canada. Kwa mwenye ujuzi, naomba anisaidie.
Katika maombi ya Visa Kuna serial number.Fika ubalozi wa Canada upo baada ya makaburi ya Kinondoni Jengo lenye Ofisi za Benk ya kilimo opposite na ilipo DSTV watakuangalizia kwenye Server zao! Kama ni kweli umo utaonekana wewe na details zako! Asije akawa mzungu Mnaija anataka kukupigia hela! Visa ya Canada niliwai mjazia mtu mmoja jamaa angu toka Burundi .100% unajiandikisha na Kujaza info zote online ni web based na unaweza jaza kwa English au kifaransaJamaa alipata now yupo Canada.Garama yake andaa kama Dola 200..pale Kuna dogo an ofisi ana saidia wale wanataka kusaidiwa kujza maombi ya Visa kwa ujira mdogo
 
Back
Top Bottom