Mifupa mikavu

Mifupa mikavu

a sinner saved by Christ

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
2,428
Reaction score
2,609
KILA MTOTO WA MUNGU ANAYEMCHA MUNGU (ana ulinzi wa UKINGO/UKUTA kutoka kwa Mungu unaomzingira pande zote yeye pamoja na mali zake kama mtumishi wa Ayubu)

Ayubu 1:10
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Lakini adui yetu,mshitaki wetu shetani huzunguka kama simba aungurumaye akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8) na huyu adui yetu kazi yake ni kuiba,kuchinja na kuharibu(yohana 10:10)

Wakati mwingine huyu adui yetu anaua na kuiba vitu vyako vya ndani kama NDOA yako,UCHUMI wako,IMANI yako au hata afya yako hata kama kwa nje unaonekana upo sawa ,ila kwa ndani ameshakumaliza unabaki kama kasha tupu,kopo tu kwa nje zuri ndani halina kitu.

SIFA YA VITU VYAKO VYA NDANI VILIVYOKUFA
NDOA iliyokufa ndani...wanandoa hawazungumzi pamoja ,tena wanaweza wakaishi kila mmoja na chumba chake,upendo wao unapoa unafutika kabisa,wanachukiana ,wanalaumiana kila mmoja ana mshutumu mwenzake mbaya,kupigizana makelele.

UCHUMI uliokufa...umasikini..kufikisika,pesa kupotea,kufunga kwa milango ya fursa za biashara na uchumi zilizokuwa wazi mwanzo,kupata pesa kwa shida kazi kubwa kama tembo mapato kiduchu kama panya,na hata ukipata matumizi mengi yanaibuka kuimaliza,madeni makubwa kuliko uwezo wako,wale watu waliokuwa wanakusapoti kwa fursa za kiuchumi kujitenga mbali,kila jitihada za kujikwamua kiuchumi zinafeli

AFYA..magonjwa yasiyo isha maradhi kuugua mara kwa mara..maradhi sugu

FANI YAKO NA UJUZI
Kudumaa hata kama una ujuzi hupigi hatua wala hupati fursa,haunufaiki kwa kiwango stahili na fani yako na hupigi hatua unadumaa.

TABIA ZINAZOPELEKEA KUPASUKA/KUVUNJIKA NYUFA KATIKA KUTA/UKINGO WA ULINZI WA MUNGU..unaokuzingira mtoto wa Mungu.
Ukuta/ukingo ulinzi wako kutoka kwa Mungu hupasuka na kuweka uwazi pale mtoto wa Mungu anapofanya mambo yafuatayo.

1)DHAMBI ZISIZOTUBIWA/kutokutubu dhambi zetu haraka kwa wakati mapema sana .
Dhambi zisizotubiwa zinabomoa ukuta..(dhambi zenu ndio zina achilia mauti ,ndio zinawatenga na Mungu hata asiweze kusikia,hata sadaka za mtu mwovu ni chukizo.
Ni lazima kuishi maisha ya TOBA kila wakati TUBU DHAMBI kila mara ,mtakatifu na azido kutakaswa..

2)LAANA ZA UKOO
wazazi wetu mababu na mabibi walitenda dhambi kabla yetu hata kabla hatupo ila maovu yao tunapatilizwa yametupata sisi hata kizazi cha tatu na cha nne,unakuta walitambikia MIZIMU,waganga wa kienyeji,wakaweka maagano kwa mizimu ,na majini ya ukoo yakatumiliki sisi na vizazi vyetu vijavyo..

3)KUTOKUSAMEHE watu,vinyongo kuweka vinyongo visasi moyoni

4)HASIRA CHUKI

5)MANENO YAKO mwenyewe ukijilaani mwewe bila kujua ,mfano unakuta mtu anajilaani mwenyewe bila kujua mfano anasema ,MIMI huu naona lazima nitakufa tu sitapona,au mimi ni wa kupata hasara tu,mimi siwezi,mimi sina uwezo,sina akili,kwetu wote huwa tuna ugonjwa wetu,kwetu hatuoi,..mimi ni masikini..n.k..UMENASWA kwa maneno ya kinywa chako mwwnyewe usijinenee mabaya

5)Uzinzi,ulevi n.k yani dhambi zote zinaingia kwenye point namba moja ya dhambi,lakini hapa nakuongezea point moja ambayo ulikuwa huijui...KUZURURA USIKU WA MANANE MBALI NA NYUMBANI KWAKO...mfano kuanzia saa sita usiku ukiwapo nyumbani kwako kuna ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu unaokulinda.

hapa nitoe mfano kabisa

kuna mtumishi wa Mungu tulikuwa tunamfuatilia kwa muda wa miaka miwili kupitia roho fuatilizi hapa tulitumia KIOO vitu vyote vya kioo kama vioo vya makabati ya nguo hasa vioo vinavyowekwa vyumba vya kulala vikitazama kitanda chako.(ni kama cctv kamera )

alikuwa mtumishi wa Mungu mtakatifu sana kwa muda wa miaka miwili ya kumfuatilia hatukuweza kumuangusha,alitumika kanisani kuhubiri,kufundisha vijana habari za ndoa akiwa na ndoa nzuri yenye upendo furaha na amani na familia yake.
Mtu wa maombi sana...yani mlokole kweli kweli..toa sadaka hakosi ibada ..na watu wote walimuona kama mfano wa kuigwa na mshauri wa watu..katika masuala ya kiroho na ndoa

tatizo lake lilikuwa moja tu ...*HASIRA KALI INAYOLIPUKA KAMA MOTO WA PETROLI"

ukuta wake ukingo wa Mungu ukaweka mwanya ukapasuka kwa hasira zake za mara kwa mara..

tukaanza kumshambulia kiroho..kidogo kidogo .hasira yake tukaiongeza mara dufu..tukaachilia roho ya umasikini..akaanza kupata changamoto za kiuchumi..tukaanza kumshambulia na mke wake..kumuwekea roho ya malalamiko/lawama

siku moja ametoka kazini amechoka na huko kazini bosi wake kamfokea sana kutokana na sisi kumuharibia hata kazini kwake kila anachofanya kinaonekana kibaya hata kazini..alipofika nyumbani kakuta mkewe anamsubiri na malalamiko kuwa hana msaada nyumbani hata hela ya saluni hajaacha,ada ya mtoto hajalipa,bili kadhaa za nyumbani mkewe kamjaza hasira kuwa hata nyumbani kwao ameanza kudharaulika kwa kumfananisha na wanaume wengine walio waoa dada zake shemeji zake wengine kuwa yeye ametia aibu na maneno mengine ...ya KUMJAZA HASIRA.

mwanzoni alijitahidi kubadilisha maongezi alihitaji kusali na kupumzika tu alijitahidi kunyamaza na kubadilisha stori..mkewe aliendelea kumoigia kelele kuanzia saa 4 usiku mpaka saa sita usiku na robo...jamaa alihitaji kula na kupumzika tu kulala kwa amani na kusali..lakini uvumilivu ukamshinda ...AKALIPUKA HASIRA akafungua mlango na kuanza kutoka nje ....mkewe na watoto wakawa wanamvuta asiondoke usiku abaki nyimbani huku wanalia ...akawasukumu akaondoka usiku huo...na hajui anakoenda anenda popote atakapokuwa ili mradi apate sehemu ya kutuliza mawazo yake mbali na makelele.

Bila kujua kuwa sisi ndio tunaosababisha hayo yote ni kazi yetu ya nguvu za giza.

HAPA ALIFANYA MAKOSA WAWILI kwa pomoja yanayozidi kubomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwake.
1)KUONDOKA eneo la nyimbani kwake USIKU kuanzia saa6
2)AKIWA AMEJAA HASIRA.

kufupisha tulimsukumia roho ya ulevi...tulianza kidogo kidogo .kumuwekea burudani kidogo kwenye pombe na kuona kwamba pombe ndio inayomuondolea matatizo
baadae tukamuwekea URAIBU na utegemezi wa pombe...akawa mlevi sugu ..

NDOA ikavunjika baadae wakapeana talaka mke akarudi kwao na watoto.

baadae maisha ya IMANI yakashuka akaacha kusali.
mwanzo alikunywa pombe kwa siri kwa kujificha baadae kakawa mlevi sugu...

akageuka aibu mfano mbaya ..kwa jamii.

Mwisho wa siku ..so sad RIP.

IAMBIE MIFUPA MIKAVU ILIYOKUFA KATIKA MAISHA YAKO IFUFUKE(Ezekieli 37 1-15)
Toa unabii juu ya mifupa hii. Iambie hivi: Enyi mifupa mikavu, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu. Bwana Mwenyezi-Mungu awaambia hivi: Nitaifanya pumzi iwaingie, nanyi mtaishi.

CHUKUA HATUA HII
Tambua eneo lolote katika maisha yako ambalo limekufa ambalo ndio kiunabii linaitwa mifupa mikavu lisemeshe maneno ya ezekieli 37 ;1-15

sema hivi wewe NDOA YANGU-mifupa mikavu taja eneo husika katika ndoa kama ni (mawasiliano hamzungumzi/mawasiliano hakuna,upendo umepote,n.k) sema nakutolea unabii,sikia neno la Mungu nitafanya pumzi ya Mungu ikuingie nawe utaishi, fanya hivyo kila siku asubuhi unapoamka na jioni unapolala kwa muda wa siku 21 mpaka 30...utanishukuru baadae.

maeneo yote yenye mifupa mikavu yaliyokufa kwenye maisha yako,iwe ni uchumi wako eneo lako la kazi ,AFYA YAKO n.k

JENGA UPYA UKINGO WA UKUTA WA ULINZI WA MUNGU ULIOBOMOKA(Ezekieli 22:30*
Ezekieli 22:30

Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, *na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka", kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.

tambua mambo yaliyobomoa ukingo wa ukuta wa ulinzi wa Mungu kwako.

kama ni laana za ukoo

tamka maneno haya

BWANA MUNGU nasimama mbele yako kama kwa ajili ya familia yangu ukoo wangu kuziba pale walipobomoa kwa maagano ya ukoo ya damu za ukoo,naziba pale mababu zangu walipopabomoa ,uharibifu hautatupata familia yengu.

tamka maneno hayo kila siku mfululizo.
NB NI MUHIMU kutamka kila siku mfululizo bila kuruka hata siku moja kwa muda wa siku kuanzia 21-30..kadiri unavyotamka kila siku kwa uaminifu na imani,kwa ujasiri utapata matokeo.

siku nyingine nitongelea kuhusu roho fuatilizi zinazofuatilia maisha yako bila wewe kujijua nyumbani kwako ni kama kamera inayomulika
maisha yako kirioho ,kiuchumi adui anajua kuwa siku tatu zijazo au wiki moja mbele utapata mafanikio kwenye eneo fulani au utapata pesa hivyo nazuia hizo baraka zisikufikie ndio maana hata ukikaribia kupata hela mkono unawasha..ina maana yake..

vioo glass vitu vyote vya vioo hata hii simu,madirisha ya kioo,na vioo vya kabati za chumbani na dressing table pembeni ya kitanda chako,wanyama na ndege kama mijusi,paka,n.k

cha kufanya takasa kwa mafuta vioo vyako visitumike kuchunguza maisha yako kupeleka taarifa ulimwengu wa giza .

kama huwa unajisikia kama kuna mtu anakuangali rohoni unajihisi kama kuna mtu mahali anakuona kwenye television yake...(wengi watapuuza haya ni chakula cha kiroho cha watu wazima waliokomaa kiroho .sio watoto wanaonyonya maziwa ..watakuja kupinga..ila roho mtakatifu atusaidie kutambua MBINU ZOTE ZA ADUI ANAZOTUMIA tupate maarifa..

Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa
 
.
 

Attachments

  • Screenshot_20260507-234925.jpg
    Screenshot_20260507-234925.jpg
    94.3 KB · Views: 2
SWALI
Kila nikipata kazi naota nanyanganwa handbag alafu baada ya apo sipati kazi tena.


JIBU
kuna (monitoring spirits)* zinazofuatilia maisha yako zinazopeleka taarifa katika ulimwengu wa giza pale unapokaribia breakthrough then unakuwa attaked by blocking your blessings/wanazuia baraka zako.

kawaida sisi watoto wa Mungu tunaomcha na kumtumaini yeye,Mungu huwa tuna ulizi wa ukingo/kuta ya Mungu kuzuia adui asikushambulie ,kama ule alikuwa nao Ayubu.

lakini ukuta huo unaweza kubomoka kwa njia mbali mbali ,ikiwemo dhambi isiyotubiwa,dhambi za ukoo,kutokusamehe vinyongo n.k

CHA KUFANYA
Omba toba na rehema kwa Mungu kisha tumia maneno haya
EZEKIEL 22:30
BWANA Mungu wangu nasimama mbele yako kuziba na kujenga mahali palipobomoka kwa makosa ya mababu zangu ancestors na laana za ukoo,
tumia na EZEKIEL (37 :1-15)
KIBALI CHAKO CHA KAZI kimekufa ,adui kazi yake ni kuchinja,kuharibu na kuiba.


semesha kibali chako cha kazi kilichokufa kikawa MIFUPA MIKAVU

sema wewe mifupa mikavu kazi yangu iliyokufa sikia neno la Mungu ,pumzi ya Mungu ikuingie,ukawe mzima.

tamka maneno hayo kwa imani,kila siku mfululizo ,kwa ujasiri kwa siku 21 mpaka 30

Kazi yako itafufuka(MIFUPA MIKAVU ITAFUFUKA NA KUWA HAI TENA) kwa jina la Yesu.
 
SWALI
Mtu akiota anendaesha gari na ina abiria full lkn asimjue hata mmoja na jiani anapata trafiki lkn hawana shughuli na yy, barabara haina matuta lkn anaona n mzoevu hata iweje anaimudu gari vizuri, n ndoto ya vipi hio na mtu hajafiikiria kuwa PSV driver?

JIBU
dereva ni kiongozi /kuhani unayeongoza kondoo katika safari ya kwenda mbinguni.

kiongozi kuanzia ngazi ya familia/mzazi ni kuhani wa familia yake na ukoo wake na jamaa zake kuwaongoza katika safari ya kwenda mbinguni...kuwapeleka watu wamfikie Yesu ,uwaendeshe kuwafikisha kwa Yesu yeye Yesu ni njia ,kweli na uzima.
 
NAFUDIA TENA KUSEMA ILE CHANJO ITAKAYOKUJA IPO KARIBU CHANJO YA LAZIMA KWA WATU WOTE IPO KARIBU SANA KUJA...

Hiyo chanjo ni chapa CHAPA ...

MWANA WA MUNGU USICHANJE HIYO CHANJO.
Kama huamini unabii huu ,kaa vizuri na Roho mtakatifu...muulize Mungu wako..akufunulie akusemeshe hata katika ndoto...

USICHANJE HIYO CHANJO ITAKAYOKUJA UTAKUWA UMEPOKEA CHAPA...

zipo njia nyingi za kupokea chapa hiyo chanjo ni mojawapo.
japo zipo njia nyingine pia
 
Gal 5:19-21
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya,
1)uasherati
2)uchafu,
3)ufisadi,
4)ibada ya sanamu,
5)uchawi,
6)uadui,
7)ugomvi,
8)wivu,
9) hasira,
10)fitina,
11)faraka,
12)uzushi,
13)husuda,
14)ulevi,
15)ulafi,

na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kor 6:9-11
Au hamjui ya kuwa
1)wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu?

Msidanganyike;
2) waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu,
3) wala waabudu sanamu,
4) wala wazinzi,
5)wala wafiraji,
6)wala walawiti,
7)wala wevi,
8)wala watamanio,
9)wala walevi,
10) wala watukanaji,
11) wala wanyang’anyi.

Na baadhi yenu mlikuwa watu
wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Kol 3:5
Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi,
1)uasherati,
2)uchafu,
3)tamaa mbaya,
4)mawazo mabaya,
5)na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu

Ufu 21:8
1)Bali waoga,
2)na wasioamini,
3)na wachukizao,
4)na wauaji,
5)na wazinzi,
6)na wachawi,
7) na hao waabuduo sanamu,
8)na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo
moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.**
 
SWALI
Kaka naumia na hizo njozi za mapolice ni njozi inayojirudiarudia,
Police maana yake nini katika ulimwengu wa roho.

JIBU
Jeshi la mapolisi katika ndoto maana yake ni wachawi(washirikina,walozi,wanga)

bundiki na silaha zao ..ni makombora yao ya kichawi..

ukiota wamebeba bunduki bunduki au mabomu au mikuki ....ndio makombora yao kichawi...wanakurushia....mana yake wanakushambulia katika ulimwengu wa roho..
Zab 27:3
Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.
CHA KUFANYA SASA..

Sali omba Mungu ,tumia damu ya Yesu..silaha yetu na nguvu zetu ni jina la Yesu na damu ya Yesu,na jeshi la malaika

ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo

isaya 54:17
zaburi 91:10-15
zaburi 35.
zaburi 18 na zaburi 19

jeshi la malaika walioko upande wetu ni wengi kuliko hao
wao watataja farasi ,wao watataja farasi lakini sisi tunakuja kwa kulitaja jina la Yesu.

Isa 41:10-13
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

USIOGOPE KABISA.
2 Kor 10:4
maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;

Usiogope kabisa ukiogopa tu unakosea unawafungulia mlango,vaa silaha za imani,tumia upanga wa neno...neno la Mungu ni silaha ,upanga mkali sana...fuatilia masomo na mafundisho yote niliyokutumia...

wachawi wanatakiwa wakuogope wewe na sio wewe uwaogope wachawi... kwa sababu wewe unamtumainia YESU BWANA WA MAJESHI...mfalme wa utukufu mwenye nguvu na utukufu..wewe ni mshundi tayari kupitia Yesu,wewe ni mwana wa Mungu mfalme ,sasa unaogopaje mapepo na wachawi,badala wao ndio waungue na kukukimbia si utumie silaha unazo ..OMBA tumia damu ya Yesu,jina la Yesu,kemea,tumia NENO ambaye huyo neno ndio Yesu

Ebr 4:12
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.


OMBA wewe mwenyewe kwa mdomo wako na kwa moyo wako..muombe Yesu kwa imani kwa kumaanisha kwa ujasiri.

hauhutaji kuombewa wala kutumia mafuta ya upako,wala kwenda popote hapo hapo ulipo Yesu yupo upo naye yupo karibu yako anakuona anakujua na anakusikia,ila ni lazima UOMBE.
 
Back
Top Bottom