Nataka kumuacha mke wangu

mwenzangu kama amezidi bwaga manyanga......wote tuna tabia mbaya ila wengine ni extreme....anayway mie nakubaliana na huyo aliesema mkae ndugu wa pande zote mbili mtafute suluhu ikishindikana ndio muachane,ila umetuambia udhaifu wa mkeo, wa mama yako unaujua??? au ndio unakuwa loyal hata kama unajua kabisaa mama yako ndie chanzo hapa?:lol::lol::lol::lol:
 
Siku nyingine ukitulia unaandika mambo ya maana sana yaliyojaa hekima na busara tele. Sijui kwanini hupenda kujitoa ufahamu ulionao.

 

Asante kwa muda wako, hii nimei-note mahali kwaajili ya reference baadae
 

Excellent!
 
Kwenda zako ukute mama yako ndio moto anauwasha ukiwa haupo ukiwepo anauzima,mama wakwe na wifi hua na midomo sana hata wake pia sikatai

Hapa naona unajaji kwa kutumia general concept, Tafadhali ukipata muda naomba upitie post chache za nyuma, unaweza kupata picha.
 
we una sababu zako tu zingine
iyo unayotwambia siyo sababu ya kumuacha mke
hata mahakama aiwezi kutoa talaka kwa sababu kama yako
labda umwache kienyeji lakini kisheria ngumu

Ntarudi kwako baada ya siku mbili au tatu acha niingie chimbo kwanza
 
Sawa weka hapa watu wakusome Mkuu, usikimbilie kuvunja ndoa kirahisi rahisi. Mke haachwi kwa kosa moja.

Nimeshafunguka kwenye post za nyuma ngoja ni copy na kupest kwako
 
nyie hamjui wanawake wenye midomo walivyo eeh
mimba kisingizio tu
mimi nkibeba mimba nakuaga kisirani nagombana na mme kila mda hadi nyumba nahama simtaki
ila si kufkia kutukana wakubwa zangu jamani
mnatetea ujinga!! hv wangetukanwa wazazi wenu mngejiskiaje...?!!
 
Ulioa kwa ajili ya mama yako? Acha ufala

Hebu Jaribuni kuwa waungwana. Kwani hata kama hajaona kwa ajili ya mama yake ndio aone mama yake anatukanwa afurahie? Mnachokifanya ni kujaribu kuinusuru ndoa ya mwenzenu sio kitu kibaya ni sawa kabisa ingawaje hajaomba ushauri isipokuwa ameuliza sheria inasemaje katika hilo la kumuacha mke kwa makosa aliyoyataja.

Jambo alilolifanya mkeo kweli sio la busara kabisa. Maana wote wenye akili timamu tunaelewa kuwa mzazi wa mwenzio ni kama mzazi wako kwa hiyo unatakiwa kumpa heshima tena ya ziada. Na ili familia yako iwe na amani ni lazima heshima iwepo. Je mapenzi yatatoka wapi utakapoona mama yako anatusiwa mbele yako? Lazima tukubaliane kuwa alilolifanya sio jambo jema.

Kama mtaombana msamaha ni sawa. Lakini pia kwenda kumwangukia mkwewe ni lazima.

Lakini pia ukimuacha sitashangaa kwa kuwa yapo mengi ambayo umesema mkeo ameyafanya lakini hujayaweka wazi hiyo ni kutokana na sababu unazozijua mwenyewe. Lakini katika kufanya maamuzi hayo pia uwe makini ukizingatia vigezo vyote vilivyopo na vile vile hakikisha umejua sheria inasemaje.

Ushauri wangu kwa wanawake: tubadilike zamani wanaume ndio walikuwa wana kila sifa mbaya unazozijua lakini sasa hivi ni wanawake. Wanawake tumekuwa tunajiamini sana hasa tunapokuwa tayari tumeingia katika ndoa ndio mtu anafyatua kucha alizokuwa amezificha.

Na wachangiaji mada hebu someni mada kwa ufasaha kabla hujachangia uelewe kwanza. Sio watu wanaropoka tu.
 
hiyo tabia aliyoionesha huwa ni kipindi alichokuwa na mimba tu au hata kabla?
 

Nathamini sana muda wako ulioutumia kuandika post hii ndefu na iliyo pangika vizuri, nashukuru pia kwa umakini wako katika kutambua nn kinahitajika lakini pia kunisaidia kutoa darasa kwa wengine, hapa kuna kitu cha kujifunza ingawaje wengi mnaniona -----
 
hiyo tabia aliyoionesha huwa ni kipindi alichokuwa na mimba tu au hata kabla?

Hata kabla ya hiyo mimba alishaanza kunivunjia heshima mm kwa domo lake chafu
 
For real?!!! Unataka kumuacha mkeo kwa ajili ya niniiii? Hebu kwanza nenda soma wamama wajawazito wanapitia vitu gani wakiwa kwenye hiyo hali, no wonder mama yako hakusema kitu sababu naye aliishapitia wakati kakubeba wewe. Acha ujinga, unless una yako mengine unamtafutia sababu. Duhhh, hii ya leo kali.
 
Tukikuelekeza namna ya kumuacha huyo wa kwanza ndiyo itakuwa muendelezo kwa watakaofuata,hutooa tena au
nawe utajirudisha kwa wazazi wako mkuu?
 
Una lako jambo. Inaonekana wewe ndio mwenye domo chafu, inawezekana hata ulikua humjali huyo mzazi mwenzako...mfewwww.

Nashukuru kwakua enapata majibu mwenyewe kadri unavyo zidi kusoma hiz post. Endelea kusoma kisha karibu tena kwa post ingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…