Hahaa hivi paka huwa wanafanyia mapenzi chumbani? Sijawahi kuwaona aiseeKatika viumbe vinavyo endekeza mapenzi ni paka, ukimuweka dume sehemu ambayo hakuna mademu anaweza akahamia mtaa wa pili kurekebisha.
Hapana mambo yao sio chumbani.Hahaa hivi paka huwa wanafanyia mapenzi chumbani? Sijawahi kuwaona aisee
Hakika umenena iliyo kweli.Napenda paka.
Tangu utoto nyumbani hapakosekani paka na nimeshawazoea.
Paka wana Upendo sana na wanatambua ukiwa unaonyesha Upendo kwao.
Raha sana pale unaporudi akishakuona tu unaanza kukupokea kuanzia mbali na anakaa karibu yako.
Hata ukiishi peke yako hutohisi upweke ukifuga huyu mnyama.
Na katika wanyama siwapendi na nawaogopa ni mbwa.
Dume nae huwa anasepaNiliokota paka akiwa mdogo nikampeleka nyumbani, baada ya kukua nikajua kumbe jike.
Madume yakawa hayakauki na zile kelele zao wanazopiga wakiwa kwenye heat utasema mtoto mchanga.
Yule paka alikua anazaa kwa frequency ya mwaka mmoja mara mbili halafu watoto wakifika umri fulani anawatorosha, mwisho na yeye akatoroka.
Nimeamua nikifuga paka awe dume, labda yale hayatojirudia.
Dah kweli tunatofautiana
Huyo jirani yetu paa lake la nyumba lipo wazi sasa pamekuwa makazi ya paka ,wamejazana wanakera vibaya
Usiku hatulali makelele zao tu juu ya bati Mara waingie ndani wapige mikelele
Ila nimeshatagaza vita nao kuna mmoja nilimwagia maji ya moto ili hasikii
Mkuu njoo uwasombe hawa paka utakuwa umenisaidia ..kila nikiwafukuza hawasikii
Kweli hata baada ya tukio nilihudhunikaMie pia sipendi mapaka Mkuu, lakini hiyo ya kummwagia maji ya moto ulivuka mipaka.
Kweli hata baada ya tukio nilihudhunika
Ila walinikera mpk nilichukua hatua hiyo ni wabishi sana halafu mm nina kasuku wangu nawafuga ,hawa paka lzm waingie halafu wapo wengi kila mbinu ya kuwatimua imeshindana wanakaa ndani ya bati. Kuna nyakati silali kwa ujinga wao halafu wezi ,nahofia kasuku sabb hawaaminiki ,sabb iliyonisukuma kuna usiku sikulala kabisa wanaingia ndani wanapigana wanapiga mikelele natoka kuwafukuza lkn wanarudi..hawa paka miezi kibao karibia mwaka wanasumbua tu na hakuna dalili ya wao kuondoka ,nikiwa harsh wataogopa ,nikiwadekeza wataendeleza ujinga
Miss Queen huwapendi? Tangu utoto wangu mpaka leo popote nitakapoishi kama hakuna paka sijisikii vema kabisa.
Mkuu ulimfundishaje??Ninae wangu ni dume na nilimfundisha mengi tangu utoto wake kwanza haibi mpaka umpe, pili hata kama nyumba imefungwa hakuna watu hatokwenda kwa jirani na nikirudi ananifuata kuanzia mbali kwa upendo mkubwa.