Imekuwa ni kawaida sana kwa kizazi cha sasa kilichozaliwakati yqa mwaka 1990 na kuja huku mbele miaka ya 2000. Imekuwa ni kawaida sanakusikia mabezo mengi tu kwamba CCM ni chama kisichofaa kuongoza. Ni kawaidausikia kwamba mwaka 2015 CCM ndo itakuwa mwisho wake. Imekuwa ni kawaida sanakusikia watu wakiombea na hata kuomba dua mbaya (na si dua nzuri) kwamba CCM kipate mikosi ilikionekane hakifai mbele za watu.
CCM kimekuwa kikibebeshwa lawama na mizigo kisichostahilikuibeba
Chama Cha Mapinduzi ni chama kinachotawala yaani ni chamakilichoshinda na kuunda serikali. Kazi ya Chama Cha Mapinduzi ni kutengenezasera ili zitekelezwe na serikali. Kinapotengeneza sera kwa mfano, sera yaajira, kasha anayezisimamia sera hizo ni serikali (serikali ni pamoja na watuwasio na mrengo wa chama chochote ama walio na mrengo wa chama tawala na vyamavya upinzani). Sera za Chama Cha Mapinduzi hazibagui maana CCM kinaamini Binadamu wote ni sawa na Kila Mtuanastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
..
Sasa utaona mtu aliyepewa mamlaka ya kuismamia utoaji waajira akafanya hivyo lakini kwa upendeleo wa kikabila ama kindugu lawama zotezinakwenda kwa CCM!!!!!Ama mtu akapewa taasisi aiendeshe lakini akawa na tamaa (greed)akafuja mali taasisi ikafa lawama zinakwenda CCM!!! Ama utakuta serikali inakamata wahujumuuchumi inawapeleka mahakamani kesiinaunguruma miaka kadhaa lakini watu wanaachiwa huru serikali inakata rufaawatu hawataki ikate rufaa. Hatimaye kesi inashindwa kuendelea kwa sababu yakelele za watu lakini lawama zinakwenda Chama Cha Mapinduzi!!!!!!!
CCM kinatengeneza sera za kujenga miundo mbinu ili wananchiwake wapate maendeleo yao lakini utakuta watu badala ya kutumia miundo mbinuhiyo katika kujiletea maendeleo watu wanatumia simu kutukanana ama kutukanawengine na hasa viongozi wakuu wanaosimamia nchi na hasa walioleta maendeleohayo ya miundombinu ya mawasiliano. Lakini lawama zote zinakwenda CCM!!!!
Watu walikuwa wanatumia masaa kumi na mbili kutoka Bukobakwenda Mutukula kiasi cha kilometa 80 tu lakini sasa wanatumia dakika 80 lakinilawama zinakwenda CCM!!! Watu walikuwa wanatumia usiku kucha kuanzia saa kumina moja jioni kwenda Tanga lakini sasa hivi ni masaa manne na nusu hadi matanotu lakini bado lawama zinakwenda CCM!!!! Zamani nchi ilikuwa giza tupu hasanyakati za usiku lakini sasa nchi inangaa na mataa usiku (mataa ya TANESCO,SOLA, TOCHI NA TAA ZA KICHINA NK). Mpaka muuza mkaa antumia taa!!!! Lakinilawama zote zinakwenda CCM!!!!!
Sera za nchi zilizowekwa na CCM kwamba kila raia mwenye umriunaokubalika kisheria anayohaki ya kupiga na kupigiwa kura lakini watuwanashindwa kuelewa haki hiyo. Wanajichanganya kwamba haki ya kupigiwa kuramaana yake kushinda uchaguzi!!! Wakishindwa lawama zinakwenda CCM wakatiwaliopiga kura si wanachama wa CCM pekee
..
Watanzania tukumbuke tulikotoka
.Tuwaelimishe vijana wasasa wasiojua dhiki na taabu za maisha
Wanaodhani haki yako unaweza kuipata kwakutukana watu
Mimi niwaulize hata hao baba za watoto hao (au hata watu wazima)wanaoshabikia anguko la CHAMAkilicholeta maendeleo haya tuliyo nayo sasa. Kwamba motto wako akija leo hiiakakuomba pesa ya shule kwa nguvu na matusi juu, je utampa? Na hata kama utampautampa ukiwa na furaha moyoni? Au motto wako aje kukulaumu wewe mzazi kwambaumesababisha umaskini katika familia wakati huohuo anataka umwandikishe awemrithi wa mali zako
..!!!! Inaingia akilini kweli????
Msitulazimishe kujiunga na vyama vyenye tabia hiiniliyoitaja hapa juu na wala si lazima wote tuwe mashabiki wa vyama vya siasa,Maana siasa haikufanyi ufaulu Engineering, Information Technology, Accountancy,Sociology ama taaluma zinginezo bali taaluma itabaki kuwa taaluma na siasaitabaki kuwa siasa. Wengine hawahitaji kuwa wanasiasa
.Wanataka kuwa raia wakawaida wajiajiri na wajiajiri. Sera za ajira na kujiajiri ziko wazi na walaserikali ya CCM haijazizuia ama kubagua watu. Kama una mtaji wako mwagamabilioni yako ujenge viwanda na CCM inatakulinda kwa sera zake. Ukikutana navikwazo inabidi kujiuliza ni wapi umekwama na si kuanza kulaumu.
Ni wapi CCM inakataza wawekezaji wazawa wasiwekeze?
Ni wapi CCM inakataza wafuasi wa vyama vya upinzaniwasiajiriwe?
Ni wapi CCM inazuia wananchi kujiunga na vyama vya siasa?
Ni wapi CCM inazuia vyama vya upinzani vitakaposhikamadaraka visitumie ikulu ya magogoni?
Ni wapi CCM inaiamuru serikali iwanyonge wapinzani?
Ni wapi CCM ikitukanwa imekwisha kwenda mahakamani?
Ni wapi chama cha upinzani duniani kilishawahi kushindauchaguzi kwa sera za ukanda?