Nataka kwenda Dubai au China kununua simu nipeni maelekezo mliowahi kwenda

Usikatishwe tamaa na ndugu zako hapo juu.hiyo 20mil ni pesa ndefu. Wengi wao wanakupigia masimu ya 200k ambayo Kwa ujumla soko lake wewe mwenyewe unalijua, Kwa hicho kiwango ni wastan wa USD 8600. Hata ukisema utenge pesa ya mzigo Tu USD 4500 itatosha kabisa kununua mzigo. Ukisema uchukue headphone, chaja, ni zile accessories nyingine Kwa usd 1000 Tu mzigo utaukimbia mwenyewe.
inaonekana umzoefu kwenye haya mambo, unaweza kunisaidia ni yako????
 
Jamaa kakupa wazo zuri sana. Yani kama mimi naweza sema anza na mtaji wa 5mln kabisa. Ukiwa unaanza biashara kuna mambo mengi sana ya kujifunza, kuna makosa mengine sana unatafanya. Unatakiwa uwe mtu mvumivu na mtu wa kujifunza sana. Uvumulivu unakuja na pesa pia, uwe na pesa ya kwamba ukikosea unaweza anza tena. Ukigawa mtaji wako kwa 5mln utakuwa na chansi 4, ukifeli mara ya kwanza, una chansi ya pili, ukifeli tena unachansi ya tatu, mpaka ukifika mara ya 4 angalau unakuwa umekomaa.

Mtu yoyote asikuvunje moyo hapa.
Kama ndo unaanza biashara kuwa makini sana na maamuzi ya mwanzo maana ukikosea step pesa yote itazama. Nakupa tu ushauri hiyo 20m igawanye nusu.

Tafuta taarifa sahihi na maagent waaminifu hasa China ili uagize mzigo wa 10m.

Kuna watu wengi sana huagiza mizigo na kufika salama bila tabu kabisa.

Utaona kama kuna mafanikio kifaida katika huu mzigo then nenda mwenyewe, maana hapa utakuwa na detail za kuanzia seller range ya bei n.k na utakuwa na confidence ya kutokupoteza mtaji wako.
 
Kama ndo unaanza biashara kuwa makini sana na maamuzi ya mwanzo maana ukikosea step pesa yote itazama. Nakupa tu ushauri hiyo 20m igawanye nusu.

Tafuta taarifa sahihi na maagent waaminifu hasa China ili uagize mzigo wa 10m.

Kuna watu wengi sana huagiza mizigo na kufika salama bila tabu kabisa.

Utaona kama kuna mafanikio kifaida katika huu mzigo then nenda mwenyewe, maana hapa utakuwa na detail za kuanzia seller range ya bei n.k na utakuwa na confidence ya kutokupoteza mtaji wako.

Thubutu hata siku moja usithubutu kutumia ma AGENT utalia kilio cha samaki.

Ushahuri mbovu kabisa huu.
 
Bora umeongea
Agent lazima ale cha juu
Lazima akuletee usichotaka
Kipindi naanza kuuza spea za pikipiki katoro Geita rafiki yangu aliniunganisha na jamaa mmoja ambaye ni mzoefu wa kiagiza kutoka Dar.
Aliandaa oda ya 5ml na kesho yake nikaingiza pesa kwenye akaunti ya benki na nyingine M-pesa kwa kuwa yalikuwa ni makampuni 3 tofauti.
Baada ya siku 3 mzigo ukafika kama tulivyoandika oda na nikaanza biashara na jamaa nikampa posho ya elfu 50 kwa msaada wake.
Alahaula! Kumbe bora ningenunulia mzigo palepale katoro kwenye maduka ya jumla au ningepanda basi kwenda mwenyewe. Kuikweli NILIPIGWA VIBAYA. Laki 5 na 72 elfu ilipigwa kwa kugawanyisha mzigo kwenye ufungaji. Siku zinashuka box zangu na yeye zika shuka zake kumbe zimetoka kwenye hela yangu bila mimi kufahamu.
Kilichokuja kunitoa usingizini baada ya mwezi mzima kuna kampuni moja wapo iliambatanisha invoice copy. Bei tuloagizia ni tofauti na bei halisi ya Dar, jamaa alizidisha kwangu ila oda halisi ilikuwa na bei ya chini na ndio maana mzigo aliugawanya ili ufungwe tofauti. Nilichoka hoi.
Nilishukuru Mungu kwakuwa sikupigwa pesa yote na mzigo ulifika japo kwa gharama ya juu na faida kidogo. Nilimuuliza jamaa akakosa cha kujibu.
Potea njia wakati wa kwenda ila kurudi wewe ni mwenyeji. Nilifanya juu chini nikapata namba za makampuni husika tena kutoka kwenye simu yake bila ya yeye kufahamu. Alishangaa tu kuona mizigo inatiririka kutoka Dar. MWANZO MGUMU.
 
Kipindi naanza kuuza spea za pikipiki katoro Geita rafiki yangu aliniunganisha na jamaa mmoja ambaye ni mzoefu wa kiagiza kutoka Dar.
Aliandaa oda ya 5ml na kesho yake nikaingiza pesa kwenye akaunti ya benki na nyingine M-pesa kwa kuwa yalikuwa ni makampuni 3 tofauti.
Baada ya siku 3 mzigo ukafika kama tulivyoandika oda na nikaanza biashara na jamaa nikampa posho ya elfu 50 kwa msaada wake.
Alahaula! Kumbe bora ningenunulia mzigo palepale katoro kwenye maduka ya jumla au ningepanda basi kwenda mwenyewe. Kuikweli NILIPIGWA VIBAYA. Laki 5 na 72 elfu ilipigwa kwa kugawanyisha mzigo kwenye ufungaji. Siku zinashuka box zangu na yeye zika shuka zake kumbe zimetoka kwenye hela yangu bila mimi kufahamu.
Kilichokuja kunitoa usingizini baada ya mwezi mzima kuna kampuni moja wapo iliambatanisha invoice copy. Bei tuloagizia ni tofauti na bei halisi ya Dar, jamaa alizidisha kwangu ila oda halisi ilikuwa na bei ya chini na ndio maana mzigo aliugawanya ili ufungwe tofauti. Nilichoka hoi.
Nilishukuru Mungu kwakuwa sikupigwa pesa yote na mzigo ulifika japo kwa gharama ya juu na faida kidogo. Nilimuuliza jamaa akakosa cha kujibu.
Potea njia wakati wa kwenda ila kurudi wewe ni mwenyeji. Nilifanya juu chini nikapata namba za makampuni husika tena kutoka kwenye simu yake bila ya yeye kufahamu. Alishangaa tu kuona mizigo inatiririka kutoka Dar. MWANZO MGUMU.
Dar noma sana,jamaa alikufanya fursa.
 
Kipindi naanza kuuza spea za pikipiki katoro Geita rafiki yangu aliniunganisha na jamaa mmoja ambaye ni mzoefu wa kiagiza kutoka Dar.
Aliandaa oda ya 5ml na kesho yake nikaingiza pesa kwenye akaunti ya benki na nyingine M-pesa kwa kuwa yalikuwa ni makampuni 3 tofauti.
Baada ya siku 3 mzigo ukafika kama tulivyoandika oda na nikaanza biashara na jamaa nikampa posho ya elfu 50 kwa msaada wake.
Alahaula! Kumbe bora ningenunulia mzigo palepale katoro kwenye maduka ya jumla au ningepanda basi kwenda mwenyewe. Kuikweli NILIPIGWA VIBAYA. Laki 5 na 72 elfu ilipigwa kwa kugawanyisha mzigo kwenye ufungaji. Siku zinashuka box zangu na yeye zika shuka zake kumbe zimetoka kwenye hela yangu bila mimi kufahamu.
Kilichokuja kunitoa usingizini baada ya mwezi mzima kuna kampuni moja wapo iliambatanisha invoice copy. Bei tuloagizia ni tofauti na bei halisi ya Dar, jamaa alizidisha kwangu ila oda halisi ilikuwa na bei ya chini na ndio maana mzigo aliugawanya ili ufungwe tofauti. Nilichoka hoi.
Nilishukuru Mungu kwakuwa sikupigwa pesa yote na mzigo ulifika japo kwa gharama ya juu na faida kidogo. Nilimuuliza jamaa akakosa cha kujibu.
Potea njia wakati wa kwenda ila kurudi wewe ni mwenyeji. Nilifanya juu chini nikapata namba za makampuni husika tena kutoka kwenye simu yake bila ya yeye kufahamu. Alishangaa tu kuona mizigo inatiririka kutoka Dar. MWANZO MGUMU.
ndo usenge wa kufanya kazi na wabongo, lazma akupige ndio ajiskie amani. Uaminifu 0 ndio maana hata wakidakwa viwanja huwa ni deport tu haina msalia mtume...kufumba na kufumbua uko Kipawa
 
1. Nauli return ticket quanzhou ni usd 850 to 950

2. Hotel ni rmb 150 sawa na usd 22 per day

3.matumizi ya kula, kula vzr utatumia rmb 100 per day sawa na usd 14

4. Simu utaenda kununua dashatou hapo quanzhou unapanda basi kutokea shushanlou no.4 au no.2 ni rmb 7 sawa na usd 1

5. Simu za mill 20 utanunua siku 2 tu, itadepend na aina za simu utakazochukua ila vzr kuchukua simu kubwa kubwa ndo zitakulipa
Nb. Kwenye ndege mwisho simu 15 tu pia usitumie agent kukununulia simu utapata hasara nenda mwenyewe na pesa zako mkononi don't trust anyone




Sent from my HUAWEI MT7-L09 using JamiiForums mobile app
Hayo ndo mawazo yakujenga tunayoyataka, shukuran
 
Mkuu Kama Hutojali PM Na Hiyo Number Kwangu Pia
Naku(Pm) namba za mchina ( yuko china kiwandani) anadeal na accessories ukichati nae muulize bei ya accessories unazohitaji anaweza pia kukupa mwongozo wa simu unazohitaji
utagundua mtaji wako ni mkubwa mno tena
Naamini utaharakisha zaidi safari yako

All the best mkuu..!
 
Naku(Pm) namba za mchina ( yuko china kiwandani) anadeal na accessories ukichati nae muulize bei ya accessories unazohitaji anaweza pia kukupa mwongozo wa simu unazohitaji
utagundua mtaji wako ni mkubwa mno tena
Naamini utaharakisha zaidi safari yako

All the best mkuu..!
Mimi pia kaka km hutojali ni pmhizo namba
 
A
kiongozi hiyo pesa inatosha kabisa.Mimi naongelea China sababu ndio niko na uzoefu nako.Nauli inategemea na season.Ila ni ina range kwenye 700$ hadi 1200$,pia kumbuka tofauti ya siku unayokata ticketi na siku unayotaka kusafiri ina matter kwenye bei.ukikata mapema bei inakuwa nzuri kiasi.Kama unataka smartphone (iphone) nyingi ni bora uende Shenzhen Ila kama ni android nyingi ama unataka kuchanganya android na iphone basi guangzhou itakufaa.Hautanunua simu mpya kabsa (0 km) bali utanunua refubrished phone ambazo huko Tanzania ndio "mpya" hizi utanunua soko lina itwa dashatou.Kuhusu malazi kuna sehemu mbili ambazo ndizo wa afrika wengi (wa Tz) hupenda kukaa. Eneo moja linaitwa sanyuanli kwa metro ni line 2,(hili wengi wanaishi wanaokuja kununua nguo),na eneo la pili linaitwa xiaobei metro line 5(hapa kulitokea kashkash before ndo wengi wakakimbilia sanyuali).Bei huwa inaanza 120 RMB hadi 200 RMB kwa single room(kuna hotel unaweza pata kwa 100 RMB,ila huko foreigners wanaoishi ni wachache.Kama si mtu wa kujichanganya patakufaa.Ni sehemu ambako kuna soko la spare parts za pikipiki.)
Kwa mizuguko ya town kama ukiweza kutumia metro ama kujua namba za basi itakusaidia sana.Kwa basi ni 2RMB tu kwa route.Ila metro inategemeaa na unakoenda.Metro is much easier sababu hakuna traffic jam.Kama unataka accessories kuna soko ukienda kwa metro kituo kinaitwa cultural park utapata unachotaka.Lakini zaidi sana uwe mzoefu wa simu na ujue kuzikagua.Wachina huwa hawaamini hadi ajue wewe ni mtu wa kudumu otherwise unaweza ukanunua simu 50 na ukawa na return 30.
Kuhusu kutuma mizigo unaweza ukaenda nazo mwenyewe around pc 30,hizi ndo wanaruhusu ku board nazo.Ila kama ni nyingi unaweza nunua baadhi ya vitu (kama mikoba ya wadada,unaweka smu ndani na unacheki in mabegi)Otherwise ni watumie watuma mizigo wa huku(wanapatikana sanyuani siku hizi)Wata kucharge 10$ kwa kila simu na utapokea Tz kuanzia siku 2-5 toka uwakabidhi mzigo.
Hope nimekusaidia kiasi
You are the best
 
Huu ni ufinyu wa akili, kuna gharama za kujifunza, kwa mara ya kwanza anaweza asipate faida kubwa lkn kujifunza ni muhim sana katika biashara
20m ndo uende Dubai au china?
au unataka kwenda kutembea?
simu aina gani? kama unanua smart phone za laki mbili 20 unanunua simu ngapi?
una duka atayari au ununue ndo uanze tembeza?

Binafsi naona tafuta biashara ingine hapa ya uhakika mtaji hata 15m

5m nenda Dubai katembee ujionee na ujifunze
15 M hata Kkoo kwa wauzaji wa jumla unaweza pata faida
Ticket na malaxi China sio gharama kubwa
Sasa hiyo TZS 20 million ukitoa ticket na malazi unabakiwa na nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom