Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Ubaya wa ukada ni unaona udikteta asubuhi ila jioni unaona huohuo udikiteka kuwa umahiri.
Ubaya wake ni pale ndugu yako au maslahi yako yakiguswa na kwa unafiki wa umri unampinga.
Ila akikamatwa fulani,kupigwa n.k ambaye hali chakula nawe,basi mdomo hutoa sifa tu kwa dikteta.
Hii comment safi sana!
Mulemule
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hiyo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Mzima? Uwa nashindwa kukuelewa.
 
Julius Magembe aka Nyani Ngabu anataka ngosha mwenzake ashindwe
849a77f616f7b7d1969de54f79df25fc.jpg
Heheheee Julius Magembe.
Bwa ha ha ha

So huyo ndo nani?
Halafu Faru Kabula wewe ni wa kitambo ee

Screenshot_20180304-004620.png
 
Julius Maghembe nakumbuka wakati tunasoma, ulikuwa mjinga sana darasani, kamasi mpaka mdomoni, kumbe bado una ujinga ule ule. Jana ulimpinga ashindwe leo unamuunga mkono ashinde kwa yale yale matendo uliyopinga awali kama sio ujinga ni nini??
 
Mimi natamani January makamba, nape nnauye na wote walioshadadia sheria ya mitandao wafe tuwazike tumalize shida. By the way nna maono watakufa soon

Na jela siendi na nisharopoka maono ya Lema
Mmoja alinusurika kupigwa risasi,vp bado dua yako inaendelea?
 
Hajanusirika kupigwa risasi bali alinyooshewa bastola. Kunusurika maana yake risasi imefyatuliwa ila ikakukosa
kushindwa kufanyika ndiyo kunusurika kwenyewe . Kwani bastola ni kitu ni kitu cha kawaida kuonyeshewa.
 
Tatizo lako Nyani Ngabu ni kubadilika badilika kwako kama kinyonga.Leo umesema vyema kabisa kwamba huyu jamaa apingwe.Lakini muda si mrefu utakuja kumsifia tena!!
 
Tatizo lako Nyani Ngabu ni kubadilika badilika kwako kama kinyonga.Leo umesema vyema kabisa kwamba huyu jamaa apingwe.Lakini muda si mrefu utakuja kumsifia tena!!
Kubadilika ni kitu cha kawaida kwa binadamu. Wapo waliokuwa wanamsema vibaya Mh. Lowassa kwamba eti ni fisadi; sasa hivi wamebadilika na wanamsifia baada ya kumfahamu vizuri! Hadi wanatamani awe presida wao!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom