Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Kubadilika ni kitu cha kawaida kwa binadamu. Wapo waliokuwa wanamsema vibaya Mh. Lowassa kwamba eti ni fisadi; sasa hivi wamebadilika na wanamsifia baada ya kumfahamu vizuri! Hadi wanatamani awe presida wao!
Wengine na walimuona sio fisadi alivyohama wakaanza kusema fisadi lakini baadae hadi ikulu fisadi akakaribishwa na. Sasa mnachanganya wananchi
 
Tatizo lako Nyani Ngabu ni kubadilika badilika kwako kama kinyonga.Leo umesema vyema kabisa kwamba huyu jamaa apingwe.Lakini muda si mrefu utakuja kumsifia tena!!

Hivi kwa nini ni wagumu wa kuelewa nyie watu?

Mimi sisukumwi wala siongozwi na itikadi za kiCCM au kiCHADEMA.

Sifungamani na upande wowote ile.

Kutokufungamana kwangu huko kunaniweka huru zaidi.

Na ndiyo maana naweza kuzikosoa pande zote kuhusu jambo au mambo fulani kama naona wamekosea na kuwaunga mkono kama nakubaliana nao kwenye mengine.

Nikimkosoa Magufuli leo haina maana kuwa endapo keshokutwa atafanya jambo ninalokubaliana nalo basi nitampinga tu kwa sababu eti nilishampinga huko nyuma.

Hapana. Haiko hivyo na mimi sipo hivyo.

Naweza kuwachana CHADEMA leo lakini kesho wakafanya jambo zuri ninalokubaliana na nikawaunga mkono.

Hizo ni fikra huru. Mambo ya kufungamana na vyama mimi sitaki maana unakuwa kama mtumwa au msukule.

Ukiwa mfia vyama hata chama chako kiboronge vipi wewe kazi yako ni kuunga mkono tu!

Sitaki kabisa mimi huo upumbavu.

Sasa kilicho kigumu kuelewa hapo ni kipi hasa??????????
 
Julius Maghembe nakumbuka wakati tunasoma, ulikuwa mjinga sana darasani, kamasi mpaka mdomoni, kumbe bado una ujinga ule ule. Jana ulimpinga ashindwe leo unamuunga mkono ashinde kwa yale yale matendo uliyopinga awali kama sio ujinga ni nini??

Mimi siyo Julius Maghembe.

Hivyo hujasoma na mimi.

Hujui hata nimesoma wapi na nimemaliza mwaka gani.

Acha kujipendekeza na kujipa ujuvi ambao hauna.
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hiyo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
...
 
Tukinywea atajiona ana nguvu kuliko umma ilihali hana nguvu kuzidi umma.. Nyani
 
Na JPM ameshashindwa kwa kweli. Leo yupo Singida kuzindua kiwanda cha Mount Meru Millers ambacho kina miaka mingi tu ktk uzalishaji wa mafuta ya alizeti.
Anarudia rudia mambo halafu hayana hadhi yake. Level ya waziri au mkuu wa mkoa
 
JF ni Jukwaa linalofuatiliwa sana na viongozi.

Inasemekana baada ya viongozi kutoa matamko yao, huja huku haraka kuangalia maoni ya watanzania.Wanakuja huku kwa kuwa waliopo huku wanajielewa.

Vita dhidi ya JF ni vita dhidi ya wanao jielewaa.

Ila wakumbuke kuwa JF haijawahi kushindwa na haitoshindwaa!

[HASHTAG]#GREATJF[/HASHTAG]
Kwa nini sasa tusiibadilishe JF na tusiifante iwe online political party, na kisajiliwe hivyo?
 
mungu kakuumbua mchana kweupe mnafiki mkubwa wewe uso na kificho @nyaningabu
 
mungu kakuumbua mchana kweupe mnafiki mkubwa wewe usie kua na kificho tumekunyoosha Nyani Ngabu big booty
 
mungu kakuumbua mchana kweupe mnafiki mkubwa wewe usie kua na kificho tumekunyoosha Nyani Ngabu big booty

Oh yeah?

Ngoja nicheke kwa dharau nyingi sana.

Pwa....Bwa....Kwa hahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.

Now I’m done. Continue losing sleep over me. I’m your superior.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom