a sinner saved by Christ
JF-Expert Member
- Feb 19, 2017
- 2,428
- 2,609
KILA MTOTO WA MUNGU ANAYEMCHA MUNGU (ana ulinzi wa UKINGO/UKUTA kutoka kwa Mungu unaomzingira pande zote yeye pamoja na mali zake kama mtumishi wa Ayubu)
Ayubu 1:10
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
Lakini adui yetu,mshitaki wetu shetani huzunguka kama simba aungurumaye akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8) na huyu adui yetu kazi yake ni kuiba,kuchinja na kuharibu(yohana 10:10)
Wakati mwingine huyu adui yetu anaua na kuiba vitu vyako vya ndani kama NDOA yako,UCHUMI wako,IMANI yako au hata afya yako hata kama kwa nje unaonekana upo sawa ,ila kwa ndani ameshakumaliza unabaki kama kasha tupu,kopo tu kwa nje zuri ndani halina kitu.
SIFA YA VITU VYAKO VYA NDANI VILIVYOKUFA
NDOA iliyokufa ndani...wanandoa hawazungumzi pamoja ,tena wanaweza wakaishi kila mmoja na chumba chake,upendo wao unapoa unafutika kabisa,wanachukiana ,wanalaumiana kila mmoja ana mshutumu mwenzake mbaya,kupigizana makelele.
UCHUMI uliokufa...umasikini..kufikisika,pesa kupotea,kufunga kwa milango ya fursa za biashara na uchumi zilizokuwa wazi mwanzo,kupata pesa kwa shida kazi kubwa kama tembo mapato kiduchu kama panya,na hata ukipata matumizi mengi yanaibuka kuimaliza,madeni makubwa kuliko uwezo wako,wale watu waliokuwa wanakusapoti kwa fursa za kiuchumi kujitenga mbali,kila jitihada za kujikwamua kiuchumi zinafeli
AFYA..magonjwa yasiyo isha maradhi kuugua mara kwa mara..maradhi sugu
FANI YAKO NA UJUZI
Kudumaa hata kama una ujuzi hupigi hatua wala hupati fursa,haunufaiki kwa kiwango stahili na fani yako na hupigi hatua unadumaa.
TABIA ZINAZOPELEKEA KUPASUKA/KUVUNJIKA NYUFA KATIKA KUTA/UKINGO WA ULINZI WA MUNGU..unaokuzingira mtoto wa Mungu.
Ukuta/ukingo ulinzi wako kutoka kwa Mungu hupasuka na kuweka uwazi pale mtoto wa Mungu anapofanya mambo yafuatayo.
1)DHAMBI ZISIZOTUBIWA/kutokutubu dhambi zetu haraka kwa wakati mapema sana .
Dhambi zisizotubiwa zinabomoa ukuta..(dhambi zenu ndio zina achilia mauti ,ndio zinawatenga na Mungu hata asiweze kusikia,hata sadaka za mtu mwovu ni chukizo.
Ni lazima kuishi maisha ya TOBA kila wakati TUBU DHAMBI kila mara ,mtakatifu na azido kutakaswa..
2)LAANA ZA UKOO
wazazi wetu mababu na mabibi walitenda dhambi kabla yetu hata kabla hatupo ila maovu yao tunapatilizwa yametupata sisi hata kizazi cha tatu na cha nne,unakuta walitambikia MIZIMU,waganga wa kienyeji,wakaweka maagano kwa mizimu ,na majini ya ukoo yakatumiliki sisi na vizazi vyetu vijavyo..
3)KUTOKUSAMEHE watu,vinyongo kuweka vinyongo visasi moyoni
4)HASIRA CHUKI
5)MANENO YAKO mwenyewe ukijilaani mwewe bila kujua ,mfano unakuta mtu anajilaani mwenyewe bila kujua mfano anasema ,MIMI huu naona lazima nitakufa tu sitapona,au mimi ni wa kupata hasara tu,mimi siwezi,mimi sina uwezo,sina akili,kwetu wote huwa tuna ugonjwa wetu,kwetu hatuoi,..mimi ni masikini..n.k..UMENASWA kwa maneno ya kinywa chako mwwnyewe usijinenee mabaya
5)Uzinzi,ulevi n.k yani dhambi zote zinaingia kwenye point namba moja ya dhambi,lakini hapa nakuongezea point moja ambayo ulikuwa huijui...KUZURURA USIKU WA MANANE MBALI NA NYUMBANI KWAKO...mfano kuanzia saa sita usiku ukiwapo nyumbani kwako kuna ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu unaokulinda.
hapa nitoe mfano kabisa
kuna mtumishi wa Mungu tulikuwa tunamfuatilia kwa muda wa miaka miwili kupitia roho fuatilizi hapa tulitumia KIOO vitu vyote vya kioo kama vioo vya makabati ya nguo hasa vioo vinavyowekwa vyumba vya kulala vikitazama kitanda chako.(ni kama cctv kamera )
alikuwa mtumishi wa Mungu mtakatifu sana kwa muda wa miaka miwili ya kumfuatilia hatukuweza kumuangusha,alitumika kanisani kuhubiri,kufundisha vijana habari za ndoa akiwa na ndoa nzuri yenye upendo furaha na amani na familia yake.
Mtu wa maombi sana...yani mlokole kweli kweli..toa sadaka hakosi ibada ..na watu wote walimuona kama mfano wa kuigwa na mshauri wa watu..katika masuala ya kiroho na ndoa
tatizo lake lilikuwa moja tu ...*HASIRA KALI INAYOLIPUKA KAMA MOTO WA PETROLI"
ukuta wake ukingo wa Mungu ukaweka mwanya ukapasuka kwa hasira zake za mara kwa mara..
tukaanza kumshambulia kiroho..kidogo kidogo .hasira yake tukaiongeza mara dufu..tukaachilia roho ya umasikini..akaanza kupata changamoto za kiuchumi..tukaanza kumshambulia na mke wake..kumuwekea roho ya malalamiko/lawama
siku moja ametoka kazini amechoka na huko kazini bosi wake kamfokea sana kutokana na sisi kumuharibia hata kazini kwake kila anachofanya kinaonekana kibaya hata kazini..alipofika nyumbani kakuta mkewe anamsubiri na malalamiko kuwa hana msaada nyumbani hata hela ya saluni hajaacha,ada ya mtoto hajalipa,bili kadhaa za nyumbani mkewe kamjaza hasira kuwa hata nyumbani kwao ameanza kudharaulika kwa kumfananisha na wanaume wengine walio waoa dada zake shemeji zake wengine kuwa yeye ametia aibu na maneno mengine ...ya KUMJAZA HASIRA.
mwanzoni alijitahidi kubadilisha maongezi alihitaji kusali na kupumzika tu alijitahidi kunyamaza na kubadilisha stori..mkewe aliendelea kumoigia kelele kuanzia saa 4 usiku mpaka saa sita usiku na robo...jamaa alihitaji kula na kupumzika tu kulala kwa amani na kusali..lakini uvumilivu ukamshinda ...AKALIPUKA HASIRA akafungua mlango na kuanza kutoka nje ....mkewe na watoto wakawa wanamvuta asiondoke usiku abaki nyimbani huku wanalia ...akawasukumu akaondoka usiku huo...na hajui anakoenda anenda popote atakapokuwa ili mradi apate sehemu ya kutuliza mawazo yake mbali na makelele.
Bila kujua kuwa sisi ndio tunaosababisha hayo yote ni kazi yetu ya nguvu za giza.
HAPA ALIFANYA MAKOSA WAWILI kwa pomoja yanayozidi kubomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwake.
1)KUONDOKA eneo la nyimbani kwake USIKU kuanzia saa6
2)AKIWA AMEJAA HASIRA.
kufupisha tulimsukumia roho ya ulevi...tulianza kidogo kidogo .kumuwekea burudani kidogo kwenye pombe na kuona kwamba pombe ndio inayomuondolea matatizo
baadae tukamuwekea URAIBU na utegemezi wa pombe...akawa mlevi sugu ..
NDOA ikavunjika baadae wakapeana talaka mke akarudi kwao na watoto.
baadae maisha ya IMANI yakashuka akaacha kusali.
mwanzo alikunywa pombe kwa siri kwa kujificha baadae kakawa mlevi sugu...
akageuka aibu mfano mbaya ..kwa jamii.
Mwisho wa siku ..so sad RIP.
IAMBIE MIFUPA MIKAVU ILIYOKUFA KATIKA MAISHA YAKO IFUFUKE(Ezekieli 37 1-15)
Toa unabii juu ya mifupa hii. Iambie hivi: Enyi mifupa mikavu, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu. Bwana Mwenyezi-Mungu awaambia hivi: Nitaifanya pumzi iwaingie, nanyi mtaishi.
CHUKUA HATUA HII
Tambua eneo lolote katika maisha yako ambalo limekufa ambalo ndio kiunabii linaitwa mifupa mikavu lisemeshe maneno ya ezekieli 37 ;1-15
sema hivi wewe NDOA YANGU-mifupa mikavu taja eneo husika katika ndoa kama ni (mawasiliano hamzungumzi/mawasiliano hakuna,upendo umepote,n.k) sema nakutolea unabii,sikia neno la Mungu nitafanya pumzi ya Mungu ikuingie nawe utaishi, fanya hivyo kila siku asubuhi unapoamka na jioni unapolala kwa muda wa siku 21 mpaka 30...utanishukuru baadae.
maeneo yote yenye mifupa mikavu yaliyokufa kwenye maisha yako,iwe ni uchumi wako eneo lako la kazi ,AFYA YAKO n.k
JENGA UPYA UKINGO WA UKUTA WA ULINZI WA MUNGU ULIOBOMOKA(Ezekieli 22:30*
Ezekieli 22:30
Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, *na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka", kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.
tambua mambo yaliyobomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwako.
kama ni laana za ukoo
tamka maneno haya
BWANA MUNGU nasimama mbele yako kama kwa ajili ya familia yangu ukoo wangu kuziba pale walipobomoa kwa maagano ya ukoo ya damu za ukoo,naziba pale mababu zangu walipopabomoa ,uharibifu hautatupata familia yengu.
tamka maneno hayo kila siku mfululizo.
NB NI MUHIMU kutamka kila siku mfululizo bila kuruka hata siku moja kwa muda wa siku kuanzia 21-30..kadiri unavyotamka kila siku kwa uaminifu na imani,kwa ujasiri utapata matokeo.
siku nyingine nitongelea kuhusu roho fuatilizi zinazofuatilia maisha yako bila wewe kujijua nyumbani kwako ni kama kamera inayomulika
maisha yako kirioho ,kiuchumi adui anajua kuwa siku tatu zijazo au wiki moja mbele utapata mafanikio kwenye eneo fulani au utapata pesa hivyo nazuia hizo baraka zisikufikie ndio maana hata ukikaribia kupata hela mkono unawasha..ina maana yake..
vioo glass vitu vyote vya vioo hata hii simu,madirisha ya kioo,na vioo vya kabati za chumbani na dressing table pembeni ya kitanda chako,wanyama na ndege kama mijusi,paka,n.k
cha kufanya takasa kwa mafuta vioo vyako visitumike kuchunguza maisha yako kupeleka taarifa ulimwengu wa giza .
kama huwa unajisikia kama kuna mtu anakuangali rohoni unajihisi kama kuna mtu mahali anakuona kwenye television yake...(wengi watapuuza haya ni chakula cha kiroho cha watu wazima waliokomaa kiroho .sio watoto wanaonyonya maziwa ..watakuja kupinga..ila roho mtakatifu atusaidie kutambua MBINU ZOTE ZA ADUI ANAZOTUMIA tupate maarifa..
Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa
Ayubu 1:10
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
Lakini adui yetu,mshitaki wetu shetani huzunguka kama simba aungurumaye akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8) na huyu adui yetu kazi yake ni kuiba,kuchinja na kuharibu(yohana 10:10)
Wakati mwingine huyu adui yetu anaua na kuiba vitu vyako vya ndani kama NDOA yako,UCHUMI wako,IMANI yako au hata afya yako hata kama kwa nje unaonekana upo sawa ,ila kwa ndani ameshakumaliza unabaki kama kasha tupu,kopo tu kwa nje zuri ndani halina kitu.
SIFA YA VITU VYAKO VYA NDANI VILIVYOKUFA
NDOA iliyokufa ndani...wanandoa hawazungumzi pamoja ,tena wanaweza wakaishi kila mmoja na chumba chake,upendo wao unapoa unafutika kabisa,wanachukiana ,wanalaumiana kila mmoja ana mshutumu mwenzake mbaya,kupigizana makelele.
UCHUMI uliokufa...umasikini..kufikisika,pesa kupotea,kufunga kwa milango ya fursa za biashara na uchumi zilizokuwa wazi mwanzo,kupata pesa kwa shida kazi kubwa kama tembo mapato kiduchu kama panya,na hata ukipata matumizi mengi yanaibuka kuimaliza,madeni makubwa kuliko uwezo wako,wale watu waliokuwa wanakusapoti kwa fursa za kiuchumi kujitenga mbali,kila jitihada za kujikwamua kiuchumi zinafeli
AFYA..magonjwa yasiyo isha maradhi kuugua mara kwa mara..maradhi sugu
FANI YAKO NA UJUZI
Kudumaa hata kama una ujuzi hupigi hatua wala hupati fursa,haunufaiki kwa kiwango stahili na fani yako na hupigi hatua unadumaa.
TABIA ZINAZOPELEKEA KUPASUKA/KUVUNJIKA NYUFA KATIKA KUTA/UKINGO WA ULINZI WA MUNGU..unaokuzingira mtoto wa Mungu.
Ukuta/ukingo ulinzi wako kutoka kwa Mungu hupasuka na kuweka uwazi pale mtoto wa Mungu anapofanya mambo yafuatayo.
1)DHAMBI ZISIZOTUBIWA/kutokutubu dhambi zetu haraka kwa wakati mapema sana .
Dhambi zisizotubiwa zinabomoa ukuta..(dhambi zenu ndio zina achilia mauti ,ndio zinawatenga na Mungu hata asiweze kusikia,hata sadaka za mtu mwovu ni chukizo.
Ni lazima kuishi maisha ya TOBA kila wakati TUBU DHAMBI kila mara ,mtakatifu na azido kutakaswa..
2)LAANA ZA UKOO
wazazi wetu mababu na mabibi walitenda dhambi kabla yetu hata kabla hatupo ila maovu yao tunapatilizwa yametupata sisi hata kizazi cha tatu na cha nne,unakuta walitambikia MIZIMU,waganga wa kienyeji,wakaweka maagano kwa mizimu ,na majini ya ukoo yakatumiliki sisi na vizazi vyetu vijavyo..
3)KUTOKUSAMEHE watu,vinyongo kuweka vinyongo visasi moyoni
4)HASIRA CHUKI
5)MANENO YAKO mwenyewe ukijilaani mwewe bila kujua ,mfano unakuta mtu anajilaani mwenyewe bila kujua mfano anasema ,MIMI huu naona lazima nitakufa tu sitapona,au mimi ni wa kupata hasara tu,mimi siwezi,mimi sina uwezo,sina akili,kwetu wote huwa tuna ugonjwa wetu,kwetu hatuoi,..mimi ni masikini..n.k..UMENASWA kwa maneno ya kinywa chako mwwnyewe usijinenee mabaya
5)Uzinzi,ulevi n.k yani dhambi zote zinaingia kwenye point namba moja ya dhambi,lakini hapa nakuongezea point moja ambayo ulikuwa huijui...KUZURURA USIKU WA MANANE MBALI NA NYUMBANI KWAKO...mfano kuanzia saa sita usiku ukiwapo nyumbani kwako kuna ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu unaokulinda.
hapa nitoe mfano kabisa
kuna mtumishi wa Mungu tulikuwa tunamfuatilia kwa muda wa miaka miwili kupitia roho fuatilizi hapa tulitumia KIOO vitu vyote vya kioo kama vioo vya makabati ya nguo hasa vioo vinavyowekwa vyumba vya kulala vikitazama kitanda chako.(ni kama cctv kamera )
alikuwa mtumishi wa Mungu mtakatifu sana kwa muda wa miaka miwili ya kumfuatilia hatukuweza kumuangusha,alitumika kanisani kuhubiri,kufundisha vijana habari za ndoa akiwa na ndoa nzuri yenye upendo furaha na amani na familia yake.
Mtu wa maombi sana...yani mlokole kweli kweli..toa sadaka hakosi ibada ..na watu wote walimuona kama mfano wa kuigwa na mshauri wa watu..katika masuala ya kiroho na ndoa
tatizo lake lilikuwa moja tu ...*HASIRA KALI INAYOLIPUKA KAMA MOTO WA PETROLI"
ukuta wake ukingo wa Mungu ukaweka mwanya ukapasuka kwa hasira zake za mara kwa mara..
tukaanza kumshambulia kiroho..kidogo kidogo .hasira yake tukaiongeza mara dufu..tukaachilia roho ya umasikini..akaanza kupata changamoto za kiuchumi..tukaanza kumshambulia na mke wake..kumuwekea roho ya malalamiko/lawama
siku moja ametoka kazini amechoka na huko kazini bosi wake kamfokea sana kutokana na sisi kumuharibia hata kazini kwake kila anachofanya kinaonekana kibaya hata kazini..alipofika nyumbani kakuta mkewe anamsubiri na malalamiko kuwa hana msaada nyumbani hata hela ya saluni hajaacha,ada ya mtoto hajalipa,bili kadhaa za nyumbani mkewe kamjaza hasira kuwa hata nyumbani kwao ameanza kudharaulika kwa kumfananisha na wanaume wengine walio waoa dada zake shemeji zake wengine kuwa yeye ametia aibu na maneno mengine ...ya KUMJAZA HASIRA.
mwanzoni alijitahidi kubadilisha maongezi alihitaji kusali na kupumzika tu alijitahidi kunyamaza na kubadilisha stori..mkewe aliendelea kumoigia kelele kuanzia saa 4 usiku mpaka saa sita usiku na robo...jamaa alihitaji kula na kupumzika tu kulala kwa amani na kusali..lakini uvumilivu ukamshinda ...AKALIPUKA HASIRA akafungua mlango na kuanza kutoka nje ....mkewe na watoto wakawa wanamvuta asiondoke usiku abaki nyimbani huku wanalia ...akawasukumu akaondoka usiku huo...na hajui anakoenda anenda popote atakapokuwa ili mradi apate sehemu ya kutuliza mawazo yake mbali na makelele.
Bila kujua kuwa sisi ndio tunaosababisha hayo yote ni kazi yetu ya nguvu za giza.
HAPA ALIFANYA MAKOSA WAWILI kwa pomoja yanayozidi kubomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwake.
1)KUONDOKA eneo la nyimbani kwake USIKU kuanzia saa6
2)AKIWA AMEJAA HASIRA.
kufupisha tulimsukumia roho ya ulevi...tulianza kidogo kidogo .kumuwekea burudani kidogo kwenye pombe na kuona kwamba pombe ndio inayomuondolea matatizo
baadae tukamuwekea URAIBU na utegemezi wa pombe...akawa mlevi sugu ..
NDOA ikavunjika baadae wakapeana talaka mke akarudi kwao na watoto.
baadae maisha ya IMANI yakashuka akaacha kusali.
mwanzo alikunywa pombe kwa siri kwa kujificha baadae kakawa mlevi sugu...
akageuka aibu mfano mbaya ..kwa jamii.
Mwisho wa siku ..so sad RIP.
IAMBIE MIFUPA MIKAVU ILIYOKUFA KATIKA MAISHA YAKO IFUFUKE(Ezekieli 37 1-15)
Toa unabii juu ya mifupa hii. Iambie hivi: Enyi mifupa mikavu, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu. Bwana Mwenyezi-Mungu awaambia hivi: Nitaifanya pumzi iwaingie, nanyi mtaishi.
CHUKUA HATUA HII
Tambua eneo lolote katika maisha yako ambalo limekufa ambalo ndio kiunabii linaitwa mifupa mikavu lisemeshe maneno ya ezekieli 37 ;1-15
sema hivi wewe NDOA YANGU-mifupa mikavu taja eneo husika katika ndoa kama ni (mawasiliano hamzungumzi/mawasiliano hakuna,upendo umepote,n.k) sema nakutolea unabii,sikia neno la Mungu nitafanya pumzi ya Mungu ikuingie nawe utaishi, fanya hivyo kila siku asubuhi unapoamka na jioni unapolala kwa muda wa siku 21 mpaka 30...utanishukuru baadae.
maeneo yote yenye mifupa mikavu yaliyokufa kwenye maisha yako,iwe ni uchumi wako eneo lako la kazi ,AFYA YAKO n.k
JENGA UPYA UKINGO WA UKUTA WA ULINZI WA MUNGU ULIOBOMOKA(Ezekieli 22:30*
Ezekieli 22:30
Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, *na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka", kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.
tambua mambo yaliyobomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwako.
kama ni laana za ukoo
tamka maneno haya
BWANA MUNGU nasimama mbele yako kama kwa ajili ya familia yangu ukoo wangu kuziba pale walipobomoa kwa maagano ya ukoo ya damu za ukoo,naziba pale mababu zangu walipopabomoa ,uharibifu hautatupata familia yengu.
tamka maneno hayo kila siku mfululizo.
NB NI MUHIMU kutamka kila siku mfululizo bila kuruka hata siku moja kwa muda wa siku kuanzia 21-30..kadiri unavyotamka kila siku kwa uaminifu na imani,kwa ujasiri utapata matokeo.
siku nyingine nitongelea kuhusu roho fuatilizi zinazofuatilia maisha yako bila wewe kujijua nyumbani kwako ni kama kamera inayomulika
maisha yako kirioho ,kiuchumi adui anajua kuwa siku tatu zijazo au wiki moja mbele utapata mafanikio kwenye eneo fulani au utapata pesa hivyo nazuia hizo baraka zisikufikie ndio maana hata ukikaribia kupata hela mkono unawasha..ina maana yake..
vioo glass vitu vyote vya vioo hata hii simu,madirisha ya kioo,na vioo vya kabati za chumbani na dressing table pembeni ya kitanda chako,wanyama na ndege kama mijusi,paka,n.k
cha kufanya takasa kwa mafuta vioo vyako visitumike kuchunguza maisha yako kupeleka taarifa ulimwengu wa giza .
kama huwa unajisikia kama kuna mtu anakuangali rohoni unajihisi kama kuna mtu mahali anakuona kwenye television yake...(wengi watapuuza haya ni chakula cha kiroho cha watu wazima waliokomaa kiroho .sio watoto wanaonyonya maziwa ..watakuja kupinga..ila roho mtakatifu atusaidie kutambua MBINU ZOTE ZA ADUI ANAZOTUMIA tupate maarifa..
Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa