Andrew Nyerere
JF-Expert Member
- Nov 10, 2008
- 3,007
- 2,462
Gazeti la leo,14 july 2009,linaripoti kwamba,Wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri,vijiji na Jiji la Tanga wanataka JKT irejeshwe kama ilivyokuwa zamani,yaani,nguvu kazi,Serikali iwakamate vijana Mijini,kushoto na kulia na kuwapeleka JKT,ili wakafanye kazi za ujenzi wa Taifa. Na hili ni jambo ambalo walikuwa wanalijadili na TAYODEA,Taasisi ya vijana Tanga,kwamba vijana wachukuliwe kutoka vijiweni wapelekwe JKT.
Wanasema wanataka Wabunge waishauri Serikali. Mimi nadhani ni jambo ambalo linaweza kufikiriwa,kuwa na militia,kuwapeleka vijana JKT, kwa sababu Mgambo na JKT walisaidia sana katika vita dhidi ya Iddi Amin. Na pia Waamerika wanawaruhusu wananchi wao kuwa na silaha kama jambo ambalo linaweza kuifanya nchi yao iwe salama kutokana na mashambulizi kutoka nje.
Kwa ajili ya Usalama wa nchi yetu,hili ni jambo ambalo tunapaswa kulifikiria. Siyo kuwaweka gerezani wazururaji ,jambo ambalo lilifanywa miaka kadhaa iliyopita na kuwafanya NCCR Mageuzi,akina Mabere Marando kulalamika sana,lakini kujaribu kuliondoa tatizo la ajira.
Wanasema wanataka Wabunge waishauri Serikali. Mimi nadhani ni jambo ambalo linaweza kufikiriwa,kuwa na militia,kuwapeleka vijana JKT, kwa sababu Mgambo na JKT walisaidia sana katika vita dhidi ya Iddi Amin. Na pia Waamerika wanawaruhusu wananchi wao kuwa na silaha kama jambo ambalo linaweza kuifanya nchi yao iwe salama kutokana na mashambulizi kutoka nje.
Kwa ajili ya Usalama wa nchi yetu,hili ni jambo ambalo tunapaswa kulifikiria. Siyo kuwaweka gerezani wazururaji ,jambo ambalo lilifanywa miaka kadhaa iliyopita na kuwafanya NCCR Mageuzi,akina Mabere Marando kulalamika sana,lakini kujaribu kuliondoa tatizo la ajira.