Kwanza combination yake unapoingia form five ni Physics, Chemistry na Biolology (PCB), au Chemistry, Biolology, Geography (CBG).
Anyway siku hizi University zimekuwa kibao hivyo maadam una Biology na Chemistry basi kuna kila linalowezekana ufike form six na baada ya hapo usomee udaktari.
Zamani Chuo kilikuwa nikimoja tu hapa nchini yaani Muhimbili. Sasa vimeenea kila kona. Kuna Kairuki, Kuna Bugando nasikia Ifakara nako kumefunguliwa. Du viko tele.
Turudi kwenye yale masomo yaani Biology, Chemistry, Physics. Hakuna aliyepita sekondari asisimulie kuhusu masomo haya. Na ndiyo yanayoongoza kwa wanafunzi kufeli. Hivyo ni masomo magumu kuliko maelezo.
Najua kuna watu wanayatandika A au B lakini inabidi uwe kichwa kwelikweli.
Serikali inajua ugumu wa msomo hayo, inajua wanafunzi wanayachukia. Inafanya kampeni nyingi kusisitiza wanafaunzi wasichukie masomo ya sayansi.
Lakini wakati serikali inasisitiza tukimbilie masomo haya, tunaona madaktari ni moja ya fani chache za sayansi zinazoongoza kwa migomo. Kuanzia mwaka 2000 hadi leo si chini ya migomo sita.
Lakini sijawahi kusikia meneja wa kamouni akigoma. Sijawahi kusikia Waziri akigoma. Sijawahi kusikia mahakimu au majaji wakigoma. Tena wale wasiogoma masomo waliyosoma utaona wengi ni yale kama history, geography, Kiswahili, English, French kwa kifupi yanaitwa arts.
Sasa kwa nini kama ninasoma nijihangaishe na masomo maguumu ya kuumiza kichwa wakati najua nikianza kazi nitaumiza kichwa tena kugoma na kuamziwa nichague kuendelea na kazi au nifukuzwe kazi.
Hivyo, nimeamua sitaki udaktari kwa sababu ambazo sasa hata mtanzania wa umri wa miaka sita najua. Udaktari na migomo ni pete na kidole.
Nataka kazi zile ambazo zitanifanya niwe na nyumba Mbezi_Beach (Dar), Capri_Point (Mwanza) na sehemu ya mji wowote ambako tunapaita "Uzunguni".
Nitakuwa wa ajabu kumshawishi mwanafunzi asomee udaktari. Asomee wa nini? Umsaidie nini?
Niseme nisiseme> Ninataka mwanafunzi asome awe mbunge au Waziri. Na ndiyo maana na wao siku hizi wanafunga safari nyingi kwenda kutembelea Bunge ili siku moja waje wawe wabunge waachane na njaa ya kugomagoma ya udaktari.
Cheers
Anyway siku hizi University zimekuwa kibao hivyo maadam una Biology na Chemistry basi kuna kila linalowezekana ufike form six na baada ya hapo usomee udaktari.
Zamani Chuo kilikuwa nikimoja tu hapa nchini yaani Muhimbili. Sasa vimeenea kila kona. Kuna Kairuki, Kuna Bugando nasikia Ifakara nako kumefunguliwa. Du viko tele.
Turudi kwenye yale masomo yaani Biology, Chemistry, Physics. Hakuna aliyepita sekondari asisimulie kuhusu masomo haya. Na ndiyo yanayoongoza kwa wanafunzi kufeli. Hivyo ni masomo magumu kuliko maelezo.
Najua kuna watu wanayatandika A au B lakini inabidi uwe kichwa kwelikweli.
Serikali inajua ugumu wa msomo hayo, inajua wanafunzi wanayachukia. Inafanya kampeni nyingi kusisitiza wanafaunzi wasichukie masomo ya sayansi.
Lakini wakati serikali inasisitiza tukimbilie masomo haya, tunaona madaktari ni moja ya fani chache za sayansi zinazoongoza kwa migomo. Kuanzia mwaka 2000 hadi leo si chini ya migomo sita.
Lakini sijawahi kusikia meneja wa kamouni akigoma. Sijawahi kusikia Waziri akigoma. Sijawahi kusikia mahakimu au majaji wakigoma. Tena wale wasiogoma masomo waliyosoma utaona wengi ni yale kama history, geography, Kiswahili, English, French kwa kifupi yanaitwa arts.
Sasa kwa nini kama ninasoma nijihangaishe na masomo maguumu ya kuumiza kichwa wakati najua nikianza kazi nitaumiza kichwa tena kugoma na kuamziwa nichague kuendelea na kazi au nifukuzwe kazi.
Hivyo, nimeamua sitaki udaktari kwa sababu ambazo sasa hata mtanzania wa umri wa miaka sita najua. Udaktari na migomo ni pete na kidole.
Nataka kazi zile ambazo zitanifanya niwe na nyumba Mbezi_Beach (Dar), Capri_Point (Mwanza) na sehemu ya mji wowote ambako tunapaita "Uzunguni".
Nitakuwa wa ajabu kumshawishi mwanafunzi asomee udaktari. Asomee wa nini? Umsaidie nini?
Niseme nisiseme> Ninataka mwanafunzi asome awe mbunge au Waziri. Na ndiyo maana na wao siku hizi wanafunga safari nyingi kwenda kutembelea Bunge ili siku moja waje wawe wabunge waachane na njaa ya kugomagoma ya udaktari.
Cheers