Nataka kwenda Msanga

Nataka kwenda Msanga

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
19,866
Reaction score
37,532
Habari zenu wakuu, ninataka kwenda Msanga, Kisarawe kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijamii.

Kuna mtu yoyote anaye pafahamu vizuri anipe ABC zake?

Natanguliza shukurani zangu za dhati kwenu.
 
Nenda buguruni sokoni, panda ma-bus ya msanga...
Pia kuna option ya Noah ambayo ipo fast sana ila ni kubahatisha pale gongo la mboto au hukohuko Buguruni sokoni...
Kwa pale sijaona guest house ila maneromango kuna guest ya 5000. Pale na Msanga sio mbali sana...
Huu ni muda wa mavuno kwahyo kama unataka kufanya utafiti inabidi uandae kiasi kidogo cha kuweza kuwalipa ili waache shughuli zao wakupe majibu unayoyahitaji...
 
Nenda buguruni sokoni, panda ma-bus ya msanga...
Pia kuna option ya Noah ambayo ipo fast sana ila ni kubahatisha pale gongo la mboto au hukohuko Buguruni sokoni...
Kwa pale sijaona guest house ila maneromango kuna guest ya 5000. Pale na Msanga sio mbali sana...
Huu ni muda wa mavuno kwahyo kama unataka kufanya utafiti inabidi uandae kiasi kidogo cha kuweza kuwalipa ili waache shughuli zao wakupe majibu unayoyahitaji...

Asante sana kaka kwa majibu mazuri. Haya ndio majibu niliyokuwa nayatarajia. Kutoka Buguruni hadi Msanga ni masaa mangapi? Unasema Msanga hakuna gesti, so itanibidi nilale gesti Mwaneromango? Mambo mengine ambayo nigependa kujua kuhusu msanga ni kuhusu usalama wa raia pamoja na uwepo huduma muhimu za kijamii....
 
Nataka kwenda Msanga, nataka kwenda Msanga oooh nauli sina -Gangwe Mobb "Ngangali Kinoma"

Ukitaka kwenda Msanga lazima uwe ngangali kinoma, la sivyo utarudi na binti wa Kizaramo.

Au unaweza kuhamia usirudi kabisa wakishakupunga madogoli.
 
Nataka kwenda Msanga, nataka kwenda Msanga oooh nauli sina -Gangwe Mobb "Ngangali Kinoma"

Ukitaka kwenda Msanga lazima uwe ngangali kinoma, la sivyo utarudi na binti wa Kizaramo.

Au unaweza kuhamiabusirudi kabisa wakishakupunga madogoli.

Bro we si unasema hayo mambo huyaamini. Vipi tena?
 
Msanga ...panda GARI had gongolamboto; halafu. Panda za chanika, ukifika chanika panda za kwenda MSANGA ZALALA A.K.A MSANGA, KUNA VUMBI JEKUNDU HATARI, HAKUNA NETWORK LABDA AIRTEL ...UMEME HAMNA KULE NI MWENDO WA SOLAR TU, JUA KALI SODA ZA BARIDI HADI WAPANDE DARADARA KUTAFTA; GARI LIKIKUACHA INABIDI HADI ULISUBIRI LILUDI TENA....Kiwanja wanauza Kwa kurusha jiwe ndio kipimo,
 
Msanga ...panda GARI had gongolamboto; halafu. Panda za chanika, ukifika chanika panda za kwenda MSANGA ZALALA A.K.A MSANGA, KUNA VUMBI JEKUNDU HATARI, HAKUNA NETWORK LABDA AIRTEL ...UMEME HAMNA KULE NI MWENDO WA SOLAR TU, JUA KALI SODA ZA BARIDI HADI WAPANDE DARADARA KUTAFTA; GARI LIKIKUACHA INABIDI HADI ULISUBIRI LILUDI TENA....Kiwanja wanauza Kwa kurusha jiwe ndio kipimo,

Nilipita kule ila nilikaa siku moja tu. Ni kasehemu kadogo sana... Pale mwanaromange, kuna shule kubwa sana nadhani ni ya sekondari ile.ipo katika mazingira mazuri sana. Msanga hakuna hata shule ya kata?
 
Mkuu kuna Msanga mbili na zote ziko kisarawe.Moja ni Msanga zalala unapitia chanika na nyingine Msanga sokoni we unaenda ipi?
 
Ukitaka kwenda Msanga sokoni nenda Buguruni sokoni kuna Eicher pale panda ya yoyote inayopitia Msanga au inayoishia Msanga nauli ni 4000 au nenda Pugu kajiungeni kuna Noah nauli 5000.Kwa Eicher hao jamaa jamaa ni saa moja na musu na Noah ni saa moja mpaka dk 45.
 
Kumbuka hizo gari zote mwendo wake kama za magazeti Gesti ziko sh 5000 mpaka 2000 pamechagamka sana kuliko mahali popote ndani ya hiyo wilaya.Huko Zalala nenda mpaka chanika ndo utapelekwa Msanga Zalala.Karibu sana uzaramoni.Ukija wikiend hii kuwa makini unaweza sahau familia,kuna watu wapo huku hawajarudi kwao.
 
Kumbuka hizo gari zote mwendo wake kama za magazeti Gesti ziko sh 5000 mpaka 2000 pamechagamka sana kuliko mahali popote ndani ya hiyo wilaya.Huko Zalala nenda mpaka chanika ndo utapelekwa Msanga Zalala.Karibu sana uzaramoni.Ukija wikiend hii kuwa makini unaweza sahau familia,kuna watu wapo huku hawajarudi kwao.

Msanga center pale mwisho wa magari nilishafika, but huko Msanga Zalala sijafika ndo napasikia leo, though nimeshasikia kuhusu Msanga Ngongere. Msanga center pale hakuna watu wengi sana sijui huko msanga zalala. Na vipi, kuna shule ya sekondari ?.. Kutoka msanga center hadi msanga zalala, kuna umbali gani?
 
Mkuu kuna Msanga mbili na zote ziko kisarawe.Moja ni Msanga zalala unapitia chanika na nyingine Msanga sokoni we unaenda ipi?

Msanga sokoni, ambayo tayari nishafika. Hiyo msanga zalala sijafika bado, i think next time i have to go msanga zalala..Kati ya Zalala na sokoni ipi imechangamka? And wapi karibu kutokea chanika?
 
Back
Top Bottom