Natamani kumsamehe baba mzazi

Natamani kumsamehe baba mzazi

Huna cha kupoteza na ushakuwa mtu mzima na una maisha yako. Regardless ya kile alichokuambia mama na ulichosikia popote msamehe na move on with your life. Afterall hakusaidii wala hakupunguzii chochote ni kiasi cha wewe kuondoa hasira moyoni mwako kaa kwako endelea na maisha yako na iwapo yeye mwenyewe atajiona baadae huko kuwa ana makosa anaweza kukutafuta. Ila moyoni mwako ondoa hizo hasira na ishi kama kipindi ambacho ulikuwa hujamjua wala kumuona.
Kwani miaka yote ulipungukiwa na nini wakati hakuwepo katika maisha yako. endelea na hayo hayo na muone kama hana nyongeza yoyote katika maisha yako.



Unajua mambo ya mahusiano yanashida nyingi na matatizo makubwa.Katika mahusiano wanawake huwa ni wepesi sana wa kusimulia matatizo ya waume zao kuliko wanaume wanavyoweza kuvumilia na kulilia moyoni.sasa Huyu jamaa kusikia stori ya upande mmoja kishamuhukumu baba yake.
jambo moja nalokushauri mpende baba yako na umuheshimu hata kama kuna matatizo yalitokea kwa upande wake,wewe huyajui.lakini ukitaka kufukunyua utakuja kukuta kuna kitu kibaya kabisa mama yako alichomfanyia baba yako, kiasi kwamba hakutaka hata kuwa karibu na nyie, kwani alijua kupitia nyie mama yenu angeweza kuwa na access nayo.
Nachokushauri achana na kutaka kujua nni kilitokea kati yao utakua dissappointed big time.Daima maisha ya wapenzi yana unafiki mkubwa ambao hutakuja kujua yupi ni mkweli na yupi ni muongo.

nakushauri endelea kumtembelea baba yako, ikiwezekana mpeleke na mdogo wako.Baada ya muda kuna siku mzee atakuja kukuambia kitu.kwa sasa hawezi kwani anajua kuna mambo mabaya juu yake ambayo mama yenu amewajaza kiasi kwamba mnaweza mdhuru.Ukimtendea wema kuna siku atakuja jua kwamba kwa kutokuishi nanyi aliwadhulumu,haki ya malezi mpaka mmeathirika kisaikolojia.Atakuja omba radhi na mtaanza maisha mapya ya amani na upendo.
Ijapokua hili la kumtembelea baba yako kuna siku litakuja kuleta mgogoro kati yako na mama yako pengine na huyo baba wa kambo kwani hawatapenda muwe na ukaribu uliomkubwa kuliko kwao.Lakini mwisho wa siku huyo ni baba yako,hata upinduke ,ugalegale vipi.Masikio hayazidi kichwa.Utamuhitaji tu,kwa namna moja au nyingine siku moja.
 
mleta mada kwanza niseme pole..!

pili nikukumbushe kuwa maisha ya mahusiano yanasafar ndefu sana had kufikia kifo,

ushaur wangu ni kwamba msamehe bila hata kwenda kumuuliza ilikuwaje, naamini mama yako bila kuamua kumsamehe huyo baba asingeweza kufanya yote aliyofanya juu yenu....! alisamehe kwanza ndipo Mungu akamletea mwenza ambaye wamesaidiana kuwalea nyie...! lak kwanza ALISAMEHE

Ili wewe usifungie baraka zako MSAMEHE KUTOKA MOYON, na wala usimuulize kabisa uliyoyasikia na kujionea yanatosha SONGA MBELE..! blieve me Mungu huikumbuka sana mioyo iliyoumizwa na KUSAMEHE
 
pole sana mkuu!umeshakuwa mtu mzima mshukuru mungu maana wapo waliopoteza uhai au kukosa elimu kwa kutelekezwa na wazazi.kwanza msamehe huyo baba yako .ipo siku ataona umuhimu wako hapa duniani!atakuhitaji na atakutafuta tu!
 
mimi nahisi ningemtafuta kumfanyia kitu roho yangu iridhike.........revenge its good for health

dunia wa mama ndio wenye mioyo mizuri, yenye huruma na uwezo wa kusamehe bila hata ya kuombwa msamaha, sasa vip best tena hivyo una fanya nini
 
Ikiwezekana mface ila am not sure kama atakuelezea what happened back then, ila kama nikumsamehe we msamehe kama mzazi iyo pia itakupa peace ww mwenyewe!
 
Mimi ni Kijana wa miaka 30. Nimezaliwa katika familia masikini, mkoani Kilimanjaro. Nimeanza kujitambua nikiwa na umri wa miaka mitano nikiwa mikononi mwa bibi wa mama yangu. Sikujua ni kwanini niliishi na bibi wa Mama lakini Baada ya muda, Mama alikuja kunichukua na Nikaenda kuishi nae wilaya nyingine mkoa wa Kilimanjaro ambapo nilianzishwa masomo ya elimu ya chekechea na msingi. Mama yangu ana watoto wane, mimi nikiwa wa pili.

Mtoto wa mwisho ni mtoto wa baba yetu mlezi, ambae nilikuja kubaini kuwa Yule sio baba yangu mzazi, ila ni mlezi kufuatia vijimaneno vya mjomba na Mama yangu mdogo aishie kijijini. ( Wewe mu-uru, . Wewe mkibosho, nk. Wakati Baba tuliekua nae ni Mzigua) Nilikuja kubaini hilo nikiwa kidato cha nne.

Nikaanza kupata Kiu ya kumjua baba yangu mzazi.
Baada ya kumaliza kidato cha sita, hamu ya kumjua baba yangu mzazi ilizidi. Nikamfuata mama yangu mdogo (R.I.P. mama mdogo), ambae alikua akiishi moshi maeneo ya Pasua.

Sikutaka kumbughudhi Mama yangu kwasababu niliona tabu zote alizopitia katika kutulea na kutusomesha. Nilijua wazi Mama mdogo atakua anamjua vizuri dada yake (Mama yangu), na anaweza kuwa na clues muhimu kumpata baba yangu. Alikataa sana, ila mama ni mama.

Nilijua niseme nini na nimshawishi vipi na hatimae alinipa details za baba yangu japo hakujua alikoishi. Kutokana na details nilizopata, ikiwa ni pamoja na sehemu alizofanya kazi, nilifanikiwa kumpata mtu ambae alinipeleka moja kwa moja mpaka nyumbani kwake.

Nilimuona na nikajitambulisha. Niliposema tu nilipotokea alinijua mimi ni nani. Akanitaja jina. By then I was around 16. Nilikaa kidogo na akanipa namba za ndugu zangu kibao niwatafute. Niliwatafuta baadhi na nikajenga nao ukaribu. Nilidhani baba, pamoja na kutokua na uwezo (Amestaafu), angetambua uwepo wangu.

Ila zaidi ya mimi kwenda kumsalimia na kuwa kama mgeni yeyote tu wa kawaida anaekuja na kuondoka, hapakua na la ziada. Hakutaka kujua naishije, niliishije, nini malengo yangu, … no dad to son talk at all. Mategemeo yangu ya kumuona na kuongea na Baba yalipotea kabisa. Nilimtembelea kama mara tatu na baada ya hapo nikakaa kimya kuona kama atanikumbuka japo kwa ku beep.

Baada ya muda, niliamua kumchunguza mama taratibu kujua kulikoni. Nilianza kwa kumuambia kuwa namjua Baba yangu mzee …(Nikamtaja jina). Alishtuka kidogo hatimae akaniambia kua ni kweli, huyo ndie baba yako. Baada ya siku kadhaa, Mama aniliita faragha.

Akaanza kunisimulia mambo ambayo baba alimtendea, iliniuma sana. Ilifika kipindi mama anaomba ridhaa kwa barua kwa baba kuwa tupelekwe jando (Ikumbukwe kuwa walishaachana miaka mingi nyuma), baba anajibu kwa barua kuwa “Hao watoto ni zawadi yako nimekupa. Fanya chochote unachotaka”.

Sijui nini chanzo cha ugomvi wao, sijui nini kilipelekea wao kuachana, sijui ni kwa nini tuliishi maisha ya shida sana na mama aliteseka sana peke yake kutulea na wakati baba alikua na uwezo, ila kwa vyovyote vile, baba alitakiwa kuonyesha kuwa altujali wanae.

Ameniona mimi tu, Mdogo wangu alienifata nae ni mwanae, ila wala kumuulizia hamuulizii. Niliwahi kumuuliza kuwa anamtambua mdogo wangu kuwa ni mwanae akajibu kuwa Anamtambua.

Mada ambayo wana Jamiiforums nataka wani shauri ni uamuzi ninaotaka kuuchukua sasa.
Nimemchukia baba yangu ever since nimemuona. Ila inawezekana kuna mengi mengine ambayo siyajui kati yake na mama yangu. Nafikiria kwenda kuongea nae aniambie mambo mengi sana kati yao na kwanini ametususa kiasi hicho.

Japo sidhani kuwa ni uamuzi sahihi kwani niko na baba mlezi ambae kwangu mimi amebeba thamani yote ya neno Baba. Natamani nimsamehe ila sina pa kuanzia. Namuona kama womanizer kwasababu ana watoto sita nje ya ndoa yake, mimi na mdogo wangu tukiwa wamoja wapo.

(Hakuwa amemwoa mama, inavyosemekana alimdanganya, akamzalisha kumbe ameoa). Je, ni uamuzi sahihi kwa mtoto kum face baba yake na kuhoji ukweli wa yaliyojiri kati ya baba na mama?

Kwanini he was irresponsible kwetu tukiwa wadogo? Lengo ni kupata sababu yakumsamehe ili nafsi iwe na Amani kila nikimkumbuka, Badala ya chuki na hasira.

Niwieni radhi kwa uzi mrefu na mchanganyiko wa lugha.

Haya mambo nendeni mkasolve kwenye ukoo wenu. Hapa JF, kuna watu wengi maisha yao yanafanana na yako. Sasa unategemea kupata ushauri gani. Nendeni mkayamalize kwenye ukoo wenu.

 
Mimi ni Kijana wa miaka 30. Nimezaliwa katika familia masikini, mkoani Kilimanjaro. Nimeanza kujitambua nikiwa na umri wa miaka mitano nikiwa mikononi mwa bibi wa mama yangu. Sikujua ni kwanini niliishi na bibi wa Mama lakini Baada ya muda, Mama alikuja kunichukua na Nikaenda kuishi nae wilaya nyingine mkoa wa Kilimanjaro ambapo nilianzishwa masomo ya elimu ya chekechea na msingi. Mama yangu ana watoto wane, mimi nikiwa wa pili.

Mtoto wa mwisho ni mtoto wa baba yetu mlezi, ambae nilikuja kubaini kuwa Yule sio baba yangu mzazi, ila ni mlezi kufuatia vijimaneno vya mjomba na Mama yangu mdogo aishie kijijini. ( Wewe mu-uru, . Wewe mkibosho, nk. Wakati Baba tuliekua nae ni Mzigua) Nilikuja kubaini hilo nikiwa kidato cha nne.

Nikaanza kupata Kiu ya kumjua baba yangu mzazi.
Baada ya kumaliza kidato cha sita, hamu ya kumjua baba yangu mzazi ilizidi. Nikamfuata mama yangu mdogo (R.I.P. mama mdogo), ambae alikua akiishi moshi maeneo ya Pasua.

Sikutaka kumbughudhi Mama yangu kwasababu niliona tabu zote alizopitia katika kutulea na kutusomesha. Nilijua wazi Mama mdogo atakua anamjua vizuri dada yake (Mama yangu), na anaweza kuwa na clues muhimu kumpata baba yangu. Alikataa sana, ila mama ni mama.

Nilijua niseme nini na nimshawishi vipi na hatimae alinipa details za baba yangu japo hakujua alikoishi. Kutokana na details nilizopata, ikiwa ni pamoja na sehemu alizofanya kazi, nilifanikiwa kumpata mtu ambae alinipeleka moja kwa moja mpaka nyumbani kwake.

Nilimuona na nikajitambulisha. Niliposema tu nilipotokea alinijua mimi ni nani. Akanitaja jina. By then I was around 16. Nilikaa kidogo na akanipa namba za ndugu zangu kibao niwatafute. Niliwatafuta baadhi na nikajenga nao ukaribu. Nilidhani baba, pamoja na kutokua na uwezo (Amestaafu), angetambua uwepo wangu.

Ila zaidi ya mimi kwenda kumsalimia na kuwa kama mgeni yeyote tu wa kawaida anaekuja na kuondoka, hapakua na la ziada. Hakutaka kujua naishije, niliishije, nini malengo yangu, … no dad to son talk at all. Mategemeo yangu ya kumuona na kuongea na Baba yalipotea kabisa. Nilimtembelea kama mara tatu na baada ya hapo nikakaa kimya kuona kama atanikumbuka japo kwa ku beep.

Baada ya muda, niliamua kumchunguza mama taratibu kujua kulikoni. Nilianza kwa kumuambia kuwa namjua Baba yangu mzee …(Nikamtaja jina). Alishtuka kidogo hatimae akaniambia kua ni kweli, huyo ndie baba yako. Baada ya siku kadhaa, Mama aniliita faragha.

Akaanza kunisimulia mambo ambayo baba alimtendea, iliniuma sana. Ilifika kipindi mama anaomba ridhaa kwa barua kwa baba kuwa tupelekwe jando (Ikumbukwe kuwa walishaachana miaka mingi nyuma), baba anajibu kwa barua kuwa “Hao watoto ni zawadi yako nimekupa. Fanya chochote unachotaka”.

Sijui nini chanzo cha ugomvi wao, sijui nini kilipelekea wao kuachana, sijui ni kwa nini tuliishi maisha ya shida sana na mama aliteseka sana peke yake kutulea na wakati baba alikua na uwezo, ila kwa vyovyote vile, baba alitakiwa kuonyesha kuwa altujali wanae.

Ameniona mimi tu, Mdogo wangu alienifata nae ni mwanae, ila wala kumuulizia hamuulizii. Niliwahi kumuuliza kuwa anamtambua mdogo wangu kuwa ni mwanae akajibu kuwa Anamtambua.

Mada ambayo wana Jamiiforums nataka wani shauri ni uamuzi ninaotaka kuuchukua sasa.
Nimemchukia baba yangu ever since nimemuona. Ila inawezekana kuna mengi mengine ambayo siyajui kati yake na mama yangu. Nafikiria kwenda kuongea nae aniambie mambo mengi sana kati yao na kwanini ametususa kiasi hicho.

Japo sidhani kuwa ni uamuzi sahihi kwani niko na baba mlezi ambae kwangu mimi amebeba thamani yote ya neno Baba. Natamani nimsamehe ila sina pa kuanzia. Namuona kama womanizer kwasababu ana watoto sita nje ya ndoa yake, mimi na mdogo wangu tukiwa wamoja wapo.

(Hakuwa amemwoa mama, inavyosemekana alimdanganya, akamzalisha kumbe ameoa). Je, ni uamuzi sahihi kwa mtoto kum face baba yake na kuhoji ukweli wa yaliyojiri kati ya baba na mama?

Kwanini he was irresponsible kwetu tukiwa wadogo? Lengo ni kupata sababu yakumsamehe ili nafsi iwe na Amani kila nikimkumbuka, Badala ya chuki na hasira.

Niwieni radhi kwa uzi mrefu na mchanganyiko wa lugha.

Wewe ni mwanamke au mwanaume? Kama ni mwanaume pambana tuu hakuna cha ziada kwani wee unamtaka akusaidie nini kama hana mpango na wewe. Achana nae
 
* Holding on to the past is like holding onto own breath, you will suffocate.(NYAKUBI)

* We must develop and maintain the capacity to 4give;he who is devoid of the capacity to 4give is devoid of the capacity to LOVE. There are some BEST in the WORST of us and some WORST in the GOOD of us. When we discover this we are less PRONE to hate our enemies. (MARTIN LUTHER KING Jr.)

* I have decided to stick with LOVE hate is too great a burden to Bear. (NYAKUBI)

Mkuu pole xaaana even myself i had a story kma yako ( though not similar exactly kma yako).. i real suffocated bt tym ilifika whn I had to learn how to 4give and move on and now i have a peace of mind and i live a peopled life.
 
aise pole sana
haina haja ya kumfuata ili kujua yaliyotokea coz yatazidi kukuumiza bure,yaliyopita achana nayo,msamehe usimuwekee kinyongo,wewe endelea maisha yako na mama yako
 
kwan kumsamehe mtu mpaka uwe nae karibu, unachopaswa kujua n kuwa kuna sbb ilifanya wawe hivo! sababu gan hiyo sasa sio juu yako! msamehe muone alikosea na maybe atajirudi baadae, endelea na maisha yako
 
umefanya vyema kumtafuta na kumfahamu.
je hiyo barua aliyoiandika baba yako kwamba nyinyi ni zawadi ya mama yenu umeiona? kama umeiona unauhakika gani kwamba mwandishi ni baba yako?

kama walisema baadhi ya wachangiaji, ni hatari sana kutaka kujua undani wa ugomvi wa wazazi wako. huo uwanja waachie wenyewe. unaweza upata ukweli ukakusumbua maisha yako yote.

bahati mbaya umekwisha toa hukumu kwamba huyo baba yako anahitaji msamaha wako. na umekwishaamua kwamba humhitaji kwa chochote (hii ni kauli nzito sana, kwani hatujui maisha yanatupeleka wapi).

ushauri wangu kwa vile sasa unamjua baba yako na ndugu zako wengine, shirikiana nao pale inapowezekana. waheshimu wazazi wako pia ukiweza tafuta ndugu wengine wa ukoo wa baba yako.

usiache kumpitia baba yako na kumjulia hali, usisahau kuwapeleka na wadogo zako. jenga maisha yako na ondokana na chuki ulizozijenga kwa baba yako. muonyeshe heshima baba yako japokuwa unajitegemea na yeye hakutegemei.
 
Msamehe ndugu yangu
Biblia inasema ' kisasi ni cha Bwana'
Achilia kabisa na muombe Mungu akusaidie kumsamehe utashangaa Mungu alivyo wa ajabu majibu ni hapahapa duniani.
 
Mimi ni Kijana wa miaka 30. Nimezaliwa katika familia masikini, mkoani Kilimanjaro. Nimeanza kujitambua nikiwa na umri wa miaka mitano nikiwa mikononi mwa bibi wa mama yangu. Sikujua ni kwanini niliishi na bibi wa Mama lakini Baada ya muda, Mama alikuja kunichukua na Nikaenda kuishi nae wilaya nyingine mkoa wa Kilimanjaro ambapo nilianzishwa masomo ya elimu ya chekechea na msingi. Mama yangu ana watoto wane, mimi nikiwa wa pili.

Mtoto wa mwisho ni mtoto wa baba yetu mlezi, ambae nilikuja kubaini kuwa Yule sio baba yangu mzazi, ila ni mlezi kufuatia vijimaneno vya mjomba na Mama yangu mdogo aishie kijijini. ( Wewe mu-uru, . Wewe mkibosho, nk. Wakati Baba tuliekua nae ni Mzigua) Nilikuja kubaini hilo nikiwa kidato cha nne.

Nikaanza kupata Kiu ya kumjua baba yangu mzazi.
Baada ya kumaliza kidato cha sita, hamu ya kumjua baba yangu mzazi ilizidi. Nikamfuata mama yangu mdogo (R.I.P. mama mdogo), ambae alikua akiishi moshi maeneo ya Pasua.

Sikutaka kumbughudhi Mama yangu kwasababu niliona tabu zote alizopitia katika kutulea na kutusomesha. Nilijua wazi Mama mdogo atakua anamjua vizuri dada yake (Mama yangu), na anaweza kuwa na clues muhimu kumpata baba yangu. Alikataa sana, ila mama ni mama.

Nilijua niseme nini na nimshawishi vipi na hatimae alinipa details za baba yangu japo hakujua alikoishi. Kutokana na details nilizopata, ikiwa ni pamoja na sehemu alizofanya kazi, nilifanikiwa kumpata mtu ambae alinipeleka moja kwa moja mpaka nyumbani kwake.

Nilimuona na nikajitambulisha. Niliposema tu nilipotokea alinijua mimi ni nani. Akanitaja jina. By then I was around 16. Nilikaa kidogo na akanipa namba za ndugu zangu kibao niwatafute. Niliwatafuta baadhi na nikajenga nao ukaribu. Nilidhani baba, pamoja na kutokua na uwezo (Amestaafu), angetambua uwepo wangu.

Ila zaidi ya mimi kwenda kumsalimia na kuwa kama mgeni yeyote tu wa kawaida anaekuja na kuondoka, hapakua na la ziada. Hakutaka kujua naishije, niliishije, nini malengo yangu, … no dad to son talk at all. Mategemeo yangu ya kumuona na kuongea na Baba yalipotea kabisa. Nilimtembelea kama mara tatu na baada ya hapo nikakaa kimya kuona kama atanikumbuka japo kwa ku beep.

Baada ya muda, niliamua kumchunguza mama taratibu kujua kulikoni. Nilianza kwa kumuambia kuwa namjua Baba yangu mzee …(Nikamtaja jina). Alishtuka kidogo hatimae akaniambia kua ni kweli, huyo ndie baba yako. Baada ya siku kadhaa, Mama aniliita faragha.

Akaanza kunisimulia mambo ambayo baba alimtendea, iliniuma sana. Ilifika kipindi mama anaomba ridhaa kwa barua kwa baba kuwa tupelekwe jando (Ikumbukwe kuwa walishaachana miaka mingi nyuma), baba anajibu kwa barua kuwa “Hao watoto ni zawadi yako nimekupa. Fanya chochote unachotaka”.

Sijui nini chanzo cha ugomvi wao, sijui nini kilipelekea wao kuachana, sijui ni kwa nini tuliishi maisha ya shida sana na mama aliteseka sana peke yake kutulea na wakati baba alikua na uwezo, ila kwa vyovyote vile, baba alitakiwa kuonyesha kuwa altujali wanae.

Ameniona mimi tu, Mdogo wangu alienifata nae ni mwanae, ila wala kumuulizia hamuulizii. Niliwahi kumuuliza kuwa anamtambua mdogo wangu kuwa ni mwanae akajibu kuwa Anamtambua.

Mada ambayo wana Jamiiforums nataka wani shauri ni uamuzi ninaotaka kuuchukua sasa.
Nimemchukia baba yangu ever since nimemuona. Ila inawezekana kuna mengi mengine ambayo siyajui kati yake na mama yangu. Nafikiria kwenda kuongea nae aniambie mambo mengi sana kati yao na kwanini ametususa kiasi hicho.

Japo sidhani kuwa ni uamuzi sahihi kwani niko na baba mlezi ambae kwangu mimi amebeba thamani yote ya neno Baba. Natamani nimsamehe ila sina pa kuanzia. Namuona kama womanizer kwasababu ana watoto sita nje ya ndoa yake, mimi na mdogo wangu tukiwa wamoja wapo.

(Hakuwa amemwoa mama, inavyosemekana alimdanganya, akamzalisha kumbe ameoa). Je, ni uamuzi sahihi kwa mtoto kum face baba yake na kuhoji ukweli wa yaliyojiri kati ya baba na mama?

Kwanini he was irresponsible kwetu tukiwa wadogo? Lengo ni kupata sababu yakumsamehe ili nafsi iwe na Amani kila nikimkumbuka, Badala ya chuki na hasira.

Niwieni radhi kwa uzi mrefu na mchanganyiko wa lugha.
Daah pole sana,ninachokiamini hukuzaliwa kwa bahati mbaya lipo kusudi kwa Mungu la wewe kuzaliwa,usimchukie daddy ako,omba hekima za Mungu ujue jinsi gani umuingie atambue nafasi yake ya Baba hata kama haishi na mama yaki,naamini umekua,ukiongea maneno yenye hekima na ambayo utaambatanisha na maombi unaweza fanya IMPOSIBLE kuwa POSIBLE,pole sana lakini kumbuka huwezi kulimaliza hili kama unamchukia baba yako,so hatua ya kwanza hapa anza kwa kumpenda baba yako.
 
Kitu ambacho wazazi wanaotelekeza, watoto wao esp wa kiume ni kwamba, hata akue azeeke hata kaa awe na mapenzi tena na huyo mzazi, bora ma binti wameumbiwa moyo mwepesi wa kusamehe na kusahau, vijana wa kiume husamehe but hawasahau.

weee! kakudanganya nani mabinti ni wepesi wa kusamehe na kusahau. Aisee hii habari ya watoto na wazazi waliowaatelekeza sijui imekaaje. Mimi mama yangu hakuwahi kuniambia chochote chema au kibaya juu ya huyu baba. Na mimi sikuwa na hisia zozote mbaya au nzuri. ila aliponitafuta tu nikiwa kwenye 20s sijui hasira zilitoka wapi. nilimchukia sana. mama akanipa hadithi yote lakini bado sikuona sababu nzito ya yeye kukaa miaka yote kimya. yule baba alivyoona simshobokei akawa anampigia mama. mama akaonekana anamhurumia mzazi mwenzie lakini mimi ndo staki hata kumsikia. Lakini baadae baada ya kugundua hasira na chuki zinakula kwangu nikaamua kumuachilia anitoke huku moyoni. nilishamsamehe ila kupanda ndege au basi kumfata kitakuwa ni kitu cha mwisho mimi kukifanya. ila akipiga simu napokea na kumsalimia. nadhani inatosha. huyu Mdoe amsamehe tu babakekama wengine walivyopendekeza ili aishi kwa furaha. huyo mzee kama ana watoto wengi nje ya ndoa ni dalili kwamba ni negligent kwa hiyo habadiliki. imagine unamchukia mtu ambaye hajali kama umekufa au u hai!
 
umefanya vyema kumtafuta na kumfahamu.
je hiyo barua aliyoiandika baba yako kwamba nyinyi ni zawadi ya mama yenu umeiona? kama umeiona unauhakika gani kwamba mwandishi ni baba yako?

kama walisema baadhi ya wachangiaji, ni hatari sana kutaka kujua undani wa ugomvi wa wazazi wako. huo uwanja waachie wenyewe. unaweza upata ukweli ukakusumbua maisha yako yote.

bahati mbaya umekwisha toa hukumu kwamba huyo baba yako anahitaji msamaha wako. na umekwishaamua kwamba humhitaji kwa chochote (hii ni kauli nzito sana, kwani hatujui maisha yanatupeleka wapi).

ushauri wangu kwa vile sasa unamjua baba yako na ndugu zako wengine, shirikiana nao pale inapowezekana. waheshimu wazazi wako pia ukiweza tafuta ndugu wengine wa ukoo wa baba yako.

usiache kumpitia baba yako na kumjulia hali, usisahau kuwapeleka na wadogo zako. jenga maisha yako na ondokana na chuki ulizozijenga kwa baba yako. muonyeshe heshima baba yako japokuwa unajitegemea na yeye hakutegemei.

Naiheshimu JF, nawaheshimu wachangiaji wote. Nitajitahidi kumsamehe bila kujua what happened. Kwa kuanzia, nitamtembelea kesho. Thanks wakuu.
 
Msamehe sio kwa sababu anastahili, au kwa sababu ameomba msamaha; bali msamehe kwa ajili ya afya ya moyo wako, msamehe kwasababu ni kitu sahihi kufanya, msamehe kwa sababu nawe wahitaji kesamehewa makosa yako na Mungu wako, msamehe ili kumfundisha na kufundisha wengine, msamehe kwasababu wewe ni zaidi ya chuki, hasira na visasi, msamehe kwa sababu UNAWEZA.

Nayatunza maneno haya moyoni kwangu. Asante sana
 
Back
Top Bottom