Ta Kamugisha
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 3,550
- 2,199
Nimetafakari sana mwenendo wa nchi yangu na kugundua kuwa mwenye tatizo si rais, yaani jakaya Mrisho Kikwete.
Nimebaini kuwa huyu jamaa anaipenda sana nchi yake na watu wake tena kwa dhati, ila tatizo linakuja kwa viongozi au wasaidizi wake aliowachagua, chukulia mfano rahisi hawa mawaziri wake, wanashindwa hata kutoa mahamuzi ya maana mpaka rais aingilie kati! vingozi wa wizara ya afya wanasubiri nini kujiuzuru au mpaka JK aseme ndo wajiuzuru?
Kwanini kila mtu anakuwa msemaji wa chama? Mara Lowasa kasema hivi, mara Kinana, mara Sumaye, mara Pinda, mara Makinda, mara Sitta, mara Nyalandu, mara Nape, mara Mukama!
Hapa tatizo ni urais wa 2015. Hata kama anakosea ndo rais wetu mpaka baada ya miaka 4 iliyobaki, JK atafanya mangapi kama wasaidizi wake wanawaza urais badala ya kumsaidia kutatua kelo za walalahoi? kila msaidizi wake amekuwa mchumia tumbo! kuanzia sasa JK nakuunga mkono, piga wote chini hawa mawaziri ambao hawakusaidii weka wapya bado una muda wa kutosha kurudisha mvuto wako na wachama.
Tengeneza serikali ya wanaokutii na ambao wako tayari kukuunga mkono katika kuinua uchumi wa wananchi. Anza na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wengi wapo tu hawakusaidii kitu zaidi ya kujimilikisha maaridhi ya wananchi na kula fedha za pembejeo. Angalia maliasili kwa jicho la kulia wanakuzunguka na kuuza wanyama, si ajabu hata vifaru uliowaleta wameshawauza.
Mzee kuwa mkali usiwachekee wanakudharu miaka 4 iliyobaki inakutosha kutimiza ahadi zako. Kuanzia sasa natangaza rasmi kuunga mkono mpaka utakapo staafu ila kumbuka kufanya maamuzi magumu.
Pinda hakusaidii ameshachoka anakuongezea mzigo nae piga chini akalime tu weka mtu wa kukusaidia katka nafasi hii.
nafasi ya pekee umepata ya hawa jamaa kukugomea kuhusu
mswada wa sheria, vunja baraza la mawaziri alaka utengeneze jina lako limechafuka ndo nafasi ya pekee mkulu.
Haya ni mawazo yangu kwa rais wangu JK, tafadhali nikosoe kwa ustaarabu nilipokosea.
Naomba kuwasilisha.
Nimebaini kuwa huyu jamaa anaipenda sana nchi yake na watu wake tena kwa dhati, ila tatizo linakuja kwa viongozi au wasaidizi wake aliowachagua, chukulia mfano rahisi hawa mawaziri wake, wanashindwa hata kutoa mahamuzi ya maana mpaka rais aingilie kati! vingozi wa wizara ya afya wanasubiri nini kujiuzuru au mpaka JK aseme ndo wajiuzuru?
Kwanini kila mtu anakuwa msemaji wa chama? Mara Lowasa kasema hivi, mara Kinana, mara Sumaye, mara Pinda, mara Makinda, mara Sitta, mara Nyalandu, mara Nape, mara Mukama!
Hapa tatizo ni urais wa 2015. Hata kama anakosea ndo rais wetu mpaka baada ya miaka 4 iliyobaki, JK atafanya mangapi kama wasaidizi wake wanawaza urais badala ya kumsaidia kutatua kelo za walalahoi? kila msaidizi wake amekuwa mchumia tumbo! kuanzia sasa JK nakuunga mkono, piga wote chini hawa mawaziri ambao hawakusaidii weka wapya bado una muda wa kutosha kurudisha mvuto wako na wachama.
Tengeneza serikali ya wanaokutii na ambao wako tayari kukuunga mkono katika kuinua uchumi wa wananchi. Anza na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wengi wapo tu hawakusaidii kitu zaidi ya kujimilikisha maaridhi ya wananchi na kula fedha za pembejeo. Angalia maliasili kwa jicho la kulia wanakuzunguka na kuuza wanyama, si ajabu hata vifaru uliowaleta wameshawauza.
Mzee kuwa mkali usiwachekee wanakudharu miaka 4 iliyobaki inakutosha kutimiza ahadi zako. Kuanzia sasa natangaza rasmi kuunga mkono mpaka utakapo staafu ila kumbuka kufanya maamuzi magumu.
Pinda hakusaidii ameshachoka anakuongezea mzigo nae piga chini akalime tu weka mtu wa kukusaidia katka nafasi hii.
nafasi ya pekee umepata ya hawa jamaa kukugomea kuhusu
mswada wa sheria, vunja baraza la mawaziri alaka utengeneze jina lako limechafuka ndo nafasi ya pekee mkulu.
Haya ni mawazo yangu kwa rais wangu JK, tafadhali nikosoe kwa ustaarabu nilipokosea.
Naomba kuwasilisha.