Natubu: Nilikuwa simuelewi Mwamposa, ila kwa idadi ya viwete walioponyeshwa Songea naanza kumuamini

Sijaona mtu wa Mungu ana mitusi kama wewe. Nilifikri utageuza shavu la pili, kumbe tukikuambia Mwamposa ni tapeli unakasirika. Basi usingeleta hii mada huku. Usijekutuiambukiza ujinga na sisi tukakubali kutapeliwa. Hata wale wa Kalynda walitumwa kuaminisha watu ule utapeli ilikuwa ukombozi wa umaskini. Kama Mwamposa anazo hizo nguvu, kwa nini analilia sadaka. Si amuombe amshushie $ na Euro kuliko kuwanyang'anya maskini kile kidogo walichonacho kwa kuwadanganya Mungu atawarudishia mara saba! Tapeli na mwizi wa imani huyo nabii wako.
Rubbish.🗑️
 
Unafact gani kusema yule ni tapeli?
Kalipa watu tsh 50 ku-act mlichokiona...

Dini ni biashara kama biashara nyingine!

Sometimes, wanaandaliwa miezi kadhaa ya nyuma, wanakuja walemavu au wagonjwa wanaishi nanyi then anakuja kwa mkutano na kujifanya kuwaponya. Baada ya mkutano hamuwaoni tena.

Siri ya vita ni wale walinzi wake, wengi husambazwa ktkt ya kusanyiko ili kudhibiti wachunguzi kama sisi...ile ni biashara haramu kama nyingine, lazima ilindwe

Ref: Mfalme Zumaridi
 
Tupe sababu 5 za kusema anafanya utapeli.

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu hilo ni swala la imani so hata kama nikikupa sababu mia bado huwezi nielewa kwani imani yako iko kwake kama ambavyo imani yangu haiko kwake
 
Anaendaje Songea wakat kuna walemavu kibao pale k koo,angeanz na wale
Ili upone lazima uamini,hao wa kkoo wanaamini kuwa watapona kwa jina la Yesu?..nikushaur kakusanye hao wa kkoo wafundishe kuamin halafu wapeleke kwenye maombez nao watapona..usijichoshe kumkebehi mtu ambaye Mungu anamtumia kama chombo kuponya watu.
 
Hizi mimi naita mbuzi!

Dhumuni la Mungu kuweka viongozi wa kiroho katikati ya watu wake toka mwanzo lilikuwa ni ili wawakumbushe watu namna nzuri ya kujiandaa na maisha baada ya kifo ila hawa fake pastors wanachokazana siyo kuwaambia watu wasizini,wasiibe wasioneane kijicho au kusemana vibaya wao wanawaambia wajiandae kupokea magari huku kazi hawana,wanawaambia wapokee nyumba hata bei ya misumari hawaijui wengine wanaambiwa pokea mtoto huku vizazi walishavitoa kwenye matukio ya utoaji mimba.

Mtu anajiita mtumishi wa Mungu lakini anakuhubiria mafanikio ya kidunia toka mwanzo wa ibada mpaka mwisho wa ibada mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka hakuna alipokukumbusha usitende dhambi yeye ni utapandishwa cheo,kazi uliyoomba utapata hakwambii kasaidie watoto yatima na wasiojiweza huko mitaani yeye ni "toa sadaka injili isonge mbele,toa sadaka kwenye madhabahu ya bwana ndo utabarikiwa” anafunga hesabu anaondoka kesho tena hivyo hivyo hakwambii ni kwa namna gani hayo yatakufaa baada ya maisha ya duniani?

Na ni wajanja,huwakuti kujenga sehemu kwamba hapa ndo pakuabudia maana wanajua siku ”wapigwaji” wakiamka hakuna wa kuingia humo wao wanafanya kwenye viwanja vya serikali wakifunga hesabu yao ya siku kesho tena hivyo hivyo wakichuja wanaenda kwenye fursa nyengine huku ”wapigwaji" wakihamia kwengine kupigwa.
Kwa mganga mnatoa sadaka adi hela ya mwisho ya akiba ila hamlalamikikwahyo ni halali mganga kudai sadaka ila mtumishi wa Mungu hatakiwi kudai sadaka...mganga akisema lete damu lita 100,mtu unatengeneza ajali kuzoa damu umpelekee mganga..ila kumtolea Mungu umekuj kukemea hapa tena huku ume bold kabisa...ivi huoni aibu
 
Ili upone lazima uamini,hao wa kkoo wanaamini kuwa watapona kwa jina la Yesu?..nikushaur kakusanye hao wa kkoo wafundishe kuamin halafu wapeleke kwenye maombez nao watapona..usijichoshe kumkebehi mtu ambaye Mungu anamtumia kama chombo kuponya watu.
Wanakosaje imani.? Kwahy wanafurahia hali zao.? Yn mtu n mlemavu afu akose imani kuwa anaweza kupona aisee.!
 
Bas mwamposa atakua na hela sana,maana kila siku watu wanashuhudia wamepona ..kumbe huwa anawalipa halafu hamsemi jamani...nyie watu ni wasiri sana
Wajua kwa siku anaingiza kiasi gani?
 
Sikatai kutenda makuu zaidi kwa imani ila ulishaona sehemu nyingine yesu aliponya watu kwa tope tena zaidi ya huyo mmoja? ushakaa ukajiukiza ni kwa nn miujiza haifanani? kwa sababu Yesu alitaka watu wamwamini kupitia yeye nguvu za mungu zinaponya ila si kwa kukariri watu mnaamini mafuta ya mwamposa zaidi ya kumuamini Mungu. Roho mtakatifu akishuka anaweza tumia chochote kumponya mtu ila haiwez kuwa consistent kwa sabb imani yako itahama utaamini mafuta kuliko kumuamini Mungu.

sasa mtu na akili zako unatembea na vichupa vya mafuta alafu tena mafuta yenyew mnauziwa nchi hii wajinga ni wengi mno mtu ameenda nigeria hapo kanunua uchawi wa kisasa anakuja kuwafanyia kiini macho na mtapigwa tuuu time will tell huo ni uchawi bro vichupa vya nn unatofauti gn na mtu alienda kwa mganga.
Nadhani hapa wewe umekaza fuvu yani hutaki kabisa kusikia vitu tofauti na ulivyomezeshwa.

Kwahiyo ni kosa kutumia mafuta siku zote kuponya..mbona anatumia maji..mbona anatumia keki za upako hayo mbona usemi.

Bado anaombe na watu wanapona bila hivyo vitu acha kukariri.

Kuhusu kuuziwa hivi unajua gharama za kuendesha ministry au unaongea tu..huyo mwamposa anafamilia inamahitaji hana kazi zaidi hiyo ulitaka ale nyasi..pia kumbuka uendeshaji wa ministry unamahitaji mengi..usafirishaji..ununuzi wa mitambo..marekebisho..usafi..bills kama maji umeme na mengine mengi.

Ulizani hayo mahitaji yatajilipa yenyewe..ebu tumia akili na acha kukaza fuvu..vitu vingine ni simpo logic tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Sikatai kutenda makuu zaidi kwa imani ila ulishaona sehemu nyingine yesu aliponya watu kwa tope tena zaidi ya huyo mmoja? ushakaa ukajiukiza ni kwa nn miujiza haifanani? kwa sababu Yesu alitaka watu wamwamini kupitia yeye nguvu za mungu zinaponya ila si kwa kukariri watu mnaamini mafuta ya mwamposa zaidi ya kumuamini Mungu. Roho mtakatifu akishuka anaweza tumia chochote kumponya mtu ila haiwez kuwa consistent kwa sabb imani yako itahama utaamini mafuta kuliko kumuamini Mungu.

sasa mtu na akili zako unatembea na vichupa vya mafuta alafu tena mafuta yenyew mnauziwa nchi hii wajinga ni wengi mno mtu ameenda nigeria hapo kanunua uchawi wa kisasa anakuja kuwafanyia kiini macho na mtapigwa tuuu time will tell huo ni uchawi bro vichupa vya nn unatofauti gn na mtu alienda kwa mganga.
Unaweza thibitisha kwamba alienda nigeria kununua huo uchawi??wabongo ndio mana ujinga hautishi yani kitu huna proof stori za mtaani ndio umeshikilia bango ukiambiwa leta ushahidi huna unabaki kukodoa mi macho..get a job na uache wivu wa kike.

#MaendeleoHayanaChama
 
chief huo unabii ni ujanja ujanja wa mjini umefanywa sana na wanaijeria hata ww ukitaka kuwa nabii unafahamu tu principle za deliverence na unakwenda nigeria kuchukua annoiting water unakuwa nabii kesho. ila hasara yake sasa unaingia kwny convenant na shetani na unamtumikia shetani

acha ulimbukeni wakuamini niujiza hivyo ni vitu vidogo sana hata musa alitupa fimbo ikabadilika nyoka na wale waganga wa farau wakafanya vivyo hivyo. so usidanganywe na miujiza ya kimapepo hiyo.
biblia inasema dhahiri kuwa nyakati hizi za mwisho manabii wa uongo watakuwa wengi.
na nabii asiye wa Mungu anatambulika kwa ishara moja kubwa ya kujitualia utukufu..!!
Endelea na hearsays ndio ulivyokaririshwa.

Tupe ushahidi wa mwamposa kwenda naijeria.

#MaendeleoHayanaChama
 
Acheni figisu na uongo. Ninyi hamna tofauti na matapeli wake na Kalynda, kazi kudanganya watu. Huyo Mwamposa anajiita mtu wa Mungu huku amejaa uongo na utapeli.
Utapeli gani na uogo gani..wewe ambaye sio tapeli na muongo umewapa msaada gani hao wahitaji na wagonjwa ili wasiende kwa muongo na tapeli..acha wivu wa kike.

#MaendeleoHayanaChama
 
yaani acha tu watanzania wajinga sana na hii ni kwasabb hatupendi kusoma. yaani mtu anajitokea3 zake huko mbwinde anakuja na yeye anajiita mchungaji hata degree ya theology hana ndo maana nchi km rwanda huo ujinga wemeuondoa ukitaka kufanya huduma ya makanisa hakikisha una angalau degree moja ya theologia
Hao manabii na mitume unao waamini walisomea chuo gani wakapata digrii ya thiologia? ?

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom