Natamani kuhama siti....

Natamani kuhama siti....

Pole Mkuu, vumilia tu utafika.....ila next time Fanya booking mapema na ukae dirishani ili ku-neutralize hiyo "pungent smell" na fresh air.....
Pungent smell ,doooohh
Umenikumbusha mbaaali kwa kweli ,mambo ya effervescence,pop sound
 
Hujabeba samaki kweli weye? Hebu chekicheki kwenye kapu lako la "mahogo-kivunde"! Hukuweka samaki kweli ndiyo watoao kajiharufu.
 
Ametoka kwenye mechi huyo si bure! Hembu muachie simu yako asome comments zetu aburudike..
 
Umeulzwa upo wap asa mbn unatutarifu mahal ulpo ukiulzw utajbuje sasa asa uchiz ww ictoxhe ushapga selfie za kutosha hilo ni basi je ukpanda ndege
Hizo ndege kwangu nishapanda saaana na ntaendelea kupanda sana ndg yangu... Zishanichosha... Wewe tu ndo labda unaona kitu kipya.
 
Na nikuhakikishie tu..huyu bwana hayuko safarini.. Amekaa sehemu ametulia tuli!
Hahahahahaaaaaaa...... Hatarii sana... Nimecheeeka kweli Mkuu. Yaani nitulie sehemu nianze kufikiria nn cha kuandika, Hapana bhana
 
Ukifika korogwe wakati wa kula, muda wakuondoka pakia basi lingine ujifanye umechanganya magari, mizigo utachukua arusha
 
Habari ya asubuhi wadau.... Niko ndani ya gari la abiria, natoka Dar naelekea Arusha... Hali ya hewa ni nzuri kabisa, ubaridi ukichagizwa na rasharasha za mvua....

Safari yangu imeanzia Ubungo, baada ya kuingia kwenye gari nimepokelewa na bashabasha la tabasamu na jirani wa siti yangu, binti kazuri tu, nikaona nina bahati kumpata jirani ambaye anaonyesha ataifanya Safari yangu niione fupi kabisa.

Maana unaweza fika kwenye siti ukamkuta jirani wa siti yako Kama kalishwa ndimu vile, lakini huyu dada yuko vizuri kabisa.

Sasa licha ya mapokezi matamu na uchangamfu wake, mpaka sasa tuko Chalinze, lakini nimeanza kuchoshwa na harufu mbaya ya huyu dada, yaani hili sio kwapa, kwa umri wangu na uzoefu wa hizi harufu, nina hakika kabisa hii ni harufu ya K -kisheti.. Kwakweli Safari naanza kuiona ndefu mno,.... Nimegeuza geuza macho yangu labda ingewepo nafasi ya siti wazi niombe nihamie,. Lakini nimefeli.

Sasa najiuliza hivi asubuhi hii ametoka kuamka, ameoga, kajipodoa,... Na hali ya hewa wala sio ya joto.. Tatizo laweza kuwa ni nini jamani,.. Yaani natamani kuhama siti kwakweli.
Polepole kwanza, Wewe mwenyewe unasema umepanda tu gari ukapokelewa na BASHABASHA !!, basi tulia.
 
Pole sana kwa adha hiyo mm kuna siku nilikaa na abiria mwenzangu ananuka pua Alafu alikaa dirishani mda wote anafunga dirisha, niliona safari ya kutoka morogoro arusha kama natoka mbeya arusha
 
Na nikuhakikishie tu..huyu bwana hayuko safarini.. Amekaa sehemu ametulia tuli!
Hata Mimi nimepiga picha mazingira ya usafiri bus unapataje mda wa kuandika vitu kama hivi

Jf imekuwa kama fb watu wanatafuta likes na comments
 
Back
Top Bottom