Kuna makabila hapa TZ ambayo kiutamaduni kama mke wa kijana wao anajifungua, basi kijana atampeleka mkewe kwa wazazi wake(wazazi wa mke) ili akale uzazi huko. But gharama zote zitakuwa juu ya mume na familia ya mume! Kwa maana hiyo, binti atakula uzazi kwa mama yake mzazi na sio kwa mama mkwe wake!
Huu uzi umenionyesha kwamba huu ndio utamaduni mzuri!...yaani wakati wa uzazi binti aende kwa wazazi wake waliomzaa kwani huko atajisikia huru zaidi kuliko kwa mama mkwe!
Mkuu sasa utaacha wangapi, Kumbuka Mama yeye tayari ana familia yake na wewe hii ndio familia yako inatakiwa uilinde kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote na ikiwezekana kwa dam yako. leo unamwacha mke na mtoto fikilia dingi na yeye angekufanyia hivyo those days wewe bado kadogo. Ndoa ni ya watu wawili. ndugu hawahusiki kabisa kwa sababu mwisho wa siku watoto wale ni wako si wa ndugu zako. Sikatai ndoa huwa zinavunjika lakini isivunjike kwa sababu ya ndugu kuwe na sababu zenu tu.
Mkuu, Niamini wadada zetu hawa ni hulka tofauti kuliko tunavyo dhania "me" kumradhi mkuu jaribu uchukwe mapumziko nje ya mji wako....na ufikirie kichangaa chako pia!! Kwani makosa yasiyo na taathira huwa ni kadhia nyepesi la kupotezeka tu!! Tena unaweza tumia wakat i wa mbele huko kumkanya.... siyo instant (hapohapo) utaharibu kwako!!
Poleni...
Na huu
Hebu kaa nae chini uzungumze nae..na umueleze ukweli alipo kosea na ikiwezekana ajirekebishe na akaombe msamaha! Naona kama umeharakisha sana labda kama hii si sababu ya pekee!Unajuaje hayo matatizo hayaku sababishwa na hali yake?
Yani unataka kuvunja ndoa kwa sababu rahisi namna hii? Mbona ndoa yenu inarekebishika kama sababu ni hii pekee? Tafuta wakubwa wako ,baba,mama na wakwe na mkeo mkae muongee myamalize! Kuvunja ndoa si rahisi namna hii..hatu ukienda popote wata shangaa sana kama hii ndio sababu!
Hebu kaa na mkeo muongee hii ni sababu dhaifu sana kuvunja ndoa msamehe msonge mbele..yani nguvu uliyotumia kufunga ndoa ivunjwe kwa sababu hii?Utatumia miaka kumi kuvunja ndoa kwa sababu hii!
Kaa chini myaongee!
Hahahaaaaaaa hata huyu wangu kuna siku aliniambia "usithubutu kuniacha utakiona cha mtema kuni" hahahahahaaaaa miss chaga big 5
Nimetamani nikupe likes 10 hivi. Umesema vzr sana
Wanajamvi, ni kama wiki tatu hivi tumebahatika kupata mtoto wa kwanza lkn kabla wife hajifungua nilimpeleka kwa mama yangu kwaajili ya huduma baada ya kujifungua, ndo ilikua mara yake ya kwanza kwenda kuishi na mama mkwe, cha ajabu kwa kipindi chote alichokaa nae ameonesha utovu wa nidhamu mkubwa.
Hivyo nimedhamilia kuachananae muda tu atakapo pata nguvu. Hivyo wanaojua sheria za ndoa na jamii naomba mnijuze ni sheria gani inaweza kunibana ktk hayo maamuzi yangu.
Asante nawasilisha tafadhali.
OK sasa Mpendwa Fedy nimekupata... Haswa kuwa Mungu katuumba wanaume kuwa na Misuli,nguvu,Ukakamavu,ujasiri,uvumilivu nk nk!! na Kamuumba mwanamke kuwa na maneno (ulimi/mdomo mkali) na mbavu moja zaidi ya kulea kizazi chake!! Hivyo wee potezea..... hio siBig Deal!! ishi na familia yako vizuri..
Huyu mtu hajaja kutaka ushauri bali kaja kutujuza kuwa anataka kumwacha mkewe kisheria kwa hiyo mpeni anachostahili tu maana inaonesha maamuzi keshafanya na hataka suluhu.
Nimekaa nae mwaka na nusu, hatujafunga ndoa yoyote zaidi ya kumtolea mahali tu.
wakat unaoa uliomba ushaur humu jf..??
Khaaaaa kumbe hujamuoa mtt wa watu then waja kumsimanga..ushamfuuujaaaa ndo wataka kumuacha..simple muache mahari yako km unadhiki kaidai..ila km huna sepa...atapata mume mwingine wa kumuoa atayemjali na kumpenda
We ushapata demu mwingine huna lolote
Km ni kuoa ungeshaoa
Tumeshakuona we kumbe si muoaji
Walipa mahali then wamfuja mwaka na nusu.??
You were never a husband material