Shomari
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 1,112
- 241
Jamani wanajukwaa wenzangu. kwanza kabisa asalaam alaykum pia bwana yesu asifiwe sana. Mimi nina nia ya kuanzisha biashara ya upigaji picha katika maeneo ya jiji la Mwanza. kuna mtu yeyote mwenye uzoefu anayeweza kuniambia itanigharimu kiasi gani kufungua studio ya kisasa kabisa, na ni vifaa gani hasa ambavyo ninatakiwa niwe navyo?. natanguliza shukrani zangu za dhati.