Mifupa mikavu

Mifupa mikavu

a sinner saved by Christ

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
2,813
Reaction score
2,992
KILA MTOTO WA MUNGU ANAYEMCHA MUNGU (ana ulinzi wa UKINGO/UKUTA kutoka kwa Mungu unaomzingira pande zote yeye pamoja na mali zake kama mtumishi wa Ayubu)

Ayubu 1:10
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Lakini adui yetu,mshitaki wetu shetani huzunguka kama simba aungurumaye akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8) na huyu adui yetu kazi yake ni kuiba,kuchinja na kuharibu(yohana 10:10)

Wakati mwingine huyu adui yetu anaua na kuiba vitu vyako vya ndani kama NDOA yako,UCHUMI wako,IMANI yako au hata afya yako hata kama kwa nje unaonekana upo sawa ,ila kwa ndani ameshakumaliza unabaki kama kasha tupu,kopo tu kwa nje zuri ndani halina kitu.

SIFA YA VITU VYAKO VYA NDANI VILIVYOKUFA
NDOA iliyokufa ndani...wanandoa hawazungumzi pamoja ,tena wanaweza wakaishi kila mmoja na chumba chake,upendo wao unapoa unafutika kabisa,wanachukiana ,wanalaumiana kila mmoja ana mshutumu mwenzake mbaya,kupigizana makelele.

UCHUMI uliokufa...umasikini..kufikisika,pesa kupotea,kufunga kwa milango ya fursa za biashara na uchumi zilizokuwa wazi mwanzo,kupata pesa kwa shida kazi kubwa kama tembo mapato kiduchu kama panya,na hata ukipata matumizi mengi yanaibuka kuimaliza,madeni makubwa kuliko uwezo wako,wale watu waliokuwa wanakusapoti kwa fursa za kiuchumi kujitenga mbali,kila jitihada za kujikwamua kiuchumi zinafeli

AFYA..magonjwa yasiyo isha maradhi kuugua mara kwa mara..maradhi sugu

FANI YAKO NA UJUZI
Kudumaa hata kama una ujuzi hupigi hatua wala hupati fursa,haunufaiki kwa kiwango stahili na fani yako na hupigi hatua unadumaa.

TABIA ZINAZOPELEKEA KUPASUKA/KUVUNJIKA NYUFA KATIKA KUTA/UKINGO WA ULINZI WA MUNGU..unaokuzingira mtoto wa Mungu.
Ukuta/ukingo ulinzi wako kutoka kwa Mungu hupasuka na kuweka uwazi pale mtoto wa Mungu anapofanya mambo yafuatayo.

1)DHAMBI ZISIZOTUBIWA/kutokutubu dhambi zetu haraka kwa wakati mapema sana .
Dhambi zisizotubiwa zinabomoa ukuta..(dhambi zenu ndio zina achilia mauti ,ndio zinawatenga na Mungu hata asiweze kusikia,hata sadaka za mtu mwovu ni chukizo.
Ni lazima kuishi maisha ya TOBA kila wakati TUBU DHAMBI kila mara ,mtakatifu na azido kutakaswa..

2)LAANA ZA UKOO
wazazi wetu mababu na mabibi walitenda dhambi kabla yetu hata kabla hatupo ila maovu yao tunapatilizwa yametupata sisi hata kizazi cha tatu na cha nne,unakuta walitambikia MIZIMU,waganga wa kienyeji,wakaweka maagano kwa mizimu ,na majini ya ukoo yakatumiliki sisi na vizazi vyetu vijavyo..

3)KUTOKUSAMEHE watu,vinyongo kuweka vinyongo visasi moyoni

4)HASIRA CHUKI

5)MANENO YAKO mwenyewe ukijilaani mwewe bila kujua ,mfano unakuta mtu anajilaani mwenyewe bila kujua mfano anasema ,MIMI huu naona lazima nitakufa tu sitapona,au mimi ni wa kupata hasara tu,mimi siwezi,mimi sina uwezo,sina akili,kwetu wote huwa tuna ugonjwa wetu,kwetu hatuoi,..mimi ni masikini..n.k..UMENASWA kwa maneno ya kinywa chako mwwnyewe usijinenee mabaya

5)Uzinzi,ulevi n.k yani dhambi zote zinaingia kwenye point namba moja ya dhambi,lakini hapa nakuongezea point moja ambayo ulikuwa huijui...KUZURURA USIKU WA MANANE MBALI NA NYUMBANI KWAKO...mfano kuanzia saa sita usiku ukiwapo nyumbani kwako kuna ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu unaokulinda.

hapa nitoe mfano kabisa

kuna mtumishi wa Mungu tulikuwa tunamfuatilia kwa muda wa miaka miwili kupitia roho fuatilizi hapa tulitumia KIOO vitu vyote vya kioo kama vioo vya makabati ya nguo hasa vioo vinavyowekwa vyumba vya kulala vikitazama kitanda chako.(ni kama cctv kamera )

alikuwa mtumishi wa Mungu mtakatifu sana kwa muda wa miaka miwili ya kumfuatilia hatukuweza kumuangusha,alitumika kanisani kuhubiri,kufundisha vijana habari za ndoa akiwa na ndoa nzuri yenye upendo furaha na amani na familia yake.
Mtu wa maombi sana...yani mlokole kweli kweli..toa sadaka hakosi ibada ..na watu wote walimuona kama mfano wa kuigwa na mshauri wa watu..katika masuala ya kiroho na ndoa

tatizo lake lilikuwa moja tu ...*HASIRA KALI INAYOLIPUKA KAMA MOTO WA PETROLI"

ukuta wake ukingo wa Mungu ukaweka mwanya ukapasuka kwa hasira zake za mara kwa mara..

tukaanza kumshambulia kiroho..kidogo kidogo .hasira yake tukaiongeza mara dufu..tukaachilia roho ya umasikini..akaanza kupata changamoto za kiuchumi..tukaanza kumshambulia na mke wake..kumuwekea roho ya malalamiko/lawama

siku moja ametoka kazini amechoka na huko kazini bosi wake kamfokea sana kutokana na sisi kumuharibia hata kazini kwake kila anachofanya kinaonekana kibaya hata kazini..alipofika nyumbani kakuta mkewe anamsubiri na malalamiko kuwa hana msaada nyumbani hata hela ya saluni hajaacha,ada ya mtoto hajalipa,bili kadhaa za nyumbani mkewe kamjaza hasira kuwa hata nyumbani kwao ameanza kudharaulika kwa kumfananisha na wanaume wengine walio waoa dada zake shemeji zake wengine kuwa yeye ametia aibu na maneno mengine ...ya KUMJAZA HASIRA.

mwanzoni alijitahidi kubadilisha maongezi alihitaji kusali na kupumzika tu alijitahidi kunyamaza na kubadilisha stori..mkewe aliendelea kumoigia kelele kuanzia saa 4 usiku mpaka saa sita usiku na robo...jamaa alihitaji kula na kupumzika tu kulala kwa amani na kusali..lakini uvumilivu ukamshinda ...AKALIPUKA HASIRA akafungua mlango na kuanza kutoka nje ....mkewe na watoto wakawa wanamvuta asiondoke usiku abaki nyimbani huku wanalia ...akawasukumu akaondoka usiku huo...na hajui anakoenda anenda popote atakapokuwa ili mradi apate sehemu ya kutuliza mawazo yake mbali na makelele.

Bila kujua kuwa sisi ndio tunaosababisha hayo yote ni kazi yetu ya nguvu za giza.

HAPA ALIFANYA MAKOSA WAWILI kwa pomoja yanayozidi kubomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwake.
1)KUONDOKA eneo la nyimbani kwake USIKU kuanzia saa6
2)AKIWA AMEJAA HASIRA.

kufupisha tulimsukumia roho ya ulevi...tulianza kidogo kidogo .kumuwekea burudani kidogo kwenye pombe na kuona kwamba pombe ndio inayomuondolea matatizo
baadae tukamuwekea URAIBU na utegemezi wa pombe...akawa mlevi sugu ..

NDOA ikavunjika baadae wakapeana talaka mke akarudi kwao na watoto.

baadae maisha ya IMANI yakashuka akaacha kusali.
mwanzo alikunywa pombe kwa siri kwa kujificha baadae kakawa mlevi sugu...

akageuka aibu mfano mbaya ..kwa jamii.

Mwisho wa siku ..so sad RIP.

IAMBIE MIFUPA MIKAVU ILIYOKUFA KATIKA MAISHA YAKO IFUFUKE(Ezekieli 37 1-15)
Toa unabii juu ya mifupa hii. Iambie hivi: Enyi mifupa mikavu, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu. Bwana Mwenyezi-Mungu awaambia hivi: Nitaifanya pumzi iwaingie, nanyi mtaishi.

CHUKUA HATUA HII
Tambua eneo lolote katika maisha yako ambalo limekufa ambalo ndio kiunabii linaitwa mifupa mikavu lisemeshe maneno ya ezekieli 37 ;1-15

sema hivi wewe NDOA YANGU-mifupa mikavu taja eneo husika katika ndoa kama ni (mawasiliano hamzungumzi/mawasiliano hakuna,upendo umepote,n.k) sema nakutolea unabii,sikia neno la Mungu nitafanya pumzi ya Mungu ikuingie nawe utaishi, fanya hivyo kila siku asubuhi unapoamka na jioni unapolala kwa muda wa siku 21 mpaka 30...utanishukuru baadae.

maeneo yote yenye mifupa mikavu yaliyokufa kwenye maisha yako,iwe ni uchumi wako eneo lako la kazi ,AFYA YAKO n.k

JENGA UPYA UKINGO WA UKUTA WA ULINZI WA MUNGU ULIOBOMOKA(Ezekieli 22:30*
Ezekieli 22:30

Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, *na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka", kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.

tambua mambo yaliyobomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwako.

kama ni laana za ukoo

tamka maneno haya

BWANA MUNGU nasimama mbele yako kama kwa ajili ya familia yangu ukoo wangu kuziba pale walipobomoa kwa maagano ya ukoo ya damu za ukoo,naziba pale mababu zangu walipopabomoa ,uharibifu hautatupata familia yengu.

tamka maneno hayo kila siku mfululizo.
NB NI MUHIMU kutamka kila siku mfululizo bila kuruka hata siku moja kwa muda wa siku kuanzia 21-30..kadiri unavyotamka kila siku kwa uaminifu na imani,kwa ujasiri utapata matokeo.

siku nyingine nitongelea kuhusu roho fuatilizi zinazofuatilia maisha yako bila wewe kujijua nyumbani kwako ni kama kamera inayomulika
maisha yako kirioho ,kiuchumi adui anajua kuwa siku tatu zijazo au wiki moja mbele utapata mafanikio kwenye eneo fulani au utapata pesa hivyo nazuia hizo baraka zisikufikie ndio maana hata ukikaribia kupata hela mkono unawasha..ina maana yake..

vioo glass vitu vyote vya vioo hata hii simu,madirisha ya kioo,na vioo vya kabati za chumbani na dressing table pembeni ya kitanda chako,wanyama na ndege kama mijusi,paka,n.k

cha kufanya takasa kwa mafuta vioo vyako visitumike kuchunguza maisha yako kupeleka taarifa ulimwengu wa giza .

kama huwa unajisikia kama kuna mtu anakuangali rohoni unajihisi kama kuna mtu mahali anakuona kwenye television yake...(wengi watapuuza haya ni chakula cha kiroho cha watu wazima waliokomaa kiroho .sio watoto wanaonyonya maziwa ..watakuja kupinga..ila roho mtakatifu atusaidie kutambua MBINU ZOTE ZA ADUI ANAZOTUMIA tupate maarifa..

Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa
 
.
 

Attachments

  • Screenshot_20260507-234925.jpg
    Screenshot_20260507-234925.jpg
    94.3 KB · Views: 5
SWALI
Kila nikipata kazi naota nanyanganwa handbag alafu baada ya apo sipati kazi tena.


JIBU
kuna (monitoring spirits)* zinazofuatilia maisha yako zinazopeleka taarifa katika ulimwengu wa giza pale unapokaribia breakthrough then unakuwa attaked by blocking your blessings/wanazuia baraka zako.

kawaida sisi watoto wa Mungu tunaomcha na kumtumaini yeye,Mungu huwa tuna ulizi wa ukingo/kuta ya Mungu kuzuia adui asikushambulie ,kama ule alikuwa nao Ayubu.

lakini ukuta huo unaweza kubomoka kwa njia mbali mbali ,ikiwemo dhambi isiyotubiwa,dhambi za ukoo,kutokusamehe vinyongo n.k

CHA KUFANYA
Omba toba na rehema kwa Mungu kisha tumia maneno haya
EZEKIEL 22:30
BWANA Mungu wangu nasimama mbele yako kuziba na kujenga mahali palipobomoka kwa makosa ya mababu zangu ancestors na laana za ukoo,
tumia na EZEKIEL (37 :1-15)
KIBALI CHAKO CHA KAZI kimekufa ,adui kazi yake ni kuchinja,kuharibu na kuiba.


semesha kibali chako cha kazi kilichokufa kikawa MIFUPA MIKAVU

sema wewe mifupa mikavu kazi yangu iliyokufa sikia neno la Mungu ,pumzi ya Mungu ikuingie,ukawe mzima.

tamka maneno hayo kwa imani,kila siku mfululizo ,kwa ujasiri kwa siku 21 mpaka 30

Kazi yako itafufuka(MIFUPA MIKAVU ITAFUFUKA NA KUWA HAI TENA) kwa jina la Yesu.
 
SWALI
Mtu akiota anendaesha gari na ina abiria full lkn asimjue hata mmoja na jiani anapata trafiki lkn hawana shughuli na yy, barabara haina matuta lkn anaona n mzoevu hata iweje anaimudu gari vizuri, n ndoto ya vipi hio na mtu hajafiikiria kuwa PSV driver?

JIBU
dereva ni kiongozi /kuhani unayeongoza kondoo katika safari ya kwenda mbinguni.

kiongozi kuanzia ngazi ya familia/mzazi ni kuhani wa familia yake na ukoo wake na jamaa zake kuwaongoza katika safari ya kwenda mbinguni...kuwapeleka watu wamfikie Yesu ,uwaendeshe kuwafikisha kwa Yesu yeye Yesu ni njia ,kweli na uzima.
 
NAFUDIA TENA KUSEMA ILE CHANJO ITAKAYOKUJA IPO KARIBU CHANJO YA LAZIMA KWA WATU WOTE IPO KARIBU SANA KUJA...

Hiyo chanjo ni chapa CHAPA ...

MWANA WA MUNGU USICHANJE HIYO CHANJO.
Kama huamini unabii huu ,kaa vizuri na Roho mtakatifu...muulize Mungu wako..akufunulie akusemeshe hata katika ndoto...

USICHANJE HIYO CHANJO ITAKAYOKUJA UTAKUWA UMEPOKEA CHAPA...

zipo njia nyingi za kupokea chapa hiyo chanjo ni mojawapo.
japo zipo njia nyingine pia
 
Gal 5:19-21
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya,
1)uasherati
2)uchafu,
3)ufisadi,
4)ibada ya sanamu,
5)uchawi,
6)uadui,
7)ugomvi,
8)wivu,
9) hasira,
10)fitina,
11)faraka,
12)uzushi,
13)husuda,
14)ulevi,
15)ulafi,

na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kor 6:9-11
Au hamjui ya kuwa
1)wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu?

Msidanganyike;
2) waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu,
3) wala waabudu sanamu,
4) wala wazinzi,
5)wala wafiraji,
6)wala walawiti,
7)wala wevi,
8)wala watamanio,
9)wala walevi,
10) wala watukanaji,
11) wala wanyang’anyi.

Na baadhi yenu mlikuwa watu
wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Kol 3:5
Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi,
1)uasherati,
2)uchafu,
3)tamaa mbaya,
4)mawazo mabaya,
5)na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu

Ufu 21:8
1)Bali waoga,
2)na wasioamini,
3)na wachukizao,
4)na wauaji,
5)na wazinzi,
6)na wachawi,
7) na hao waabuduo sanamu,
8)na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo
moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.**
 
SWALI
Kaka naumia na hizo njozi za mapolice ni njozi inayojirudiarudia,
Police maana yake nini katika ulimwengu wa roho.

JIBU
Jeshi la mapolisi katika ndoto maana yake ni wachawi(washirikina,walozi,wanga)

bundiki na silaha zao ..ni makombora yao ya kichawi..

ukiota wamebeba bunduki bunduki au mabomu au mikuki ....ndio makombora yao kichawi...wanakurushia....mana yake wanakushambulia katika ulimwengu wa roho..
Zab 27:3
Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
CHA KUFANYA SASA..

Sali omba Mungu ,tumia damu ya Yesu..silaha yetu na nguvu zetu ni jina la Yesu na damu ya Yesu,na jeshi la malaika

ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo

isaya 54:17
zaburi 91:10-15
zaburi 35.
zaburi 18 na zaburi 19

jeshi la malaika walioko upande wetu ni wengi kuliko hao
wao watataja farasi ,wao watataja farasi lakini sisi tunakuja kwa kulitaja jina la Yesu.

Isa 41:10-13
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

USIOGOPE KABISA.
2 Kor 10:4
maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;

Usiogope kabisa ukiogopa tu unakosea unawafungulia mlango,vaa silaha za imani,tumia upanga wa neno...neno la Mungu ni silaha ,upanga mkali sana...fuatilia masomo na mafundisho yote niliyokutumia...

wachawi wanatakiwa wakuogope wewe na sio wewe uwaogope wachawi... kwa sababu wewe unamtumainia YESU BWANA WA MAJESHI...mfalme wa utukufu mwenye nguvu na utukufu..wewe ni mshundi tayari kupitia Yesu,wewe ni mwana wa Mungu mfalme ,sasa unaogopaje mapepo na wachawi,badala wao ndio waungue na kukukimbia si utumie silaha unazo ..OMBA tumia damu ya Yesu,jina la Yesu,kemea,tumia NENO ambaye huyo neno ndio Yesu

Ebr 4:12
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.


OMBA wewe mwenyewe kwa mdomo wako na kwa moyo wako..muombe Yesu kwa imani kwa kumaanisha kwa ujasiri.

hauhutaji kuombewa wala kutumia mafuta ya upako,wala kwenda popote hapo hapo ulipo Yesu yupo upo naye yupo karibu yako anakuona anakujua na anakusikia,ila ni lazima UOMBE.
 
Jinsi ufalme wa Mungu unavyofanya kazi ni mfano wa ufalme au serikali inayofuata SHERIA zilizo katika katiba katika kutoa hukumu A HAKI kifupi ni kama mfumo wa MAHAKAMA ya haki.

Mungu akiwa kama HAKIMU
(2 Wathesalonike 1:5
kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki



YESU malaika wa Mungu kama mtetezi wetu,wakili wetu(
Ayu 19:25
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai



SHETANI na mapepo wabaya ufalme wa giza pamoja na jeshi la wakuu wa anga giza wa,majini,wachawi hawa ni WASHITAKI wetu.
1 Pet 5:8-10
mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

SHEATANI ufalme wa giza mapepo wanaongea na Mungu pia katika kusikiliza hizi kesi juu ya wanadamu(USIFIKIRI shetani na Mungu hawaongei..Ayu 1:7
BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

kila siku shetani anapeleka mashitaka kuwashitaki watakatifu wa Mungu kila wanapokosea.

SHERIA ama KATIBA ZINAZOTUMIKA INAYOTUMIKA ni sheria za Mungu NENO LA MUNGU ama kitabu cha biblia BIBLIA hii ndio kama katiba ya milele inayouhukumu ulimwengu wote sasa na hata siku ya hukumu ya mwisho mbeleni future.Dunia na ulimwengu utapita lakini neno la Mungu litasimama halitapita..hakuna katiba mpya wala sheria mpya ni neno lile lile la Mungu litasimama BIBLIA TAKATIFU milele.

kutokujua sheria haikuondelei kosa hivyo ni vizuri tukajua sana sheria ya Mungu neno la Mungu ili tusije tukaangukia katika dhambi(NENO la Mungu tuliweke moyoni mwetu kwa wingi ili tisitende dhambi,kuijua sheria ya na katiba ya kitabu cha hukumu.

upande wa MASHITAKA(ufalme wa giza ,shetani ,mapepo ,wachawi)

Unafungua kesi za mashitaka kila dakika dhidi yetu pale tunapovunja sheria ya Mungu (KIUKA NENO LA BIBLIA NENO LA MUNGU) kwa kutumia ishahidi wa kisheria wa kimaandiko..

kitu cha kujua..KILA DHAMBI unayoifanya hata kwa SIRI DHAMBI ZA SIRI (za moyoni mwako) ufalme wa giza unazijua ,kitu cha kufahamu ukitenda dhambi tu ile dhambi inapiga kengele inapiga kelele au inaonekana kwenye kioo au television (HAKUNA DHAMBI YA SIRI ) utakayoifanya Shetani na mapepo wachawi wasijue au wasio one yani wewe ni kama KIOO kinachoangaza kuonyesha maisha yako ya dhambi na utakatifu wako kwa shetani na mapepo na wachawi na hata mbele za Mungu kila kitu unachofanya na hali yako ya kiroho ,kama ukiwa mtakatifu otaonekana wazi na kama umefanya dhambi sekunde hiyo hiyo itaonekana(wewe ni kama BARUA inayosomeka katika ulimwengu wa roho hakuna kilichojificha huwezi kumdanganya Mungu wala huwezi kumficha shetani,hata dhambi za moyoni mwako zinaonekana ,asiloweza kulijua sheteni kuhusu wewe ni mawazo yako unawaza nini ila pindi ikitenda dhambi tu INAREKODIWA video inaonekana kwwnye screen haijifichi.
INAKUWA USHAHIDI hata kama ni dhambi ya SIRI ya ndani ya moyo.

MASHITAKA anayotushtaki nayo shetani ni DHAMBI zetu kwa kuwa anazijua dhambi zetu na yeye shetani ndiyo baba wa uovu ndio kiongozi wa uovu na dhambi toka mwazo ndiye anayepeleka mashitaka mashitaka YANAPELEKWA KILA DAKIKA (umetenda dhambi shetani anafungua kesi kupeleka kwa Mungu kukushitaki KUKATA rufaa kupinga KUZUIA MAPINGAMIZI mahakama ya Mungu ILI kuzuia maombi yako ,yani ili Mungu asikubariki,asijibunmaombi yako ,na UPATE HUKUMU ya kuadhibiwa au mapepo wachawi shetani apate uhalali wa kukushambulia.

MAMBO YA KUFANYA KWAKO
1) Maisha ya TOBA tubu mara kwa mara,omba ROho mtakatifu akuonyeshe dhambi zote ulizofanya ndani ya siku nzima tokanimeanza na tubu haraka mapema kabla ya siku kuisha kabla hujalala usilale ukiwa hujatubu dhambi zako ulizofanya ambazo zimemuhuzinisha roho mtakatifu hata kama ni zile unazo ona ni dhambi ndogo ndogo na hata ulizozisahau au ambazo hukujua .(TOBA na kuomba kutakaswa)

2.SAMEHE WATU usiweke kinyongo kubeba watu moyoni kitokusamehe vinyongo,chuki na hasira hata kama aliyekukosea hajakuomba msamaha ama unahisi hastahili kusamehemwa msamehe kwa ajili ya faida yako mwwnyewe.

mfano..MKE alimfumania MUMEWE sasa akaweka kinyongo na kuyokusamehe ..kupitia hiyo dhambi ya kutokumsamehe mume wake aliyefanya dhambi ya uzinzi/uasherati ..inapelekea shetani kupata uhalali wa kisheria kukushambulia kwa sababu
atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo.na tena mshahara wa dhambi ni mauti na zaidi dhambi zetu zinatutenga na Mungu

KWA KIFUPI DHAMBI INAFUNGUA MLANGO wa kuruhusu shetani akushambulie zaidi.

tena atashambulia zaidi hiyo hiyo NDOA yako kwa kitendo cha wewe mwanamke kutokumsamehe tu mumeo kwa vile amefanya uzinifu/uasherati..Shetani atakusukumia maroho ya MAGOMVI,CHUKI HASIRA,na HATA KUVUNJA KUTENGANA kuvunja ndoa ,kabisa,na hata kudhuru familia na maisha ya kiroho na inada zako...

itambue mitego ya SHETAni ukitambua Silaha wanazotumia ulimwengu wa giza ukiwapeleleza siyo vibaya kujua ulimwengu wa giza unavyofanya kazi kuharibi kushambulia watu wa Mungu,hata JOSHUA alituma wapelelezi kuipeleleza maadui waliokuwa wanakalia nchi ya KAANANI..ukimjua adui yako utajua pia namna ya kupambana naye na silalaha anazotumia.

Mwanamke ukimsamehe mume wako ukaondoa kinyongo utaiponya ndoa yako na maisha yako ya kiroho wewe mwenyewe .

VINYONGO KUTOKUSAMEHE (unforgiveness,bitternes,na uzinzi/uasherati )ni moja ya mashitaka yanayopelekwa kutishitaki na kufungulia mlango wa kuingiza MAUTI katika maisha yetu...USIMPE SHETANI NAFASI ..usimruhusu usimfungulie mlango..huo ni mfano mmojawapo ipo mifano mingi ya vinyongo na kutokusamehe.

3)...TUMIA DAMU YA YESU katika hukumu DAMU ya YESU inatupa NEEMA yani kama ni kesi inalipa FAINI au DENI zetu au inafuta mashitaka kwa kulipa gharama ya tuliyostahili adhabu DAMU YA YESU inalipa in FULL..

sasa hata kama kesi ni kubwa kiasi gani,lakini hii neema ya damu ya Yesu siyo ya kuichezea yani kurudia rudia kufanya dhambi kwa makusudi kwa kuwakuwa kuna neema ya damu ya Yesu..BIG NO.!!!

Unapoanza siku funika siku yako kwa damu ya Yesu,akili zako nafsi yako,watito wako,nyumba yako ,jifunike kwa damu ya YESU na familia yako na kila jambo lako ,kazi yako,ndoa yako ,milango ,madirisha FUNIKA KWA DAMU YA YESU na usiku kabla ya kulala funika kwa damu ya Yesu.
Tunahesabiwa haki kwa kupitia Yesu mwenye haki,na kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumepona,Yesu amechukua dhambi zetu na adhabu yetu.

Ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo,



4)KUMSIFU MUNGU katikati ya mateso katikati ya shida na dhiki.
Mungu wetu anakaa katika sifa ,yani ni sawa na kukata rufaa kwenda kumfukia Mungu kwa njia ya sifa,na ile kumsifu Mungu ukiwa katikati ya mateso magumu unayopitia ni lugha unayo ongea kumwambia Mungu pamoja na haya magumu yote adui amenitendea amenifanyia ila bado wewe kwangu ni BWANA hii hi kumfikia Mungu anayekaa katika sifa.

Zaburi 22:3
Hata hivyo, wewe ni mtakatifu; wewe watawala na kusifiwa

yani ni sawa na kumwambia Mungu hata yanipate mabaya kiasi gani hata adui anitende mabaya kiasi gani hata nichinjwe shingo katika hali yeyote ile wewe Mungu kwangu ni yote katika vyote hata nikose vyote wewe Mungu kwangu unatosha ,ni sawa na kusema ,Mungu kwangu wewe ndio kila kitu,hakuna cha kunitenga na upendo na wema wa Mungu.

mfano mzuri ,PAULO NA SILO walipofungwa gerezani wakiwa wamegungwa minyororo katikati ya gereza waliomba,milango ya gereza na minyororo iliyowafunga ikafunguka..



Kamwe usije ukamlalamikia Mungu usimnungunikie Mungu hata kama unapitia shida usilalamike hata kama unapitia mateso makubwa kiasi gani ,wewe msifu Mungu ,wengi wamepokea uponyaji na wameona wanapoea majibu kupitia kumsifu Mungu katikati ya MATESO na majaribu makubwa waliyokuwa wanapiatia.

Mdo 16:25
Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza(Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.

minyororor maana yake ni vifungo vyote vya shetani vinavyokutesa na mashitaka yote ,usiangalie minyororo ya mwilini na milango ya jengo la gereza.

gereza ni mambo yako yaliyofungwa maeneo mbalimbali.


5)KUWAJALI WAHITAJI"

hii ni kusaidia wale wasiojiweza wanyonge ambao hutarajii wakulipe fadhila yoyote na wala sio kwa lengo la kupata sifa au kujioyesha,ni tofauti kusaidia watu waojiweza marafiki zako ukiwa na lengo kuna siku na wao watakulipa fadhila kama unawakopesha utakuja kulipwa.

Mit 19:17
Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

sasa hapa ukimsaidia masikini ni sawa na kumkopesha MUNGU mwenyewe na lazima atakulipa mema,hapa hata shetani aje na kesi yake kukushitaki unampiga knock out.

lakini mkono unaotoa ndio unaobariwa kuliko unaopokea,lakini ukiwapa watu vitu utapokea kwa kipimo cha Mungu kilichosukwa sukwa na kusindikiwa hata kumwagika.

lakini dini iliyo safi isiyo na taka ni kuwasaidia wahitaji,Yakobo 1:27
Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao,

zaidi ya yote ni hii

ZABURI YA 41
Heri amkumbukaye mnyonge;
BWANA atamwokoa siku ya taabu
.
2BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,

Naye atafanikiwa katika nchi;

Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake
.
3BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.
Katika ugonjwa wake unamponya maradhi yake.

(wanaojua siri hii utawakuta wanatoa sana misaada kwa masikini na wahitaji,ni vizuri tuwe na maarifa mbona wana wa giza wana maarifa sana katika kututenda maovu,na sisi tuwe na maarifa ya KIROHO)

6)KUTII SHERIA/NENO YA MUNGU
Submissive kutii hata kile ambacho unaona kinakunyima starehe ama raha ya mwili au hata kama kinaonekana kinafurahisha mwili.

mfano..mfanyakazi mkoja wa taasisi moja alipata JARIBU mtihani ,boss wake alimlazimisha afanye kughushi udanganyifu ofisini kwake ili waweze kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ..lakini yeye alisimama akisema hiki kiti ni siwezi kufanya kwa sababu ni dhambi kwa Mungu ni bora kama ni kazi nipoteza kazi lakini sipo tayari kufanya dhambi ya udanganyifu na wizi ,..mwisho wa siku yule bosi alietaka kumfukuza kazi kwa kukataa kutii agizo la kufanya udanganyifu wa wizi wa kalamu,kukipatia pesa alifukuzwa kazi yeye na yule aliyelinda uaminifu mbele za Mungu alipandishwa cheo.

Meshacj ,shedrak Abednego walikataa kuabudu sabamu ya nebukadreza wakatupwa kwenye tanuru la moto ila Mungu akawaoko kwa kuwatumia malaika hata kwwnye tundu la simba.

Zab 1:2-3
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.

Zab 119:
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

huyu DAUDI aliyeandika zaburi hata moyoni mwake anasema hana kiburi,na hata kutubu dhambi alikuwa mwepesi kutubu dhambi kwa haraka mara kwa mara.

ndiyo maana alimpendeza Mungu.

so utii ni bora kuliko dhabifu yani kumtii Mungu ni bora zaidi kuliko.

kwa maana ya kusikia na kuyafanya mapenzo ya Mungu.

YESU ANAKUPENDA Isa 53:5

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,

Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
 
Back
Top Bottom