Natangaza rasmi kumuunga mkono JK

Natangaza rasmi kumuunga mkono JK

Ta Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 17, 2011
Posts
3,550
Reaction score
2,199
Nimetafakari sana mwenendo wa nchi yangu na kugundua kuwa mwenye tatizo si rais, yaani jakaya Mrisho Kikwete.

Nimebaini kuwa huyu jamaa anaipenda sana nchi yake na watu wake tena kwa dhati, ila tatizo linakuja kwa viongozi au wasaidizi wake aliowachagua, chukulia mfano rahisi hawa mawaziri wake, wanashindwa hata kutoa mahamuzi ya maana mpaka rais aingilie kati! vingozi wa wizara ya afya wanasubiri nini kujiuzuru au mpaka JK aseme ndo wajiuzuru?

Kwanini kila mtu anakuwa msemaji wa chama? Mara Lowasa kasema hivi, mara Kinana, mara Sumaye, mara Pinda, mara Makinda, mara Sitta, mara Nyalandu, mara Nape, mara Mukama!

Hapa tatizo ni urais wa 2015. Hata kama anakosea ndo rais wetu mpaka baada ya miaka 4 iliyobaki, JK atafanya mangapi kama wasaidizi wake wanawaza urais badala ya kumsaidia kutatua kelo za walalahoi? kila msaidizi wake amekuwa mchumia tumbo! kuanzia sasa JK nakuunga mkono, piga wote chini hawa mawaziri ambao hawakusaidii weka wapya bado una muda wa kutosha kurudisha mvuto wako na wachama.

Tengeneza serikali ya wanaokutii na ambao wako tayari kukuunga mkono katika kuinua uchumi wa wananchi. Anza na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wengi wapo tu hawakusaidii kitu zaidi ya kujimilikisha maaridhi ya wananchi na kula fedha za pembejeo. Angalia maliasili kwa jicho la kulia wanakuzunguka na kuuza wanyama, si ajabu hata vifaru uliowaleta wameshawauza.

Mzee kuwa mkali usiwachekee wanakudharu miaka 4 iliyobaki inakutosha kutimiza ahadi zako. Kuanzia sasa natangaza rasmi kuunga mkono mpaka utakapo staafu ila kumbuka kufanya maamuzi magumu.

Pinda hakusaidii ameshachoka anakuongezea mzigo nae piga chini akalime tu weka mtu wa kukusaidia katka nafasi hii.
nafasi ya pekee umepata ya hawa jamaa kukugomea kuhusu
mswada wa sheria, vunja baraza la mawaziri alaka utengeneze jina lako limechafuka ndo nafasi ya pekee mkulu.
Haya ni mawazo yangu kwa rais wangu JK, tafadhali nikosoe kwa ustaarabu nilipokosea.

Naomba kuwasilisha.
 
Ta Kamugisha, hongera kwa kutangaza kumuunga mkono JK. Unapounga mkono sio vibaya akayataja na hayo mazuri yake yeye kama yeye na hao unaodai wanamwangusha ili nasi tujiunge na wewe kwenye huo uugwaji mkono wako.

Pia unapomshauri kuwa fulani na fulani hawafai, fukuzia mbali, pia nashauri hebu angalau u suggest akishawafukuza hao wasiofaa, awalete kina nani wanaofaa.

Kuna hoja zilijengwa kuwa CCM ni yote imeoza kwa rushwa from top to buttom, sasa kama unawajua wasafi miongoni mwao wataje ili nasi tuwafahamu.

Mimi ni miongoni mwa wapiga debe wa kujitolea wa EL kuwa ndiye pekee ndani ya CCM akipitishwa, ataweza kutupatia Tanzania tunayoitaka!. Hiyo ni suggestion yangu na wewe weka ya kwako!.
 
Baba huwa anapimwa na rafiki zake kwa jinsi familia yake inavyo onekana.
Sasa kama watendaji aliowateua yeye mwenyewe wanamharibia na hawezi kuwawajibisha, then na yeye ni wale wale.
kama aliingia madarakani kwa wizi wa hela na kura za watanzania, na anashindwa kuwawajibisha wezi wa EPA, RICHMOND, KAGODA etc,etc, unawezaje kusema huyu Mkuu anaipenda nchi yake??
Jk kama JK nadhani sio tatizo. Ila JK kama Raisi ni janga la kidunia. Angekuwa China, KASHANYONGWA LONG TIME
 
Hivi Ta Kamugisha nikuulize swali ukiwa na watoto watatu hata wanne lakini ukiwatuma wanakukatalia au wanaenda lakini hawafiki ulikowatuma,unawapeleka shule wanaishia kucheza njiani walimu wanakulala mikia,majirani na wanakulalamikia wewe hapo unadhani ninani anastahili lawama??Ninani mzembe wewe kama Baba????Jibu unalo hivyo lawama hawezi kuzikwepa!!Hata ungemuunga mguu =0!
 
Pasco, si kwamba samaki mmoja akioza wote wameoza! mfano uyo lowasa wako c alishawajibika? kama jk anaona anafaa amrudishe kuwa pm, si ameshatubu na kusamehewa? kama anafaa apewe, mimi sichagui nataka mtendaji tu, kuna magufuri, kuna mwanri, akishindwa kabisa basi amteue mkapa kuwa mbunge then ampe u-pm natumai atamsaidia na si pinda anayekosa msimamo. au afunge macho achomeke wapinzani wamsaidie mbona wapo wengi wa kurudisha mvuto wake na kutekeleza ahadi zake? aondoe wote wanaoutafuta urais abaki na wale wasioutaka apige kazi ya ukweli na kuacha kumbukumbu
 
Hivi Ta Kamugisha nikuulize swali ukiwa na watoto watatu hata wanne lakini ukiwatuma wanakukatalia au wanaenda lakini hawafiki ulikowatuma,unawapeleka shule wanaishia kucheza njiani walimu wanakulala mikia,majirani na wanakulalamikia wewe hapo unadhani ninani anastahili lawama??Ninani mzembe wewe kama Baba????Jibu unalo hivyo lawama hawezi kuzikwepa!!Hata ungemuunga mguu =0!

ni kuwapeleka jela ya watoto kwanza, wasipojifunza nawaachia rahana kama babayao.
 
nakubaliana na wewe kuhusu JK tatizo linakuja yeye ndo aliwateua woote hao anashindwaje kuwadhibiti?
au ndo alisaidiwa na lowasa.
 
Ta Kamugisha kileki waimukota si. Mie namshauri jk afanye dissolution of parliament. Hata hao wabunge wanaotaka kukwamisha muswada wa marekebisho ya katiba wakagomee maskani kwao
 
Inabidi akiwapiga chini pia wapelekwe mahakamani haraka

ndo maana nkasema anatakiwa kuwa na maamuzi magumu, hasimuonee mtu aibu, wote wasio na maadili na orodha ndefu ya nape ya mafisadi atumie iyo iyo, ntamuunga mkono mwanzo mwisho
 
"Show me your friends and I will tell you what you are!" Unao uhakika kwamba hao "wasaidizi", kwa namna moja au nyingine, si tegemeo na nguzo muhimu kwa kuwepo na kudumu kwa JK madarakani? Unadhani amekurupuka tu kuwateua kwenye nyadhfa walizo nazo?
 
Ta Kamugisha kileki waimukota si. Mie namshauri jk afanye dissolution of parliament. Hata hao wabunge wanaotaka kukwamisha muswada wa marekebisho ya katiba wakagomee maskani kwao

Ta muganyizi, maimukage, lakn jamaa anaonewa kila kitu, avunje baraza lote la mawaziri, atoe wote wajinga wajinga, wanaosinzia tu kwenye vikao, wanaoleta mipasho ya taarabu kwenye kazi kama dr nkya, hawa gasia, sophia , tyson, sitta, ngeleja, mkulo, mponda, naodha nk, hawa wote ndo kaburi lake, wanamwangu c mchezo! wanajibu maswali kirahic rahic kama c mawaziri mpaka naboreka.
 
huyu jamaa ananichanganya tu.
alichoshindwa kufanya rais na tunachokilalamikia ndio hicho unachomshauri kufanya.
alisema hawajui richmond na hana haja wala wao hawana haja kumjua,hapo kuna baba kweli?
 
nakubaliana na wewe kuhusu JK tatizo linakuja yeye ndo aliwateua woote hao anashindwaje kuwadhibiti?
au ndo alisaidiwa na lowasa.

Jamaa aliletewa na wana mtandao na c lowassa pekeyake! na hakujua kama anaingizwa mjini! ndo tunamwambia ashituke kabla hakujakucha
 
huyu jamaa ananichanganya tu.
alichoshindwa kufanya rais na tunachokilalamikia ndio hicho unachomshauri kufanya.
alisema hawajui richmond na hana haja wala wao hawana haja kumjua,hapo kuna baba kweli?

Wewe kama baba hauwezi kukiri udhaifu wako mbele ya watoto wako! hata mkubwa akijamba anasingiziwa mtoto, ndo mila zetu kaka.
 
tehteh....kikwete amlaani chenge, lowassa, rost ham...sitta..hiyo laana haiendagi

Mbona tayari ameshawalaani, kitendo cha kusema gutter politics au siasa uchwara, au gamba limeishia kiunoni au kwenda makanisani na kwa tb joshua zote ni rahana za jk, zingekuwa si rahana wasingeangaika ivyo kaka.
 
kumuunga mkono tu haitoshi'unapaswa kumshauli aache ushikaji kwenye uteuzi anaofanya pia avae sura ya Uongozi iliaweze kuchukua hatua nakuwawajibisha wateule wake...yeye nirais wa nchi anashindwaje kuhutubia wananchi na kuelezea msimamo wake kuhusu posho mpya za wabunge? mbona aliweza kuwaambia wafanyakazi 315000 hailipiki? angalia mgomo wa madaktari kuna ugumu gani wayeye kutoa kauli za matumaini kwa madaktari na kuwaamulu viongozi wawizara wajiuzuru? usidanganywe na tabasamu watanzania wenzako wanateseka na mfumuko wa bei, Tanzania yaleo hata chai na mkate waslesi nianasa....kweli wanasiasa niwatu wabinafsi sana wanapaswa kuwa nao makini sana...binafsi siamini lakini naomba wote tujiulize hivi TANZANIA NI NCHI MASIKINI KWELI........? mungu Ibariki tanzania.
 
Uongozi ni maono!!Kwa Kuitwa Rais kwa nchi zakiafrica Unaweza kufanya chochote kile na hakuna wakuzungumza kwani hakuna democrasia sasa yeye anashindwa kuwafunga watu wakati kitendo cha yeye kutamka neno lake moja litafanya kazi!!wewe kama Rais unatoa maagizo kwa Waziri Mkuu na kumpa muda kwa maagizo unataka agizo liwe limetekelezwa within,unampa time frame.
 
Back
Top Bottom