Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,728
- 2,259
Mwelekeo wa uchumi wa dunia sasa hivi ni kwa uchumi binafsi wa Nchi kujilinda katokana na ushindani wa nje.
Katika matukio ambayo yanatikisa uwekezaji has a katika Nchi za Latin America, hususan Argentina na Bolivia, ni Nchi hizo kuchukua hatua mahsusi KUTAIFISHA sekta muhimu za uchumi katika Nchi zao kwa manufaa ya umma.
Argentina imetaifisha kampuni ya uchimbaji mafuta,YPF ambayo ni kampuni ya uchimbaji wa mafuta na imetaifishwa mnamo April 16 mwaka huu.
Kampuni ya YPF ilikuwa inamilikiwa kwa pamoja na Nchi ya Spain.
Jana, May, 1 ,2012, nayo Nchi ya Bolivia imetaifisha kampuni ya kufua umeme, TDE, ambayo vile vile ni ya kutoka Nchi ya Spain.
Hili ni fundisho kubwa sana kwa Nchi zetu hizi, Kama Tanzania, ambazo ziko katika michakato ya "kuuza" njia kuu za uchumi kwa " kubinafsisha" viwanda na makampuni ya umma.
Wengine wetu tulikuwepo miaka ya 60's wakati hatua hii ikifanyika, KUTAIFISHA njia kuu za uchumi.
Leo tunashuhudia zoezi hili likijirudia kwa kuanzia Latin America.
Kuishi kwingi, kuona mengi, and what goes around, comes around!!
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere must be turning in his grave today.
Katika matukio ambayo yanatikisa uwekezaji has a katika Nchi za Latin America, hususan Argentina na Bolivia, ni Nchi hizo kuchukua hatua mahsusi KUTAIFISHA sekta muhimu za uchumi katika Nchi zao kwa manufaa ya umma.
Argentina imetaifisha kampuni ya uchimbaji mafuta,YPF ambayo ni kampuni ya uchimbaji wa mafuta na imetaifishwa mnamo April 16 mwaka huu.
Kampuni ya YPF ilikuwa inamilikiwa kwa pamoja na Nchi ya Spain.
Jana, May, 1 ,2012, nayo Nchi ya Bolivia imetaifisha kampuni ya kufua umeme, TDE, ambayo vile vile ni ya kutoka Nchi ya Spain.
Hili ni fundisho kubwa sana kwa Nchi zetu hizi, Kama Tanzania, ambazo ziko katika michakato ya "kuuza" njia kuu za uchumi kwa " kubinafsisha" viwanda na makampuni ya umma.
Wengine wetu tulikuwepo miaka ya 60's wakati hatua hii ikifanyika, KUTAIFISHA njia kuu za uchumi.
Leo tunashuhudia zoezi hili likijirudia kwa kuanzia Latin America.
Kuishi kwingi, kuona mengi, and what goes around, comes around!!
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere must be turning in his grave today.