Faida na hasara za kuoa mwanamke msomi na mtumishi

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,800
Ni ndoto za wanaume wengi kuoa mwanamke mrembo na mwenye kipato ili wasaidiane kutengeneza familia bora ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri, kusomesha watoto kwenye shule bora n.k Hapo ndipo baadhi ya vijana hufikiria kuoa wanawake wasomi wenzao wenye kazi nzuri. Lakini kabla ya kufikiria kuoa mke msomi na mwajiriwa( hasa serikalini) ni vema ukajua faida na hasara zake.

Tukianza na faida
1. Mke mwajiriwa atakusaidia kuongeza kipato kwa maendeleo ya familia.

2. Pili,km hali yako ya kiuchumi ikiyumba,familia inaweza isiathirike na kama itaathirika basi ni kidogo.

3. Kazi/cheo cha mkeo kinaweza kuleta heshima fulani ndani ya familia.

Hasara zake:-
1. Kuna baadhi ya wanawake akichangia hela yake kununua kitu mfano kiwanja usishangae siku mkikosana akakudhalilisha kwamba kiwanja kanunua yeye au nyumba kajenga yeye.

2. Wanawake waliosoma na wenye kazi wengi wao (SI WOTE ) huwa si watiifu kwa waume zao hasa ikitokea kipato chake ni kikubwa kuliko mme.

3. Jiandae na mivutano ya haki sawa. Kuna baadhi ya wanawake wasomi huigeuza ndoa kuwa sehemu ya kufanya uanaharakati. Hali hii inaweza kuibua mivutano ya mara kwa mara.

4. Ndoa kuongozwa na vichwa 2. Maandiko yanasema, "Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe" Efeso 5:23.

Kuna baadhi wanawake wakishasoma na kuwa na ajira nzuri hujipa mamlaka ndani ya nyumba. Badala ya mume kuwa sauti ya mwisho kimaamuzi atataka yeye awe msemaji wa mwisho. "In nature"wanaume hatuko tayari kutawaliwa na mwanamke hapo inaweza kuwa chanzo cha ndoa yenu kusambaratika.

5. Ndugu wa mke kukudharau/ kutokupa heshima unayostahili hasa km familia yao ni ya kishua na wasomi.Hebu fikiria mkeo ni mkuu wa kitengo muhimu aafu wewe Mwalimu wa shule ya msingi( mfano tu), Usishangae kwa baadhi ya matukio ukawa wa mwisho kupewa taarifa. Tena usiombe iwe familia ya Kihaya( kidding).

6. Watoto wakigundua mama yao ana pesa nyingi kuliko baba heshima yao kwako inaweza shuka na usishangae kuona shida zao nyingi wanamalizana na mama yao. Hapa usipokuwa makini unaweza jikuta kama umetengwa ndani ya nyumba yako.

Kuna afande ni rafiki angu hiki kimemkuta, watoto hawana time nae kabisa.

7. Usitegemee neno pole na kazi au kupokewa mzigo utokapo kazini. Mwanamke mwenye kazi anajiona hata yeye ni mtafutaji. Hivyo anaweza asione sababu ya kukupokea kwani hata yeye katoka kutafuta huo mkate.

8. Kuna wakati "Stress"za kazini anaweza kuzihamishia nyumbani. Hapo ndo hatari maana anaweza kukosa hata hamu ya kukupa unyumba.

9.Kuleta ubosi kitandani. Wanawake wengi wenye kazi na mabosi hujisahau na kuleta ubosi wao hadi nyumbani. Hivyo mkiwa faragha usishangae kauli za kibabe na wengi wao hawawezi kuwa romantic.

Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo mengi nimejifunza kwa brother yangu aliyeoa Daktari mwenzake mwenye cheo kikubwa kuliko yeye na kwa baadhi ya wafanyakazi wenzangu.

NB: Niko tayari kurekebishwa.


Pia soma hoja hii ilivyojibiwa: Kamgomoli: Mwanamke wa Miaka ile sio Mwanamke wa leo
 
Ni ndoto za wanaume wengi kuoa mwanamke mrembo na mwenye kipato ili wasaidiane kutengeneza familia bora ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri,kusomesha watoto kwenye shule bora n.k Hapo ndipo baadhi ya vijana hufikiria kuoa wanawake wasomi wenzao wenye kazi nzuri. Lakini kabla ya kufikiria kuoa mke msomi na mwajiriwa( hasa serikalini) ni vema ukajua faida na hasara zake.

Tukianza na faida
1.Mke mwajiriwa atakusaidia kuongeza kipato kwa maendeleo ya familia.
2.Pindi hali yako ya kiuchumi ikienda vibaya,familia inaweza isiyumbe na km itayumba basi ni kidogo.
3.Kazi/cheo cha mkeo kinaweza kuleta heshima fulani ndani ya familia.

Hasara zake:-
1.Kuna baadhi ya wanawake akichangia hela yake kununua kitu mfano kiwanja usishangae siku mkikosana akakudhalilisha kwamba kiwanja kanunua yeye,au nyumba kajenga yeye.

2. Wanawake waliosoma na wenye kazi wengi wao (SI WOTE ) huwa si watiifu kwa waume zao hasa ikitokea kipato chake ni kikubwa kuliko mme.

3.Jiandae kuhusu mivutano ya haki sawa. Kuna baadhi ya wanawake wasomi huigeuza ndoa kuwa sehemu ya kufanya uanaharakati. Hali hii inaweza kuibua mivutano ya mara kwa mara.

4.Ndoa kuongozwa na vichwa 2. Maandiko yanasema, "Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe" Efeso 5:23.

Kuna baadhi wanawake wakisha soma na kuwa na ajira nzuri hujipa mamlaka ndani ya nyumba. Baadala ya mume kuwa sauti ya mwisho kimaamuzi atataka yeye awe msemaji wa mwisho. "In nature"wanaume hatuko tayari kutawaliwa na mwanamke hapo inaweza kuwa chanzo cha ndoa yenu kusambaratika.

5.Ndugu wa mke kukudharau/ kutokupa heshima unayostahili hasa km familia yao ni ya kishua na wasomi.Hebu fikiria mkeo ni mkuu wa kitengo muhimu aafu wewe Mwalimu wa shule ya msingi( mfano tu), Usishangae kwa baadhi ya matukio ukawa wa mwisho kupewa taarifa. Tena usiombe iwe familia ya Kihaya( kidding).

6.Watoto wakigundua mama yao anapesa nyingi kuliko baba heshima yao kwako inaweza shuka na usishangae kuona shida zao nyingi wanamalizana na mama yao. Hapa usipokuwa makini unaweza jikuta km umetengwa ndani ya nyumba yako.
Kuna afande ni rafiki angu hiki kimemkuta,watoto hawana time nae kabisa.

Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo mengi nimejifunza kwa brother angu aliyeoa Daktari mwenzake mwenye cheo kikubwa kuliko yeye na kwa baadhi ya wafanyakazi wenzangu.

NB: Niko tayari kurekebishwa.
Mwanamke msomi PhD masters hata ukinipa bure sichukiwi ni kama kubeba gunia la misumari kichwani.
 
Umesahau kuhusu

1. tendo la ndoa:
wanawake wasomi wagumu kutoa ushirikiano kwenye tendo na ni wavivu kitandani kwa madai kuwa wako buzy na majukumu ya ofisi.

2.Kugongewa mkeo:
Kwenye trip za ofisi mikoani na wafanyakazi wengine, unakuta trip ni ya 3 weeks au zaidi,
Hapa kuna hatohati mkeo KULIWA KIMASIHARA.

Zingine maboss wanakuja kuchangia

Sent from my SM-M307F using JamiiForums mobile app
 
Unatakiwa kupima tu mwenyewe, uoe msomi mwenzako na heshima yako kama baba ni swala la 50-50 au uoe mama wa nyumbani na ubebe majukumu yote kama kichwa cha familia na heshima yako iwe juu.

Swala la kuachana na kugawa mali liko pale pale iwe umeoa mfanyakazi mwenzako au mama wa nyumbani. Hizo mali kisheria ni zenu wote. Ndio maana emwanaume siku hizi wanaona either wafiche baadhi ya mali au washee katika majukumu ya maendeleo ya familia coz either way lazima mgawane tu.
 
Uko sawa ila nakuambia ivi mwanamke mweny kazi hutomfaidi mfano mm nilikuwa intership taasisi fulani miaka ya nyuma nilikuta utaratibu huu kuingia saa mbili kutoka saa 11 jioni Tena pakiwa na kazi mpaka 1 usiku na weekend overtime lazima kama hatokuja jumamosi basi jumapli

Point yangu mke ana spend masaa 11 kwa siku za wiki means ana mapumziko ya siku moja na baada ya kurudi kazini mpaka kufika kwake ni usiku pigilia mahesabu na foleni za dar kazi posta kwake kimara au mbezi akifika usiku je huo mda wa kuact kama mama mwenye nyumba ni masaa mangapi na mda wa kupakuana na mumewe anakuwa amachoka hilo moja

La pili hapa kazini hujui aliyeolewa wala aliyeoa kukumbatiana hadharani japo sio code za utumishi ila hivi sio vizuri jua kabisa hata mkeo awe vip anatakiwa kujielewa akiwa na mazoea ya kishamba ataliwa sana

Kingine mke ana spend mda mwingi na wafanyakazi wenzie include wakiune kuliko wewe

Kiasili wanawake wasomi anatakiwa ajitambua na awe na udini na kujiheshimu kama ni ile kanda ya kina maria surungi ,mange kimavi angalia sana au angalia meno Kama yamechakaa wanajikuta wajuaji hWajui nafasi yao wengine wanaamua kuwa ma Tomboys kabisa
 
Kwenye hii dunia kila mtu ana mitizamo yake. Hata kwenye kuoa, watu hawaoi kwa sababu zinazofanana. Mwingine anatafuta mke anayevuta bangi ili apate kampani hahahahaha.

Hata hivyo nakubaliana na mleta mada. Kwa bahati mbaya kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda mwanamke anabadilika kutoka kuwa complimentor wa mwanaume hadi kuwa compitititor. Hapo ndipo shughuli inapoanzia.
 
Kwenye hii dunia kila mtu ana mitizamo yake. Hata kwenye kuoa, watu hawaoi kwa sababu zinazofanana. Mwingine anatafuta mke anayevuta bangi ili apate kampani hahahahaha.

Hata hivyo nakubaliana na mleta mada. Kwa bahati mbaya kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda mwanamke anabadilika kutoka kwa complimentor wa mwanaume hadi kuwa compitititor. Hapo ndipo shughuli inapoanzia.
Mkuu point yako imeeleweka wanawake wa sasa hawapambani kuleta maendeleo ila wanataka usaw hapo do wanakokosea sana
 
Kwa mtizamo wangu, ukioa mke kwa mtizamo kuwa aje akusaidie a.k.a kusaidiana, unakuwa ushaanza kwa mguu wa kushoto. Ni suala la mda tu utalia kimanga.

Unatakiwa kuoa mwanamke kwa jicho la wewe kumsaidia yeye. Ukiwa na mtizamo wa namna hiyo ni ngumu kuwa disappointed.

Kwa mantiki hiyo, kabla ya kuoa, unapaswa ujiulize, unayemuoa anahitaji msaada wako? Anahitaji aina ya msaada unaotaka kumpa? Kama jibu ndio oa, kama sio, wewe unachotakiwa ni kummzabzab kisha pita. Huyo sio wako, waachie wengine. Kumbuka hupaswi kulazimishia kumpa mtu huduma kama mwenyewe haoneshi kuihitaji ( haijalishi uzuri wa huduma yako)

Kwa ujumla dhana ya mwanaume kufikiria kusaidiwa na mwanamke kuanzia mwanzo ni mtego wa hatari sana. Kwa bahati mbaya zaidi ni kwamba kwa sasa wanawake wanakuwa na nguvu za kiuchumi na kimamlaka kuliko wanaume na hivyo taasisi ya ndoa kuwa miguu juu kifo cha mende. In the future, wanaume wanaweza kuolewa na wanawake. Kwa lugha nyingine wanawake kushika nafasi ya wanaume na wanaume kushika nafasi za wanawake kwenye familia na maisha kwa ujumla. Kwa bahati mbaya zaidi hatuna la kufanya kuzuia hii kutokea.

Kwa mfano zamani hata ukiongea na mwanamke alikuwa na aibu anaangalia chini, siku hizi anakutolea macho hadi wewe ndio unaona aibu.

In the future, wanawake wasomi watatongoza wanaume na wanaume wataanza kuringa ringa kama wanawake wa zamani.

Basi utakuta mwamba anatupiwa mistari na mwanadada, huku mwamba kainamia chini anachimba kashimo kwa miguu. Dunia ngumu sana hii ndugu zangu.
Mkuu point yako imeeleweka wanawake wa sasa hawapambani kuleta maendeleo ila wanataka usaw hapo do wanakokosea sanai
 
Imagine umeoa mwanamke msomi kabisa, yeye kule ofisini ndio HoD labda, stress levels zake zinakuwa juu sana wakati mwingine. Swala la kumnyandua kila wakati liweke pembeni, yeye ndio ata-initiate sex, sio wewe! Pro's and Co's zipo nyingi, ni swala la wewe kuamua tu unataka maisha ya namna gani.
 
Kwa mtizamo wangu, ukioa mke kwa mtizamo kuwa aje akusaidie a.k.a kusaidiana, unakuwa ushaanza kwa mguu wa kushoto. Ni suala la mda tu utalia kimanga.

Unatakiwa kuoa mwanamke kwa jicho la wewe kumsaidia yeye. Ukiwa na mtizamo wa namna hiyo ni ngumu kuwa disappointed.

Kwa mantiki hiyo, kabla ya kuoa, unapaswa ujiulize, unayemuoa anahitaji msaada wako? Anahitaji aina ya msaada unaotaka kumpa? Kama jibu ndio oa, kama sio, wewe unachotakiwa ni kummzabzab kisha pita. Huyo sio wako, waachie wengine. Kumbuka hupaswi kulazimishia kumpa mtu huduma kama mwenyewe haoneshi kuihitaji ( haijalishi uzuri wa huduma yako)
Ok kwahiyo tuendelee kuwagegeda tuu au sio🤣🤣🤣🤣
Aisee wanawake watafika mbinguni wamechoka sana.
 
Hahahahaha naomba nistoe maoni yangu kwenye hili.
Sawa mkuu ila umeongea bonge la point. Kwa hawa wanawake wa sasa ukitaka kuoa uingie ukijua wao wanakuja kuchukua tuu na sio kutoa, which in essence defeats the purpose ya marriage. Hence why, ni bora tugegegduane tuu lah sivyo ukiingia na mentality ya kusaidiana utampoga mtu risasi saba bure.
 
Ni ndoto za wanaume wengi kuoa mwanamke mrembo na mwenye kipato ili wasaidiane kutengeneza familia bora ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri,kusomesha watoto kwenye shule bora n.k Hapo ndipo baadhi ya vijana hufikiria kuoa wanawake wasomi wenzao wenye kazi nzuri. Lakini kabla ya kufikiria kuoa mke msomi na mwajiriwa( hasa serikalini) ni
Faida ni 3 na hasara ni 6?
 
Ngoja niwape real story about my marriage....japokuwa sii ndoa kbs ya kufunga harusi ila NI tunaishi Zaid ya mwaka Sasa...Mimi nimeajiriwa fresh kbs na huyu shemeji/wifi yenu NI kwamba hajasoma hajamaliza la Saba ila NI mvumilivu Sana na ananitii Sana hana mambo mengi just imagine haniombi pesa yoyote kikubwa ninunue chakula,mavazi na kulipa bills...

Nimekubali TU nitoe huduma japo natamani kweli nimfundishe baadhi ya current issues ili ajie ile knowledge general...ili baadae Mungu akinibariki naye nimfungulie biashara ujasirimali...kinachonishangaza me NI mlevi sometimes nalewa narudi akinikera kidogo au kiburi kdg bas anakula makofi ya kufa mtu kesho najutia Ila hataki kutoka kesho yanaisha na mapenzi Kama yote...

At the same time wazazi wangu wa kike mashangazi etc wamesoma Sana na Bado ndoa zao nahisi ziko vzr japo siwezi kujua Siri za ndani ila hawajaachwa.
 
Back
Top Bottom