Nataka kumuhudumia mtoto peke yake

Nataka kumuhudumia mtoto peke yake

Sasa kumbe kuna mwanaume aliyekuzidi hela? Huyo ndo anamnawirisha, na kama sio yeye basi kuna mwingine.

Pole kwa maswahibu lakini, inaonekana ulilazimisha sana kuwa nae tangu mwanzo. Kama baadhi ya hayo yanayokuchukiza yalitokea kabla hujazaa nae basi ulifanya makosa kuzaa nae. We kama unampenda mtoto jitahidi kumjali bila kumuwaza mama yake, thamani yako haitoacha kuonekana kwa mtoto huko mbeleni.

nilimpenda sana ndo maana nilimvumilia nikajua akizaa atabadilika nikamshawishi adi akakubali kunzalia baada ya kuzaa mtoto akiwa na miaka miwili ndo kama akanambia moyo wake haunipendi basi nilichofanya nikamtishia kumuaribia kazi akanambia kama ni kazi haina tabu kesho yake akaandika barua ya kuacha kazi.

kibaya zaidi akahama na kwao na mtoto akaniandikia sms kwamba nisimtafute na mtoto atamlea mwenyewe. sijui huko yaliyompata nikashtuka ananishinikiza matunzo ya mtoto nikamwambia amlete nikae nae akapeleka shitaka ustawi wa jamii nikawasihi wanipe mtoto akagoma kwamba bado mdogo nikapewa bili ya matunzo nikaambiwa nitoe 500 kila mwezi natoa lakini nikikumbuka nahisi namfaidisha kwa maana jamaa nasikia amemtosa na kazi hana. kwa kweli kwa moyo mweupe namuombea shida zooooooote zimpate.
 
Aiseee kuna baadhi ya wanaume ni wabinafsi cjapata kusikia ila ndo naona. uyo mtoto hujamleta pekeako hudumia wote mpaka mwanao atakavofikia mda wa kumchukua then yanaisha. usiwe na roho ya korosho ivo.
 
Ha ha ha ha...kwa hiyo ana nawili sababu ya hela yako....
 
kaka kama kwel unatoa jero kwa mwez si sahih akanawir kwa hyo hela yako maana hata mafuta madogo aina ya laiz haitosh
mchkue mtoto umlee wew uone umhim wa mwanamke!
 
Usipanick bana. Mimi bado sijawa convinced kwamba eti mama anakula anamnyima mwanae, uzoefu wangu ni kwamba mama anajinyima anampa mwanae.

Ni kweli kabisa wa mama wa zamani walifanya hivyo na walijinyima kweli lakini nyie wa siku hiyo huruma hakuna. Imebaki historia tu. Labda exceptional cases. Lakini pia inawezekana wewe hujakutana nao ila ukweli ndo huo
 
Mkuu inabidi urudi nyuma kufikiria tena , kumbuka anamlea mwanao cha msingi unapotoa hiyo hela usiwaze kwamba yeye ndo mnufaika wa kwanza LA,mfikirie mwanao.
 
Daah, una roho nzito,!! Huenda huyo mama alikukosea bt bado ni mzaz mwenzio na ndo mlez wa mwanao
 
Ukisoma sheria ya nchi inahitaji matunzo kwa wotr mama na mtt. Kwa sbb mama hawezi kuhudumia mtt kama afya yake umezorota. For benefit of ur child the mother should b taken care of
 
pakaywatek

Lifikirie hili katika uwanja mpana zaidi, binafsi najua unachokiongelea lakini huna jinsi kwa asilimia mia moja kuweza kumzuia mzazi mwenzako asinufaike na pesa unayotoa

Inawezekana kabisa pengine ni mtu wa starehe sana hivyo kukosa muda wa kukaa na kumhudumia mtoto ipasavyo !!!INAUMA NA KUUMIZA MNO MOYO
Fanya hivi muwekee msichana wa kazi halafu jitahidi kununua vitu mwenyewe kuliko kutoa cash! Malezi ya namna hiyo yana changamoto zake nyingi tu

Msisahau kwamba watoto wana moments zao hawapendi kula. Mwanangu wa kumlea mwenyewe kuna kipindi alikonda mpk nikimwona machozi yananilenga namkumbatia tu. Hata ukimpa chakula apendacho anakula kijiko kimoja anaenda kucheza. Kwa hiyo kuzorota kwa mtt sio lazima iwe misuse ya mama
 
Last edited by a moderator:
Haahahaaaaaaaa! Wanaume kwa roho za mchongoma siwawezi. Basi kuwa hutoi cash, kama lukuunapeleka luku, maziwa unanunua kabisa, nepi, pampers, unga, mafuta, kila kitu, nguo, sabuni, maji yaani hadi chumvi na sukari. kAMA ADA UNALIPA KABISAA. Unahakikisha hali senti tano yako.

Atakula ugali na umeme atatumia... kama ingekua inawezekana angeweka password kwenye kila kitu halafu awe amempa neno la siri mtoto
 
ahahahaa...mshkaji utakuwa umekosea aisee...mie naamini ulitaka kuandika usd 500 kwa mwezi...

ila kama kweli unatoa tshs 500 kwa mwezi na mwanamke ananawiri na kupendeza basi jua kuna mtu mwingine kabisaaa anamuhudumia....pia amini kabisa kuwa huyo mtoto sio wako...wewe utakuwa baba mzazi ila kuna baba mlezi anakulelea mtoto uliyechangia mbegu...

kuwa makini huko mbeleni watoto wa aina hiyo kuwakataa nyie kina "baba wa mbegu" wala huwa sio ishu kabisaa......yani unamlea mtoto kwa jero kisha unakuja kulalamika kwa wanaume wenzio...kweli?

nipe namba ya huyo mkeo niwe namtumia tsh 1000 kila siku la kukulelea mwanao. wewe hilo jero lako kaa nalo nunulia vocha ujiunge kifurushi cha chuo, kisha punguza hasira juu ya mtalaka wako kunenepa na kupendeza maana atakuwa hali vyako na mwanao pia atanenepa kwakuwa atakuwa anakula mali za kaka yako mkubwa.

sawa dogo?
 
ahahahaa...mshkaji utakuwa umekosea aisee...mie naamini ulitaka kuandika usd 500 kwa mwezi...

ila kama kweli unatoa tshs 500 kwa mwezi na mwanamke ananawiri na kupendeza basi jua kuna mtu mwingine kabisaaa anamuhudumia....pia amini kabisa kuwa huyo mtoto sio wako...wewe utakuwa baba mzazi ila kuna baba mlezi anakulelea mtoto uliyechangia mbegu...

kuwa makini huko mbeleni watoto wa aina hiyo kuwakataa nyie kina "baba wa mbegu" wala huwa sio ishu kabisaa......yani unamlea mtoto kwa jero kisha unakuja kulalamika kwa wanaume wenzio...kweli?

nipe namba ya huyo mkeo niwe namtumia tsh 1000 kila siku la kukulelea mwanao. wewe hilo jero lako kaa nalo nunulia vocha ujiunge kifurushi cha chuo, kisha punguza hasira juu ya mtalaka wako kunenepa na kupendeza maana atakuwa hali vyako na mwanao pia atanenepa kwakuwa atakuwa anakula mali za kaka yako mkubwa.

sawa dogo?

500,000
 
hiyo hela unayotoa ni nyingi sanaaaa kama mtoto hajafikia umri wa kusoma. Na kama mmekubaliana ustawi wa jamii kwa maandishi ni ngumu kuacha kumpa hizo hela na uliyofanyiwa ni makubwa kwanza kwa mimi ningemuua kabisa huyo mwanamke tena kimya kimya . Nadhani utumie mbinu yeyote umchukue mtoto. Niliwahi kuwa na kesi kama yakwako mimi niliweza kumchukua mtoto maana mwanamke aliamua kuishi na mwanaume mwingine so ustawi wa jamii wakazingatia hilo wakanipa mtoto nashukuru Mungu kwa sasa ana miaka nane. Pole sana mkuu kwa Troumer unayopata hasa ikifika mwisho wa mwezi.
 

kweli mkuu lazima uwe na hasira...kwahiyo ulikubali kumlipia kodi ya nyumba tsh 100,000/= matumizi kwa mwezi tshs 200,000/=, pesa ya house girl tsh 50,000/= matibabu tsh 100,000/= na pesa ya bia kwa mama wa mtoto tshs 50,000/= KWA KILA MWEZI. ulipata bonge la gold n diamond digger.

unahitaji kufanya UMAFIA ili sheria ikuruhusu kumchukua mwanao umlee mwenyewe la sivyo nakuona unavyoumizwa na huyo mtaka vyote kwa pupa akaishia kukosa sasa anakuegeme wewe.
 
Back
Top Bottom