Naweza kabisa kuituliza Zanzibar

Naweza kabisa kuituliza Zanzibar

Namshukuru manani leo ndio mara yangu ya kwanza kusoma comments za ma great thinker ambao hawaku base udini wala siasa wala kumponda mtu mungu akubarikini

Nashukuru kwa kuliona na kulitambua hilo.Nina kiu na hamu kuiona Zanzibar yenye utulivu.Amani ni haki ya kwanza ya Wanzanzibar
 
kama iliandikwa kutoka kwa mungu kwamba znz itajitenga hakuna yoyote kati yetu anayeweza kuzuia,na wao wenyewe wakubali kuwa chochote kile kitakachotokea huko baada ya kujitenga kwao ni jukumu lao wenyewe na si watanganyika.pia wakumbuke ardhi yao ni ndogo watakapojitenga idadi yao ikiongezeka watakwenda wapi?,watalima wapi?,watafanya biashara wapi? Tujue kwamba kuna mabeberu ya kizungu,kiarabu,kichina yanapataka sana kule ajili ya kula raha tu. Je kwa wale waswahili wenzangu na mimi vipi mtayamudu maisha ya kibeberu?.ndugu zangu waznz toeni tofauti zenu zote ebu tafakalini maisha ya baadae ya jamii zenu na si vinginevyo,maana maisha ya sasa ya vijimisaada vya hapa na pale madhala yake watayaona wajukuu zenu pindi watakapokosa sehemu japo ya kupanda mchicha ama kuvua vibua.
 
CCM,ni wanafiki.wameshatoa ahadi nyingi sana za kuondoa kero za muungano na hakuna kilichotekelezwa.wananchi wamegutuka kutoka usingizi waliokuwa nao wa muda mrefu sana,sasa hawataki kabisa huo muungano.wapeni nchi yao na kutakuwa shwari kabisa.
 
kwani kwnn wanaing'ang'ania c wawaachie nchi yao?ccm hamtakiwi kule hamuelewi

Hata mimi naona hivyo

Halafu Muungano wenyewe ilikuwa ni mbinu ya Marekani ili Abdulrahman Babu asiweze kuinfluence Zanzibar ifuate mfumo wa kiCommunist. Kuna umuhimu gani tena kwa sasa?
 
Tupe mwongozo,hatua zipi utaenda kuzichukua pale walau watu wa pale wakuelewe,plan zako ni zipi!na kwanini uende wewe!Why can't you analyse all the steps&plans na ukawashauri viongozi wa ngazi za juu kuzifanyia kazi kama kweli ni workable?ukinijibu walau kidogo ntakuelewa!Zanzibar kinachohitajika ni uhuru!let her go!
 
Tupe mwongozo,hatua zipi utaenda kuzichukua pale walau watu wa pale wakuelewe,plan zako ni zipi!na kwanini uende wewe!Why can't you analyse all the steps&plans na ukawashauri viongozi wa ngazi za juu kuzifanyia kazi kama kweli ni workable?ukinijibu walau kidogo ntakuelewa!Zanzibar kinachohitajika ni uhuru!let her go!

Mkuu,nashukuru cha changamoto.Nina mambo ambayo najua tu ndio kiini cha matatizo,moto hauzimwi kwa moto,njaa hainyamazizwi kwa usingizi,kope kazi yake ni kukinga macho.Kama ni mwanafalsafa utakuwa umeisoma vision yangu hata zaidi.Ndio viongozi wapo na hakuna anayethubutu kusimamia haki na kweli.Uwe mkweli,watu wa Zanzibar wakipata mtu mwenye vision ya kweli na dhamira ya uwazi ya uwajibikaji basi itatuli(si kazi yangu).Nipate tu nafasi,Siui mtu,kwa maneno tunajenga na kubomoa.Hata hivyo si kwamba viongozi wameshindwa kufanya hayo ninayoyamaanisha,ila chawa akikung'ata maungoni hutafutwa haraka.Wanaoathirika na fujo hizo ni wengi,wanaozifanya ni wechache.Viongozi wana taabu gani?Ndio kwanza wanavuta blanket ya kujifunika.Nimeomba mchango wako uungane na wako endapo nitakwenda nikaongee 'steki' na si mifupa.Natumai umenielewa.
 
Back
Top Bottom