Wanaume tunadhani kuwa ukioa tu ndio unakuwa na mamlaka ya kufanya lolote kwa mwenza wako,mbaya zaidi alidhani mkewe kazini anafanya kazi na wanawake wenzake peke yake bila wanaume kitu ambacho anashindwa kuelewa kuwa huwa inafikia kipindi masuala ya kazini hulazimika kuja mpaka nyumbani kwa dharula.Kweli kaka lakini pia amesahau kwamba simu ya mkewe si ya kwake, hatakiwi kuipokea mkewe akiwepo. ninaamini asingepokea yote haya yasingetokea
Hukunisoma vizuri lara 1 mimi huwa sipigii mke wa mtu kijinga jinga hivyo kwani mwenyewe nina mke nafahamu kero hii, kilichotokea ni kwamba simu alipiga mtoto akiwa anaichezea, sema kosa nililolifanya ni kutokui-lock na kuiweka mahala asipoweza kufikia mtoto
Ngalikihinja ushauri wako mzuri sana,jamaa akiufuata utamsaidiaRidhiko la bwana mawivu halitapattikana kwa huyu jamaa kuacha kuwasiliana na mke wa bwana mawivu, bali kwa kupata uhakika kuwa mkewe hajabanduliwa na jamaa. Na uhakika wa hili utapatika kwa jamaa kuhusisha polisi nq ndugu wengine, basi. Akae kimya then what next? Bwana mawivu akishaona ishu imehusisha watu tofauti, wakiwemo polisi, atageuka kuwa mlinzi wa ndugu yetu huyu maana anajuwa jamaa akipata madhara, mtuhumiwa wa kwanza atakuwa yeye...
Lara 1, kwenye maisha yako hadi leo, hujawahi singiziwa kuwa unatembea na fulani wakati si kweli? How did you handle it? Maana kuna wengine wakisingiziwa tu basi wanaamua kfanya kweli.
Sikulaumu na pia sikutetei....kuna mambo ambayo tunapaswa kuyawekea tahadhari toka mwanzo hasa tunapokuwa tunawasiliana na wake/waume za watu ..Na wewe inaonyesha uli-mess up from the day go..mfano hata wewe ukijiweka kwenye nafasi ya huyo jamaa ..afu mtu unayemhisi ampigie simu mkeo ..asiongeee..lolz..nahsi utaona ambavyo ni ngumu sana kuaminika kirahisirahisi...
La kwanza jifunze namna bora ya kuishi na mke wa mtu hata kama mnafanya kazi pamoja (distancing)...La pili, kuhusu hili jambo kama una mke mshirikishe kwanza ili ajue kilichokutokea na hata likitokea la kutokea akupe support (manake unaweza kupoteza huku na kule)..Then, usifanye mawasiliano yeyote na huyu dada..hell no...naaamini kama hamkuwa na kitu chochote the truth will set you free..........................
Hata kama unapigiwa simu usiku, kwanini hataki kuutafuta ukweli? Hapo ndo kwenye tatizo la bwana mawivu. Kwani nani kasema sms zikiwa nyingi inamaanisha ngono? Inawezezekana hata hiyo sms moja tu ikaashiria tatizo. Bwana mawivu anatakiwa kuutafuta ukweli na si kuendeshwa na hisia.!!!
Tatizo inaonesha huwa unampigia sana kuhusiana na kazi hata kipindi ambacho sio cha kazi. We unafikiri utajisikiaje uko na mkeo unakula denda kwa raha zako. Mara kisimuKipi bora huyu dada angebaki ofisini kumalizia majukumu yake yenye deadline kesho yake asubuhi au aende akampokee mpenzi wake ila aendelee kuwasiliana na watu aliowaacha ofisini kupata msaada wa kumaliza kazi yake?
Hata kama unapigiwa simu usiku, kwanini hataki kuutafuta ukweli? Hapo ndo kwenye tatizo la bwana mawivu. Kwani nani kasema sms zikiwa nyingi inamaanisha ngono? Inawezezekana hata hiyo sms moja tu ikaashiria tatizo. Bwana mawivu anatakiwa kuutafuta ukweli na si kuendeshwa na hisia.!!!
Huyu jamaa anampenda sana mkewe kiasi kwamba anakuwa na wivu wa kijinga, na tunaomfahamu huyu dada hapa ofisini hana tabia anazomzania labda huko mtaani kwao...mimi kinachoniuma ni huyu dada ikivunjika ndoa yake ilihali hana kwasababu yangu na akiwa hana uhusiano wowote na mimi
Well said mkuuWanaume tunadhani kuwa ukioa tu ndio unakuwa na mamlaka ya kufanya lolote kwa mwenza wako,mbaya zaidi alidhani mkewe kazini anafanya kazi na wanawake wenzake peke yake bila wanaume kitu ambacho anashindwa kuelewa kuwa huwa inafikia kipindi masuala ya kazini hulazimika kuja mpaka nyumbani kwa dharula.
Mimi simu ya mke wangu sina haja nayo na nikitaka kumfuatilia si mpaka nisubiri apigiwe simu kuna mbinu nyingi tu za kufanya,huyu jamaa kachemka sana.
Hapo cha muhimu tafuta watu wazima wamuone mumewe wamueleze kila kitu...halafu baada ya hapo acha kabisa kuwasiliana na wake za watu ............
....angekwepo JF na yeye mume amwage mashitaka yake ungeshangaa sana kiasi anachokutuhum. usichukulie rahisirahisi. kama umeoa uwe bize na mkeo bana.