Nataka kumuhudumia mtoto peke yake

Nataka kumuhudumia mtoto peke yake

Nipeni ushauri jinsi ya kumuhudumia mtoto bila mama yake kunufaika make sitaki huyu mwanamke aonje pesa zangu ninazotoa kwa ajili huyo mtoto.

tangu nianze kutoa gharama za matunzo huyu mwanamke anazidi tu kunawiri inaniuma sana.

Umetafuta kwanza siri ya kunawili kwake? Isijekuwa kwa sasa ana-peace of mind kwa wewe kutoa huduma kwa mtoto, halafu mtoto ni mbishi kula.
 
Nitakuwa wa mwisho kukurushia jiwe hadi nitapojua kwa nini unasema hivyo???maumivu ya mahusiano huwa hakuna anayeweza kuyahimili kwa usahihi zaidi yako uliyeumizwa
 
Na uelewa wangu wanawake wengi wameichangia kwa kuropoka na kutoa maneno ambayo hawakustahili kutoa.

Hii yote inaonyesha ni jinsi gani,huwa mnafanya vitu ambavyo unahisi kuwa utamkomesha mwanaume wako kwa kuwa umezaa nae.

Kwa uelewa wangu mwenzetu amepata tatizo na mzazi mwenzake ameondoka na mtoto.hvyo anatafuta njia ambayo anaweza kumuhudumia mtoto wake moja kwa moja,na hapendi huyo mwanamke apate mwanya wa kuonja hiyo hudumua.yupo sahihi na ndio maana amewashikisha kuomba ushauri.

Ntatoa mfano mmoja

Kuna rafiki yangu mmoja alikuwa ameoa na alikuwa na maisha ya kawaida tuu.wakabahatika kupata mtoto mmoja.baada ya familia kukua na majukumu yakaongezeka.matokeo yake uchumi ukaporoka na kilichotokea yule mwanamke aliondoka na mtoto.

Yule mwanamke alipata bwana akamuona mumewe sio kitu hvyo akamuacha tena alimuacha kwa kashfa nyingi na maneno ya kumdhalilisha.yule rafiki yangu akapambana na mpaka sasa maisha yamerudi kwenye mstari.

Kilichotokea sasa yule mwanamke ameanza kumfatafata na kuanza kyomba fedha za matumizi kuwa analea mtoto.

Mpaka hapo nikajiuliza kuwa alivyoondoka nae alijua nani atamlea na fedha za matumizi mwanzo alipata wapi.

Kwa mfano huo nahisi mwomba ushauri nae anatatizo kama hilo au linalofanana.cha msingi ni kumpa ushauri tuu sio kutoa kauli mbovu.

Na nyie wanawake mnaoropoka tuu bila kufikiria wakati muda huo nyie ndio mnafanya maamuzi bila kufikiria nyuma kwa kuwa huwa mnaona mbele tuu mpunguze viherehere na maneno ya kuropoka.
 
Kuna watu wana roho mbaya. Pamoja na kukupa mtoto bado humthamini duh
 
Wanawake huwa wanaondoka na maneno ambayo yanaweza kukufanya ukachukia wanawake wote kama una roho nyepesi.

Kejeli,dharau na masimamgo ni baadhi tuu na kiukweli wanaume wengi wanakutwa na haya kila siku.

Kwa ushauri wanguu tuuu wewe nunua vitu peleka kwa mwanao,pia jukumu la kulea mtoto ni baba na mama.
 
pakaywatek

Huwezi kumweka mfanyakazi wa kukulea mwanao bila kumlipa.

Na huwezi pia kuhudumia mtoto kwa pesa tu.

Huyo mama alikwambia ana shida ya pesa yako?

Si umchukuwe umhudumie wewe? kinakushinda nini?

Watu kama wewe ndiyo wanafanya watoto wa mitaani waongezeke.

Punguani wahed.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: J33
pakaywatek;

Duu hii roho mbaya umeipata wapi? Yani umesahau kama na wewe pia umezaliwa na mwanamke? Ivi Unajua thamani Ya mwanamke? Unampenda mzazi wako? Mwanamke amekuzalia Mtoto sasa unaitwa Dad, huyo hata iweje heshima Yake iwepo na ndio mlezi wa mtoto Wako, usiwe na roho mbaya Chakula ni Kitu kidogo sana toa na mungu ata kuongezea...
 
Last edited by a moderator:
pakaywatek

Mkuu umenichekesha sana duh!!... Lakini naona wananchi wanakushambulia bila ya kujua kwa nini umeamua hivyo. Mimi nilikua napeleka matumizi lakini matokeo yake ananitangaza sipeleki.

Mtoto anakonda yeye ananenepa. Nilipomchukua mtoto akaona ile pesa haipati akaja kumchukua. Hivi viumbe unaweza ukavichukia hadi watu wengine wakashangaa. Lakini ambaye anakushambulia hapa yeye hayajamkuta
 
Last edited by a moderator:
Kuwa unamtumia mtoto hela mwenyewe. Mwambie chakula awe anakula hotelini tu, nguo zake apeleke kwa dobi, kuoga awe anaoga kwa jirani sabuni ikibaki anaficha, mafuta yake na vikorokoro vingine viwe vinakaa kwa jirani ili mama yake hata mafuta ya mgando asije akafaidi!!!
 
Mkuu umenichekesha sana duh!!... Lakini naona wananchi wanakushambulia bila ya kujua kwa nini umeamua hivyo. Mimi nilikua napeleka matumizi lakini matokeo yake ananitangaza sipeleki. Mtoto anakonda yeye ananenepa. Nilipomchukua mtoto akaona ile pesa haipati akaja kumchukua. Hivi viumbe unaweza ukavichukia hadi watu wengine wakashangaa. Lakini ambaye anakushambulia hapa yeye hayajamkuta

Kwahiyo unamaanisha mtoto kwa mama yake hali?

Watu msiwe mnaongozwa na hisia kuongea tu ilimradi. Alivyokaa kwako amenenepa? Alivyorudi kwa mama yake ameanza kukonda tena? Mtoto alivyoondoka mama alikonda? Unaweza usijibu ukweli hapa, ila kuwa mkweli kwenye nafsi yako!!!
 
Kwahiyo unamaanisha mtoto kwa mama yake hali?

Watu msiwe mnaongozwa na hisia kuongea tu ilimradi. Alivyokaa kwako amenenepa? Alivyorudi kwa mama yake ameanza kukonda tena? Mtoto alivyoondoka mama alikonda? Unaweza usijibu ukweli hapa, ila kuwa mkweli kwenye nafsi yako!!!

Nisingezungumza haya kama sina ushahidi wewe ndo naona unasema tu as if ulikuwepo au unamjua. Hapa kila mtu anaeleza experience yake na namna anavyoliona jambo. Anyway sishangai mana inaonyesha ndio nyie wote. Hivi kwanza unafahamu mtoto akiwa na umri fulani pia anatakia kufikia kilo fulani? Haya ninayo yazungumza nayafahamu ndio maana nikatoa ushuhuda wangu.
 
Mkuu, chukua mwanao na utafute msaidizi wa kumuhudumia na kwakua mtoto ni mmoja haita kusumbua.
Mimi niliwachukua wakwangu wakiwa na miezi 6, tena walikua mapacha. Nilitafuta msaidizi wa kuwahudumia na nilichokifanya ni kumlipa ujira mzuri na vijizawadi vya hapa na pale. Nilijitahidi kuwa karibu na wanangu na nili hakikisha navunja ratiba zisizo mashiko ili nipate muda wa kutosha kua nao.
Leo wamekua, wana umri wa miaka 11. Wanajitambua na hawajawahi kuwaza kitu mama.
 
pakaywatek

Kubaliana na hali maana chochote utakachokitoa lazima kifikie mikononi mwake, labda km mtoto ana umri wa miaka 7 unaweza kwenda muomba umlee au km hajafikisha na mama yake hana maadili mema ya kumlea au kumjenga vizuri mtoto nenda mahakamani ukaiombe ikupe rukhusa ya kumchukua na kumlea mtoto km utairidhisha.
 
Last edited by a moderator:
hamuwez kujua uyo mwanamke amemfanya nn jamaa msi hukumu...mm kid wangu nilimchukua nakaa nae ila mama ake stak ata kumsikia

Mi mwanamke mishenzi tu. linakutegeshea mimba halafu linataka ulee mtoto na ulilee lenyewe. Hata mie ningefanya kama wewe
 
Mi mwanamke mishenzi tu. linakutegeshea mimba halafu linataka ulee mtoto na ulilee lenyewe. Hata mie ningefanya kama wewe

Wakati unamtia hakua mshenzi? Kama umetia mshenzi nawewe ni mshenzi tu. Ndege wanaofanana
 
Mi mwanamke mishenzi tu. linakutegeshea mimba halafu linataka ulee mtoto na ulilee lenyewe. Hata mie ningefanya kama wewe

Wengi wanalia kutopata watoto kwny ndoa zako wengine mnakashifu kupata mwanamke alokuzalia mtoto?

"Wonders will Never End"
 
hamuwez kujua uyo mwanamke amemfanya nn jamaa msi hukumu...mm kid wangu nilimchukua nakaa nae ila mama ake stak ata kumsikia

freddie;
Ulipo likuta hilo ---- lako tena kicheche asiyejua kutunza wala asiye na upendo kwa mtoto ati unajitapa kuwa ulimchukua mwanao hukutaka mamake ale senti yako. Ulimwengu huu umejaa maajab. Unaijua sheria ya nchi weye? Mtoto ni wa mamake mpaka afikie 18 je huyo wako ni zaidi ya 18??? Funga domo lako asije pitia tu humu jf kwa bahati mbaya akakurudi bro.
Back to yu mleta hoja;
Acha kabisa roho mbaya hiyo. Mtoto hawezi kula peke yake mama asile hata siku moja. Alipokuwa anamnyonya mamake mbona hukulalamika kuwa asimnyonyeshe mwanao?
Ati unasema huyo mama ananenepeana, acha wenzio wafaidi. Ganda la muwa la jana, chungu ajionee kivuno. Tena mitaani wana kausemi; Ukisusa wenzio twala. Kama ni nini, kamchukue mwanao, peleka hoteli asubuhi, mchana, jioni, mwogeshe, mlishe, arudi kuja kulala na mamake.
Usisikilize ujinga wa watu. Sheria haikuachii
 
Back
Top Bottom