Nataka kuoa jini

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Sep 7, 2016
17,374
21,069
Wakuu nina hamu sana ya kuoa jini
Sababu kuu zilizopelekea kufikia uamuzi huu ni hizi

1)Majini hayachepuki

2)Majini hayaombi hela

3)Majini hayana magonjwa ya zinaa kama vile ukimwi

4)Majini yanajua kuhonga sana pesa So nitakuwa milionea kama Bakhresa

5)Nitakuwa nafanikiwa sana katika mishe zangu kama vile mitihani nitakuwa napasua saana kwa kuwa swali likinishinda mke wangu anakuja kunijazia

6)Nitakuwa na ulinzi popote pale niendapo kuanzia ulinzi wa ulimwengu wa giza mpaka ulimwengu wa nuru

Ulimwengu wa giza hapa namaanisha wachawi hawataweza kunifata hata kidogo na wakithubutu tu mke wangu atawamaliza

Ulimwengu wa nuru hapa namaanisha wezi ,majambazi nk hawataweza kunifanya chochote hivyo basi sitakuwa na haja ya kuajili watu wa ulinzi wala bodyguard wa aina yoyote ile


Pia kingine uzuri wa majini ni kuwa nikitaka kitendo cha unyumba nitakipata muda wowote ule ninao hitaji ,majini hayasumbui hovyo kugawa unyumba So ntaachoma zangu tu udi then naamuita mke wangu ananipa unyumba au lah ananibeba mpaka ujinini naenda kula vyakula vya kule ambavyo wenyewe waanaita Chane kiroho saafi yani



Naimani ndoto yangu ya kupata jini itatimia .
 
Haya yoote uliyajuaje kuwa yanapatikana kwa mke jini?
Nawe unazo sifa ambazo mke jini, anazitaka kwa mume mtarajiwa?
 
Back
Top Bottom