PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Ndugu zangu wapendwa... Habarini za jioni?!
Imekuwa ni kasumba yangu na pengine hata kwa wanaume wenzangu (ambao wako wazi kuzungumzia ukweli kuhusu wao) kwamba, kila akipita mwanamke/msichana mrembo (Asiye ndugu yangu) karibu au hata mbali kidogo, namgeuka na kutamani nimtongoze, na anikubalie. Natamani kumpata kila binti mrembo anayekatiza machoni mwangu. Wakati fulani nimetimiza azma hiyo, na nimefanikiwa na pengine najilazimisha kuacha kumfuatilia kwa lengo la kumtongoza. Mke ninaye na ni mrembo. Nina mpenda naye ananipenda tena sana. Binafsi, siifurahii tabia hii na ningefurahi kama ningepunguza kasi hii hasa ukizingatia hali halisi ya sasa kwani magonjwa ni mengi sana, hasa VVU/UKIMWI. Je, nifanyeje ili niepukane na tabia hii?? Je ni tatizo la kiafya? Tafadhali wanaJF nipeni ushauri unaonifaa kwa ajili ya mustakabali wa maisha yangu... Nashukuru!!
Imekuwa ni kasumba yangu na pengine hata kwa wanaume wenzangu (ambao wako wazi kuzungumzia ukweli kuhusu wao) kwamba, kila akipita mwanamke/msichana mrembo (Asiye ndugu yangu) karibu au hata mbali kidogo, namgeuka na kutamani nimtongoze, na anikubalie. Natamani kumpata kila binti mrembo anayekatiza machoni mwangu. Wakati fulani nimetimiza azma hiyo, na nimefanikiwa na pengine najilazimisha kuacha kumfuatilia kwa lengo la kumtongoza. Mke ninaye na ni mrembo. Nina mpenda naye ananipenda tena sana. Binafsi, siifurahii tabia hii na ningefurahi kama ningepunguza kasi hii hasa ukizingatia hali halisi ya sasa kwani magonjwa ni mengi sana, hasa VVU/UKIMWI. Je, nifanyeje ili niepukane na tabia hii?? Je ni tatizo la kiafya? Tafadhali wanaJF nipeni ushauri unaonifaa kwa ajili ya mustakabali wa maisha yangu... Nashukuru!!