Unatafuta mawaidha kutoka kwa watz kuhusu safari ya Kenya?Watakuzingua bureee!Mada yako ungeiweka Kenya forums wakenya wangekukaribisha vizuri tu!Usiskize hizo hadithi za vijiweni.Kenya utafika na kutoka ukiwa mzima,Mombasa raha utataka kurudi tena.Kama ulivoambiwa paspoti,kadi ya yellow fever tu,hapo sawa.Ukifika usiwe na wasiwasi bora usiombe vitu unapoagiza,iwe mkahawani au dukani.Fanya kama mkenya,sema nipe soda moja,haraka!Au ukipenda uwe nyang'au kabisa sema wewe mathe(dada) au we buda(kaka)!Leta Soda na kaimati haraka,chap chap!Haha!Usiogope kujitambulisha kama mtz,wakenya wanapenda watz achana na utani wa hapa jf.Utapata rafiki wapya kwa wingi tu,bora usiwe mtu wa kunyamaza sana.Cheka,furahia ongea na watu,hata usiowajua.Karibu Kenya!