ras jeff kapita
JF-Expert Member
- Jan 4, 2015
- 19,734
- 28,289
Pambana na fisiemu kwanzaNikiwa kama mkazi wa sayari hii tuliyo rehemishwa na Mwenyezi Mungu tuikalie kwa haki, amani na usawa, nina laani uvamizi wa Russia 🇷🇺 nchini Ukraine 🇺🇦.
Siishii tu kulaani na kukemea uvamizi huo, bali kwa hiari yangu na ridhaa ya familia yangu, tukiwa kama watetezi wa wanyonge, wanaoonewa, familia yangu imenituma niende mstari wa mbele wa mapambano, nikashike bunduki kumuondoa Mrusi ndani ya mipaka ya ardhi ya Ukraine 🇺🇦 aliyoiingia kimabavu.
Ndugu wana JamiiForums, naomba mine muongozo wa namna gani nitaweza kuyafikia malengo ya familia yangu ya kuwa askari wa hilarious wa Ukraine 🇺🇦.
Natanguliza shukrani za dhati.