Nataka Kuoa Nitulie, Msaada Please

Nataka Kuoa Nitulie, Msaada Please

Power G

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2011
Posts
3,884
Reaction score
1,200
Wana mmu, naona kama vile umri wangu (miaka 35) umetosha kabisa kuwa na mwenza ili tuweze kuanza kutengeneza familia yetu. Lakini hadi sasa sijafanya uamuzi wa kwamba nioe mkoa gani. Lengo ni kwamba baada ya kuoa nisipate stress za ndani ya ndoa ambazo zitanifanya nilazimike kutafuta nyumba ndogo (nitulie kabisaa).

Kuna marafiki ambao wamejaribu kunipa dondoo ya baadhi ya mikoa ambayo wanaamini kuwa nikioa huko nitakuwa mfalme ndani ya nyumba yangu na kamwe sitakaa niwaze kutoka nje ya ndoa yangu, kwani hakuna nitakachokikosa au nitakalolikosa ndani na kushawishika kutafuta nje. Baadhi ya mikoa ninayotajiwa ni Tanga na Tabora. Nawaomba wana mmu mnipe uzoefu wenu ili nikioa nitulie kabisaa.
 
Uoe Mkoa wa Shinyanga; kigezo una madini ya dhahabu ya kutosha, ukishindwa kauoe mkoa wa Arusha ndio mkoa pekee wenye madini ya Tanzanite.
 
unaamini kabila fulani litakupa mke bora???
nachelea kusema unajitia kwny tatizo zaidi!

acha roho mbaya weye, au kwa vile ruvuma haijawekwa kwenye list?
mwaya Power G ngoja nikuunganishie na mke (mnyamwezi) wa kaka yangu (mnyamwezi) aliyemuendesha kaka yangu mpaka akaishia kwenye nyumba ndogo wa kipare; au la rafiki yangu mmoja wa kibondei ambaye bila wanaume 4 mzuka hautulii kabisa!
 
Last edited by a moderator:
Nakupa pole mkuu.Unasikitisha sana na kuhuzunisha.Naomba niishie hapo
 
acha roho mbaya weye, au kwa vile ruvuma haijawekwa kwenye list?
mwaya Power G ngoja nikuunganishie na mke (mnyamwezi) wa kaka yangu (mnyamwezi) aliyemuendesha kaka yangu mpaka akaishia kwenye nyumba ndogo wa kipare; au la rafiki yangu mmoja wa kibondei ambaye bila wanaume 4 mzuka hautulii kabisa!

angetajiwa ruvuma unafkir angekuja kuuliza huku,angetuwekea news alert tu!
NIMEOA MWANAMKE WA KINGONI,NAJUTA KUCHELEWA KUOA MIAKA YOTE!
 
Mkuu Power G njoo uoe kwetu. Sisi wakurya huwa tunawabeba wanaume mgongoni na kuwakogesha kama watoto wachanga. Nadhani hizo huduma zitakufanya utulie tuli na usiwe na mawazo ya kutoka nje.
 
::
Sitaki kuamini kuwa kuna mahusiano ya watu wawili ambao hupatana tu wakakosa stress!
::
Kama una amini kuna mkoa special ambao utapata ambae hatakupa stress,basi bado una safari ndefu ktk maisha yako.
::
Binadamu ni hawa hawa,Maisha ni haya haya,Usiache kumuoa aliye mkoa fulani kwa kutegemea mkoa fulani.Wote tuna mapungufu.
=
 
Jamani huwezi kumpata mke kwa kuangalia kabila au mkoa fulani kwani karibu kila kabila wako wema na wabaya, Mungu ameandaa wake wema wa kila lugha,kila kabila na kila taifa ili yule atakaye huyo mke mwema Bwana humuongoza tu aliko.
 
Duh... majanga... kama hujatulia kabla ya kuoa usitarajie kutulia ukioa, afterall anayehitaji kutulia sio mkeo bali ni wewe, na ukioa kabila ndo utajutaaa...
 
Oa unaempenda kila kabila lina kasoro zake. Lkn ukioa unaempenda naamini utaishi nae vizuri . Kuhusu kutulia inategemea wewe mwenyewe ndoa utaichukuliaje. Hauwezi kutulia kisa umeoa bali waweza kutulia ukiamua na kama utamthamini huyo utakaeoa. Halafu angalia usioe kisa umri umeenda bali oa kwasababu unampenda ulie nae. Kumbuka mke mwema mtu hupewa na Bwana.
 
mke si nguo,utaomba mtu uvaee weee,nyie ndio mnaingia ndoani na high expectations mkikuta vinginevyo mnaanza kuhangaikia,theres no such thing called perfect woman,wewe tafuta unayeendana naye kwa asilimia kubwa mengine kubali kyucompromizee siku ziende
 
Bado hauko tayari kuoa,subiri mpaka hayo mawazo yako ya kuoa mkoa yaishe kwanza.
 
mke mwema hawi determined by mkoa wala kabila ni yeye mwenyewe hilo swala la mkoa gani, duuuh.....
 
Bado hauko tayari kuoa,subiri mpaka hayo mawazo yako ya kuoa mkoa yaishe kwanza.
Mkuu huko kwenu, siwezi pata perfect wife? Lengo ni kwamba sitaki nikose baadhi ya mambo ndani ili niyafuate nje. Ni kweli kwamba wanaume wengi huenda nje ili kufuata yale wanayoyakosa ndani mwao.
 
Wana mmu, naona kama vile umri wangu (miaka 35) umetosha kabisa kuwa na mwenza ili tuweze kuanza kutengeneza familia yetu. Lakini hadi sasa sijafanya uamuzi wa kwamba nioe mkoa gani. Lengo ni kwamba baada ya kuoa nisipate stress za ndani ya ndoa ambazo zitanifanya nilazimike kutafuta nyumba ndogo (nitulie kabisaa).

Kuna marafiki ambao wamejaribu kunipa dondoo ya baadhi ya mikoa ambayo wanaamini kuwa nikioa huko nitakuwa mfalme ndani ya nyumba yangu na kamwe sitakaa niwaze kutoka nje ya ndoa yangu, kwani hakuna nitakachokikosa au nitakalolikosa ndani na kushawishika kutafuta nje. Baadhi ya mikoa ninayotajiwa ni Tanga na Tabora. Nawaomba wana mmu mnipe uzoefu wenu ili nikioa nitulie kabisaa.

Hehe kazi kweli kweli!
 
Apatae mke apata kitu chema na kibari machoni mwa Bwana.ckiliza mkuu kuanzia sasa kila unapotaka kulala na uamkapo asubuhi sali kwa dini yako mbali na mengine akupatie mke mwema,kwani ni mpango wake iwe hivyo.pamoja na hayo USITANGULIZE MAPENZI KABLA YA TARATIBU ZA MAISHA ambazo kila mtu ana za kwake.nitakupatia mwongozo A-isimame badala ya ability-thinkink capacity-acceptence kwao na kwenu.B-body structure,tambua mwanamke hubadirika kiumbo kutokana namajukumu yao ikiwamo uzazi.C-character-kama wewe ni mkimya alafu ukapata mcheshi utaboreka na kinyume chake pia.D-dizizi.kwa msisitizo,kunamagonjwa ya kurithi kama sekoseli,hali ya ualibino na mengine unayoyafahamu.E-education background.c kweli una jiwe la chuo chichote ukaoe la tano au la saba.au wewe ni form four mkeo ana masters hapo lazima uwe mwelewa kwelikweli la sivyo kuna kuburuzana na Mungu apite kati.F-family background.wachiyo,wachawi,wanakaa kwenye ndoa,utakuta mama hajaolewa mama mdogo nje,sgangazi mtu walewale,unafikiri mkitifuana watamshauri nini-ACHANA NAE ASIKUTISHE CC MBONA TUNAISHI.na mwisho G-inasimama kwa GOD huyu ndo kila kitu ukimwomba kwa dhati atakupatia,stoo yake ina watu wengi ispokuwa cc ndo tunakosea kumpangia nani awe mkeo au mumeo.TAMBUA KUWA C KILA MWANAUME ANAFAA KUWA MUME WA MTU NA C KILA MWANAMKE ANAFAA KUWA MKE WA MTU.akili kumkichwa.ukitanguliza mapenzi cku ukipata kibovu huwezi ku-let it go coz unampenda na ndo utakuwa msalaba wako.ukikosea kuoa tu umekosea maisha kwa sehemu kubwa.IMEANDIKWA WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.USIOE KWA WASIFU WA NJE OA KWA MWONGIZO WA MUNGU KWA WASIFU WA NDANI.fanya utafiti wengi wa walioolewa ni wakaida tu.mengine tumia akili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom